1Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
1I kad Isus završi sve te besjede, reče svojim učenicima:
2"Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe."
2"Znate da je za dva dana Pasha, i Sin Čovječji predaje se da se razapne."
3Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
3Uto se sabraše glavari svećenički i starješine narodne u dvoru velikoga svećenika imenom Kajfe
4Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
4i zaključiše Isusa na prijevaru uhvatiti i ubiti.
5Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
5Jer se govorilo: "Nikako ne o Blagdanu da ne nastane pobuna u narodu."
6Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
6Kad je Isus bio u Betaniji, u kući Šimuna Gubavca,
7mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
7pristupi mu neka žena s alabastrenom posudicom skupocjene pomasti i polije ga po glavi, dok je on bio za stolom.
8Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, "Ya nini hasara hii?
8Vidjevši to, učenici negodovahu: "Čemu ta rasipnost?
9Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha."
9Moglo se to skupo prodati i dati siromasima."
10Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
10Zapazio to Isus pa im reče: "Što dodijavate ženi? Dobro djelo učini prema meni.
11Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
11Ta siromaha svagda imate uza se, a mene nemate svagda.
12Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
12Izlila je tu pomast na moje tijelo - za ukop mi to učini.
13Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye."
13Zaista, kažem vam, gdje se god bude propovijedalo ovo evanđelje, po svem svijetu, navješćivat će se i ovo što ona učini - njoj na spomen."
14Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
14Tada jedan od dvanaestorice, zvan Juda Iškariotski, pođe glavarima svećeničkim
15akawaambia, "Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?" Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
15i reče: "Što ćete mi dati i ja ću vam ga predati." A oni mu odmjeriše trideset srebrnjaka.
16na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
16Otada je tražio priliku da ga preda.
17Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, "Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?"
17Prvoga dana Beskvasnih kruhova pristupiše učenici Isusu i upitaše: "Gdje hoćeš da ti pripravimo te blaguješ pashu?"
18Yeye akawajibu, "Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu."
18On reče: "Idite u grad tomu i tomu i recite mu: 'Učitelj veli: Vrijeme je moje blizu, kod tebe slavim pashu sa svojim učenicima.'"
19Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
19I učine učenici kako im naredi Isus i priprave pashu.
20Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
20Uvečer bijaše Isus za stolom s dvanaestoricom.
21Walipokuwa wakila, Yesu akasema, "Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti."
21I dok su blagovali, reče: "Zaista, kažem vam, jedan će me od vas izdati."
22Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, "Bwana! Je, ni mimi?"
22Silno ožalošćeni, stanu mu jedan za drugim govoriti: "Da nisam ja, Gospodine?"
23Yesu akajibu, "Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
23On odgovori: "Onaj koji umoči sa mnom ruku u zdjelu, taj će me izdati.
24Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa."
24Sin Čovječji, istina, odlazi kako je o njemu pisano, ali jao čovjeku onomu koji predaje Sina Čovječjega. Tomu bi čovjeku bolje bilo da se ni rodio nije."
25Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, "Mwalimu! Je, ni mimi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
25A Juda, izdajnik, prihvati i reče: "Da nisam ja, učitelju?" Reče mu: "Ti kaza."
26Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni mle; huu ni mwili wangu."
26I dok su blagovali, uze Isus kruh, izreče blagoslov pa razlomi, dade svojim učenicima i reče: "Uzmite i jedite! Ovo je tijelo moje!"
27Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, "Nyweni nyote;
27I uze čašu, zahvali i dade im govoreći: "Pijte iz nje svi!
28maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
28Ovo je krv moja, krv Saveza koja se za mnoge prolijeva na otpuštenje grijeha.
29Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu."
29A kažem vam: ne, neću od sada piti od ovog roda trsova do onoga dana kad ću ga - novoga - s vama piti u kraljevstvu Oca svojega."
30Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
30Otpjevavši hvalospjeve, zaputiše se prema Maslinskoj gori.
31Kisha Yesu akawaambia, "Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
31Tada im reče Isus: "Svi ćete se vi još ove noći sablazniti o mene. Ta pisano je: Udarit će pastira i stado će se razbjeći.
32Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya."
32Ali kad uskrsnem, ići ću pred vama u Galileju.'
33Petro akamwambia Yesu "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe."
33Nato će mu Petar: "Ako se i svi sablazne o tebe, ja se nikada neću!"
34Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
34Reče mu Isus: "Zaista, kažem ti, još ove noći, prije negoli se pijetao oglasi, triput ćeš me zatajiti!"
35Petro akamwambia, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe." Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
35Kaže mu Petar: "Bude li trebalo i umrijeti s tobom, ne, neću te zatajiti." Tako rekoše i svi učenici.
36Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali."
36Tada dođe Isus s njima u predio zvan Getsemani i kaže učenicima: "Sjednite ovdje dok ja odem onamo pomoliti se."
37Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
37I povede sa sobom Petra i oba sina Zebedejeva. Spopade ga žalost i tjeskoba.
38Hapo akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami."
38Tada im reče: "Duša mi je nasmrt žalosna. Ostanite ovdje i bdijte sa mnom!"
39Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: "Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe."
39I ode malo dalje, pade ničice moleći: "Oče moj! Ako je moguće, neka me mimoiđe ova čaša. Ali ne kako ja hoću, nego kako hoćeš ti."
40Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, "Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
40I dođe učenicima i nađe ih pozaspale pa reče Petru: "Tako, zar niste mogli jedan sat probdjeti sa mnom?
41Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu."
41Bdijte i molite da ne padnete u napast! Duh je, istina, voljan, no tijelo je slabo."
42Akaenda tena mara ya pili akasali: "Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike."
42Opet, po drugi put, ode i pomoli se: "Oče moj! Ako nije moguće da me čaša mine da je ne pijem, budi volja tvoja!"
43Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
43I ponovno dođe i nađe ih pozaspale, oči im se sklapale.
44Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
44Opet ih ostavi, pođe i pomoli se po treći put ponavljajući iste riječi.
45Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, "Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
45Tada dođe učenicima i reče im: "Samo spavajte i počivajte! Evo, približio se čas! Sin Čovječji predaje se u ruke grešničke!
46Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti."
46Ustanite, hajdemo! Evo, približio se moj izdajica."
47Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
47Dok je on još govorio, gle, dođe Juda, jedan od dvanaestorice, i s njime silna svjetina s mačevima i toljagama poslana od glavara svećeničkih i starješina narodnih.
48Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni."
48A izdajica im dao znak: "Koga poljubim, taj je, njega uhvatite!"
49Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, "Shikamoo, Mwalimu!" Kisha akambusu.
49I odmah pristupi Isusu i reče: "Zdravo, Učitelju!" I poljubi ga.
50Yesu akamwambia, "Rafiki, fanya ulichokuja kufanya." Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
50A Isus mu reče: "Prijatelju, zašto ti ovdje!" Tada pristupe, podignu ruke na Isusa i uhvate ga.
51Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
51I gle, jedan od onih koji bijahu s Isusom maši se rukom, trgnu mač, udari slugu velikoga svećenika i odsiječe mu uho.
52Hapo Yesu akamwambia, "Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
52Kaže mu tada Isus: "Vrati mač na njegovo mjesto jer svi koji se mača laćaju od mača i ginu.
53Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
53Ili zar misliš da ja ne mogu zamoliti Oca svojega i eto umah uza me više od dvanaest legija anđela?
54Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?"
54No kako bi se onda ispunila Pisma da tako mora biti?"
55Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, "Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
55U taj čas reče Isus svjetini: "Kao na razbojnika iziđoste s mačevima i toljagama da me uhvatite? Danomice sjeđah u Hramu naučavajući i ne uhvatiste me."
56Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie." Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
56A sve se to dogodilo da se ispune Pisma proročka. Tada ga svi učenici ostave i pobjegnu.
57Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
57Nato uhvatiše Isusa i odvedoše ga velikomu svećeniku Kajfi, kod kojega se sabraše pismoznanci i starješine.
58Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
58A Petar je išao za njim izdaleka do dvora velikog svećenika; i ušavši unutra, sjedne sa stražarima da vidi svršetak.
59Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
59A glavari svećenički i cijelo Vijeće tražili su kakvo lažno svjedočanstvo protiv Isusa da bi ga mogli pogubiti.
60lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
60Ali ne nađoše premda pristupiše mnogi lažni svjedoci. Napokon pristupe dvojica
61wakasema, "Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu."
61i reknu: "Ovaj reče: 'Mogu razvaliti Hram Božji i za tri ga dana sagraditi.'"
62Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
62Usta nato veliki svećenik i reče mu: "Zar ništa ne odgovaraš? Što to ovi protiv tebe svjedoče?"
63Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, "Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!"
63Isus je šutio. Reče mu veliki svećenik: "Zaklinjem te Bogom živim: Kaži nam jesi li ti Krist, Sin Božji?"
64Yesu akamwambia, "Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni."
64Reče mu Isus: "Ti kaza! Štoviše, kažem vam: Odsada ćete gledati Sina Čovječjega gdje sjedi zdesna Sile i dolazi na oblacima nebeskim."
65Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, "Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
65Nato veliki svećenik razdrije haljine govoreći: "Pohulio je! Što nam još trebaju svjedoci! Evo, sada ste čuli hulu!
66Ninyi mwaonaje?" Wao wakamjibu, "Anastahili kufa!"
66Što vam se čini?" Oni odgovoriše: "Smrt zaslužuje!"
67Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
67Tada su mu pljuvali u lice i udarali ga, a drugi ga pljuskali
68wakasema, "Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!"
68govoreći: "Proreci nam, Kriste, tko te udario?"
69Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, "Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya."
69A Petar je sjedio vani u dvorištu. I pristupi mu jedna sluškinja govoreći: "I ti bijaše s Isusom Galilejcem."
70Petro akakana mbele ya wote akisema, "Sijui hata unasema nini."
70On pred svima zanijeka: "Ne znam što govoriš."
71Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, "Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti."
71Kad iziđe u predvorje, spazi ga druga i kaže nazočnima: "Ovaj bijaše s Isusom Nazarećaninom."
72Petro akakana tena kwa kiapo: "Simjui mtu huyo."
72On opet zanijeka sa zakletvom: "Ne znam toga čovjeka."
73Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, "Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha."
73Malo zatim nazočni pristupiše Petru i rekoše: "Doista, i ti si od njih! Ta govor te tvoj izdaje!"
74Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, "Simjui mtu huyo!" Mara jogoo akawika.
74On se tada stane zaklinjati i preklinjati: "Ne znam toga čovjeka." I odmah se oglasi pijetao.
75Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: "Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu." Basi, akatoka nje akalia sana.
75I spomenu se Petar riječi koju mu Isus reče: "Prije nego se pijetao oglasi, triput ćeš me zatajiti." I iziđe te gorko zaplaka.