Swahili: New Testament

Croatian

Mark

6

1Yesu aliondoka hapo akaenda katika kijiji chake, akifuatwa na wanafunzi wake.
1I otišavši odande, dođe u svoj zavičaj. A doprate ga učenici.
2Siku ya Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika sunagogi. Wengi waliomsikia walishangaa, wakasema, "Je, ameyapata wapi mambo haya? Ni hekima gani hii aliyopewa? Tena, anatendaje maajabu haya anayoyafanya?
2I kada dođe subota, poče učiti u sinagogi. I mnogi što su ga slušali preneraženi govorahu: "Odakle to ovome? Kakva li mu je mudrost dana? I kakva se to silna djela događaju po njegovim rukama?
3Je, huyu si yule seremala mwana wa Maria, na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simoni; Je, dada zake si wanaishi papa hapa kwetu?" Basi, wakawa na mashaka naye.
3Nije li ovo drvodjelja, sin Marijin, i brat Jakovljev, i Josipov, i Judin, i Šimunov? I nisu li mu sestre ovdje među nama?" I sablažnjavahu se o njega.
4Yesu akawaambia, "Nabii hakosi heshima isipokuwa katika nchi yake, kwa jamaa zake na nyumbani mwake."
4A Isus im govoraše: "Nije prorok bez časti doli u svom zavičaju i među rodbinom i u svom domu."
5Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache, akawaponya.
5I ne mogaše ondje učiniti ni jedno čudo, osim što ozdravi nekoliko nemoćnika stavivši ruke na njih.
6Alishangaa sana kwa sababu ya kutoamini kwao. Kisha Yesu alivitembelea vijiji vya pale karibu akiwafundisha watu.
6I čudio se njihovoj nevjeri. Obilazio je selima uokolo i naučavao.
7Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawiliwawili. Aliwapa uwezo wa kuwatoa pepo wachafu,
7Dozva dvanaestoricu te ih poče slati dva po dva dajući im vlast nad nečistim dusima.
8na kuwaamuru, "Msichukue chochote mnapokwenda isipokuwa fimbo tu. Msichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni.
8I zapovjedi im da na put ne nose ništa osim štapa: ni kruha, ni torbe, ni novaca o pojasu,
9Vaeni viatu lakini msivae kanzu mbili."
9nego da nose samo sandale i da ne oblače dviju haljina.
10Tena aliwaambia, "Popote mtakapokaribishwa nyumbani, kaeni humo mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
10I govoraše im: "Kad uđete gdje u kuću, u njoj ostanite dok ne odete odande.
11Mahali popote ambapo watu watakataa kuwakaribisheni au kuwasikiliza, ondokeni hapo na kuyakung'uta mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao."
11Ako vas gdje ne prime te vas ne poslušaju, iziđite odande i otresite prah ispod svojih nogu njima za svjedočanstvo."
12Basi, wakaondoka, wakahubiri watu watubu.
12Otišavši, propovijedali su obraćenje,
13Waliwafukuza pepo wengi wabaya; wakawapaka mafuta wagonjwa wengi, wakawaponya.
13izgonili mnoge zloduhe i mnoge su nemoćnike mazali uljem i oni su ozdravljali.
14Basi, mfalme Herode alisikia juu ya hayo yote, maana sifa za Yesu zilienea kila mahali. Baadhi ya watu walikuwa wakisema, "Yohane Mbatizaji amefufuka kutoka wafu, ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
14Dočuo to i kralj Herod jer se razglasilo Isusovo ime te se govorilo: "Ivan Krstitelj uskrsnuo od mrtvih i zato čudesne sile djeluju u njemu."
15Wengine walisema, "Mtu huyu ni Eliya." Wengine walisema, "Huyu ni nabii kama mmojawapo wa manabii wa kale."
15A drugi govorahu: "Ilija je!" Treći opet: "Prorok, kao jedan od proroka."
16Lakini Herode alipopata habari hizi alisema, "Huyu ni Yohane! Nilimkata kichwa, lakini amefufuka."
16Herod pak na to govoraše: "Uskrsnu Ivan kojemu ja odrubih glavu."
17Hapo awali Herode mwenyewe alikuwa ameamuru Yohane atiwe nguvuni, akamfunga gerezani. Herode alifanya hivyo kwa sababu ya Herodia ambaye Herode alimwoa ingawaje alikuwa mke wa Filipo, ndugu yake.
17Herod doista bijaše dao uhititi Ivana i svezati ga u tamnici zbog Herodijade, žene brata svoga Filipa, kojom se bio oženio.
18Yohane alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kumchukua mke wa ndugu yako."
18Budući da je Ivan govorio Herodu: "Ne smiješ imati žene brata svojega!",
19Basi Herodia alimchukia sana Yohane, akataka kumwua, asiweze.
19Herodijada ga mrzila i htjela ga ubiti, ali nije mogla
20Herode alimwogopa Yohane kwa maana alijua kwamba yeye ni mtu mwema na mtakatifu, na hivyo akamlinda. Herode alipenda kumsikiliza Yohane, ingawaje baada ya kumsikiliza, alifadhaika sana.
20jer se Herod bojao Ivana; znao je da je on čovjek pravedan i svet pa ga je štitio. I kad god bi ga slušao, uvelike bi se zbunio, a rado ga je slušao.
21Ikapatikana nafasi, wakati wa sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode. Herode aliwafanyia karamu wazee wa baraza lake, majemadari na viongozi wa Galilaya.
21I dođe zgodan dan kad Herod o svom rođendanu priredi gozbu svojim velikašima, časnicima i prvacima galilejskim.
22Basi, binti yake Herodia aliingia, akacheza, akawafurahisha sana Herode na wageni wake. Mfalme akamwambia huyo msichana, "Niombe chochote utakacho, nami nitakupa."
22Uđe kći Herodijadina i zaplesa. Svidje se Herodu i sustolnicima. Kralj reče djevojci: "Zaišti od mene što god hoćeš i dat ću ti!"
23Tena akamwapia, "Chochote utakachoniomba, nitakupa: hata ikiwa ni nusu ya ufalme wangu."
23I zakle joj se: "Što god zaišteš od mene, dat ću ti, pa bilo to i pol mojega kraljevstva."
24Hapo huyo msichana akatoka, akamwuliza mama yake, "Niombe nini?" Naye akamjibu, "Kichwa cha Yohane mbatizaji."
24Ona iziđe pa će svojoj materi: "Što da zaištem?" A ona će: "Glavu Ivana Krstitelja!"
25Msichana akamrudia mfalme mbio akamwomba, "Nataka unipe sasa hivi katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
25I odmah žurno uđe kralju te zaište: "Hoću da mi odmah dadeš na pladnju glavu Ivana Krstitelja!"
26Mfalme akahuzunika sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake, na kwa ajili ya wale wageni wake karamuni, hakutaka kumkatalia.
26Ožalosti se kralj, ali zbog zakletve i sustolnika na htjede je odbiti.
27Basi, mfalme akamwamuru askari kukileta kichwa cha Yohane. Askari akaenda, akamkata kichwa Yohane mle gerezani,
27Kralj odmah posla krvnika i naredi da donese glavu Ivanovu. On ode, odrubi mu glavu u tamnici,
28akakileta katika sinia, akampa msichana naye msichana akampa mama yake.
28donese je na pladnju i dade je djevojci, a djevojka materi.
29Wanafunzi wa Yohane walipopata habari, walikwenda wakachukua mwili wake, wakauzika kaburini.
29Kad za to dočuše Ivanovi učenici, dođu, uzmu njegovo tijelo i polože ga u grob.
30Wale mitume walirudi, wakakusanyika mbele ya Yesu wakamwarifu yote waliyotenda na kufundisha.
30Uto se apostoli skupe oko Isusa i izvijeste ga o svemu što su činili i naučavali.
31Alisema hivyo kwa kuwa kulikuwa na watu wengi mno walikuwa wanafika hapo na kuondoka hata Yesu na wanafunzi wake hawakuweza kupata nafasi ya kula chakula. Basi, Yesu akawaambia, "Twendeni peke yetu mahali pa faragha kula chakula, mkapumzike kidogo."
31I reče im: "Hajdete i vi u osamu na samotno mjesto, i otpočinite malo." Jer mnogo je svijeta dolazilo i odlazilo pa nisu imali kada ni jesti.
32Basi, Wakaondoka peke yao kwa mashua, wakaenda mahali pa faragha.
32Otploviše dakle lađom na samotno mjesto, u osamu.
33Lakini watu wengi waliwaona wakienda, wakawatambua. Hivyo wengi wakatoka katika kila mji, wakakimbilia huko Yesu na wanafunzi wake walikokuwa wanakwenda, wakawatangulia kufika.
33No kad su odlazili, mnogi ih vidješe i prepoznaše te se pješice iz svih gradova strčaše onamo i pretekoše ih.
34Waliposhuka pwani, Yesu aliona umati mkubwa wa watu, akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji. Akaanza kuwafundisha mambo mengi.
34Kad iziđe, vidje silan svijet i sažali mu se jer bijahu kao ovce bez pastira pa ih stane poučavati u mnogočemu.
35Saa za mchana zilikwisha pita. Basi, wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwambia, "Hapa ni nyikani, na sasa kunakuchwa.
35A u kasni već sat pristupe mu učenici pa mu reknu: "Pust je ovo kraj i već je kasno.
36Afadhali uwaage watu waende mashambani na katika vijiji vya jirani, wanunue chakula."
36Otpusti ih da odu po okolnim zaseocima i selima i kupe sebi što za jelo."
37Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Nao wakamwuliza, "Je, twende kununua mikate kwa fedha dinari mia mbili, na kuwapa chakula?"
37No on im odgovori: "Podajte im vi jesti." Kažu mu: "Da pođemo i kupimo za dvjesta denara kruha pa da im damo jesti?"
38Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame." Walipokwisha tazama, wakamwambia, "Kuna mikate mitano na samaki wawili."
38A on će im: "Koliko kruhova imate? Idite i vidite!" Pošto izvidješe, kažu: "Pet, i dvije ribe."
39Basi, Yesu akawaamuru wanafunzi wawaketishe watu wote makundimakundi penye nyasi.
39I zapovjedi im da sve, u skupinama, posjedaju po zelenoj travi.
40Nao wakaketi makundimakundi ya watu mia moja na ya watu hamsini.
40I pružiše se po sto i po pedeset na svaku lijehu.
41Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akaimega mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu. Na wale samaki wawili pia akawagawia wote.
41On uze pet kruhova i dvije ribe, pogleda na nebo, izreče blagoslov pa razlomi kruhove i davaše učenicima da posluže ljude. Tako i dvije ribe razdijeli svima.
42Watu wote wakala, wakashiba.
42I jeli su svi i nasitili se.
43Wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
43I od ulomaka nakupiše dvanaest punih košara, a i od riba.
44Nao waliokula hiyo mikate walikuwa wanaume elfu tano.
44A jelo je pet tisuća muškaraca.
45Mara Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie kwenda Bethsaida, ng'ambo ya ziwa, wakati yeye anauaga umati wa watu.
45On odmah prisili učenike da uđu u lađu i da se prebace prijeko, prema Betsaidi, dok on otpusti mnoštvo.
46Baada ya kuwaaga watu alikwenda mlimani kusali.
46I pošto se rasta s ljudima, otiđe u goru da se pomoli.
47Ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya ziwa, naye alikuwa peke yake katika nchi kavu.
47Uvečer pak lađa bijaše posred mora, a on sam na kraju.
48Basi, akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kupiga makasia, maana upepo ulikuwa unawapinga. Karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea akitembea juu ya maji. Alitaka kuwapita.
48Vidjevši kako se muče veslajući, jer im bijaše protivan vjetar, oko četvrte noćne straže dođe k njima hodeći po moru. I htjede ih mimoići.
49Lakini walimwona akitembea juu ya maji, wakadhani ni mzimu, wakapiga yowe.
49A oni, vidjevši kako hodi po moru, pomisliše da je utvara pa kriknuše.
50Maana wote walipomwona waliogopa sana. Mara Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
50Jer svi su ga vidjeli i prestrašili se. A on im odmah progovori: "Hrabro samo! Ja sam! Ne bojte se!"
51Kisha akapanda mashuani walimokuwa, na upepo ukatulia. Nao wakashangaa sana.
51I uziđe k njima u lađu, a vjetar utihnu. I veoma se, prekomjerno, snebivahu;
52maana hawakuwa bado wameelewa maana ya ile mikate. Akili zao zilikuwa bado zimepumbazika.
52još ne shvatiše ono o kruhovima, nego im srce bijaše stvrdnuto.
53Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.
53Pošto doploviše na kraj, dođu u Genezaret i pristanu.
54Walipotoka mashuani, mara watu wakamtambua Yesu.
54Kad iziđu iz lađe, ljudi ga odmah prepoznaju
55Basi, kwa haraka wakazunguka katika nchi ile yote, wakaanza kuwachukua wagonjwa wamelala juu ya mikeka yao, wakawapeleka kila mahali waliposikia Yesu yupo.
55pa oblete sav onaj kraj. I počnu donositi na nosilima bolesnike onamo gdje bi čuli da se on nalazi.
56Kila mahali Yesu alipokwenda, vijijini, mijini, au mashambani, watu waliwaweka wagonjwa uwanjani, wakamsihi waguse walau pindo la vazi lake. Nao wote waliomgusa walipona.
56I kamo bi god ulazio - u sela, u gradove, u zaseoke - po trgovima bi stavljali bolesnike i molili ga da se dotaknu makar skuta njegove haljine. I koji bi ga se god dotakli, ozdravljali bi.