Swahili: New Testament

Croatian

Matthew

27

1Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
1A kad objutri, svi su glavari svećenički i starješine narodne održali vijećanje protiv Isusa da ga pogube.
2Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
2I svezana ga odveli i predali upravitelju Pilatu.
3Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
3Kada Juda, njegov izdajica, vidje da je Isus osuđen, pokaja se i vrati trideset srebrnjaka glavarima svećeničkim i starješinama
4Akawaambia, "Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe." Lakini wao wakasema, "Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako."
4govoreći: "Sagriješih predavši krv nedužnu!" Odgovoriše: "Što se to nas tiče? To je tvoja stvar!"
5Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
5I bacivši srebrnjake u Hram, ode te se objesi.
6Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, "Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu."
6Glavari svećenički uzeše srebrnjake i rekoše:
7Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
7"Nije dopušteno staviti ih u hramsku riznicu jer su krvarina." Posavjetuju se i kupe za njih lončarovu njivu za ukop stranaca.
8Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
8Stoga se ona njiva zove "Krvava njiva" sve do danas.
9Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: "Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
9Tada se ispuni što je rečeno po proroku Jeremiji: Uzeše trideset srebrnjaka - cijenu Neprocjenjivoga kojega procijeniše sinovi Izraelovi -
10wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza."
10i dadoše ih za njivu lončarovu kako mi naredi Gospodin.
11Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, "Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamwambia, "Wewe umesema."
11Dovedoše dakle Isusa pred upravitelja. Upita ga upravitelj: "Ti li si kralj židovski?" On odgovori: "Ti kažeš."
12Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
12I dok su ga glavari svećenički i starješine narodne optuživale, ništa nije odgovarao.
13Hivyo Pilato akamwuliza, "Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?"
13Tada mu reče Pilat: "Ne čuješ li što sve protiv tebe svjedoče?"
14Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
14I ne odgovori mu ni na jednu riječ te se upravitelj silno čudio.
15Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
15A o Blagdanu upravitelj je običavao svjetini pustiti jednoga uznika, koga bi već htjeli.
16Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
16Tada upravo bijaše u njih poznati uznik zvani Baraba.
17Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, "Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?"
17Kad se dakle sabraše, reče im Pilat: "Koga hoćete da vam pustim: Barabu ili Isusa koji se zove Krist?"
18Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
18Znao je doista da ga predadoše iz zavisti.
19Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: "Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake."
19Dok je sjedio na sudačkoj stolici, poruči nu njegova žena: "Mani se ti onoga pravednika jer sam danas u snu mnogo pretrpjela zbog njega."
20Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
20Međutim, glavari svećenički i starješine nagovore svjetinu da zaište Barabu, a Isus da se pogubi.
21Mkuu wa mkoa akawauliza, "Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?" Wakamjibu, "Baraba!"
21Upita ih dakle upravitelj: "Kojega od ove dvojice hoćete da vam pustim?" A oni rekoše: "Barabu!"
22Pilato akawauliza, "Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?" Wote wakasema, "Asulubiwe!"
22Kaže im Pilat: "Što dakle da učinim s Isusom koji se zove Krist?" Oni će: "Neka se razapne."
23Pilato akauliza, "Kwa nini? Amefanya kosa gani?" Wao wakazidi kupaaza sauti: "Asulubiwe!"
23A on upita: "A što je zla učinio?" Vikahu još jače: "Neka se razapne!"
24Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, "Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe."
24Kad Pilat vidje da ništa ne koristi, nego da biva sve veći metež, uzme vodu i opere ruke pred svjetinom govoreći: "Nevin sam od krvi ove! Vi se pazite!"
25Watu wote wakasema, "Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!"
25Sav narod nato odvrati: "Krv njegova na nas i na djecu našu!"
26Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
26Tada im pusti Barabu, a Isusa, izbičevana, preda da se razapne.
27Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
27Onda vojnici upraviteljevi uvedoše Isusa u dvor upraviteljev i skupiše oko njega cijelu četu.
28Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
28Svukoše ga pa zaogrnuše skrletnim plaštem.
29Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, "Shikamoo mfalme wa Wayahudi!"
29Spletoše zatim vijenac od trnja i staviše mu na glavu, a tako i trsku u desnicu. Prigibajući pred njim koljena, izrugivahu ga: "Zdravo, kralju židovski!"
30Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
30Onda pljujući po njemu, uzimahu trsku i udarahu ga njome po glavi.
31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
31Pošto ga izrugaše, svukoše mu plašt, obukoše mu njegove haljine pa ga odvedoše da ga razapnu.
32Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
32Izlazeći nađu nekoga čovjeka Cirenca, imenom Šimuna, i prisile ga da mu ponese križ.
33Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la kichwa,"
33I dođoše na mjesto zvano Golgota, to jest Lubanjsko mjesto,
34wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
34dadoše mu piti vino sa žuči pomiješano. I kad okusi, ne htjede piti.
35Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35A pošto ga razapeše, razdijeliše među se haljine njegove bacivši kocku.
36Wakaketi, wakawa wanamchunga.
36I sjedeći ondje, čuvahu ga.
37Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, "Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi."
37I staviše mu ponad glave krivicu napisanu: "Ovo je Isus, kralj židovski."
38Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
38Tada razapeše s njime dva razbojnika, jednoga zdesna, drugoga slijeva.
39Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
39A prolaznici su ga pogrđivali mašući glavama:
40"Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!"
40"Ti koji razvaljuješ Hram i za tri ga dana sagradiš, spasi sam sebe! Ako si Sin Božji, siđi s križa!"
41Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
41Slično i glavari svećenički s pismoznancima i starješinama, rugajući se, govorahu:
42"Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
42"Druge je spasio, sebe ne može spasiti! Kralj je Izraelov! Neka sada siđe s križa pa ćemo povjerovati u nj!
43Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka."
43Uzdao se u Boga! Neka ga sad izbavi ako mu omilje! Ta govorio je: 'Sin sam Božji!'"
44Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
44Tako ga vrijeđahu i s njim raspeti razbojnici.
45Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
45Od šeste ure nasta tama po svoj zemlji - do ure devete.
46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eli, Eli, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
46O devetoj uri povika Isus iza glasa: "Eli, Eli, lema sabahtani?" To će reći: "Bože moj, Bože moj, zašto si me ostavio?"
47Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, "Anamwita Eliya."
47A neki od nazočnih, čuvši to, govorahu: "Ovaj zove Iliju."
48Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
48I odmah pritrča jedan od njih, uze spužvu, natopi je octom, natakne je na trsku i pruži mu piti.
49Wengine wakasema, "Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa."
49A ostali rekoše: "Pusti da vidimo hoće li doći Ilija da ga spasi."
50Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
50A Isus opet povika iz glasa i ispusti duh.
51Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
51I gle, zavjesa se hramska razdrije odozgor dodolje, nadvoje; zemlja se potrese, pećine se raspukoše,
52makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
52grobovi otvoriše i tjelesa mnogih svetih preminulih uskrsnuše
53nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
53te iziđoše iz grobova nakon njegova uskrsnuća, uđoše u sveti grad i pokazaše se mnogima.
54Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu."
54A satnik i oni koji su s njime čuvali Isusa vidješe potres i što se zbiva, silno se prestrašiše i rekoše: "Uistinu, Sin Božji bijaše ovaj."
55Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
55A bijahu ondje i izdaleka promatrahu mnoge žene što su iz Galileje išle za Isusom poslužujući mu;
56Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
56među njima Marija Magdalena i Marija, Jakovljeva i Josipova majka, i majka sinova Zebedejevih.
57Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
57Uvečer dođe neki bogat čovjek iz Arimateje, imenom Josip, koji i sam bijaše učenik Isusov.
58Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
58On pristupi Pilatu i zaiska tijelo Isusovo. Tada Pilat zapovjedi da mu se dadne.
59Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
59Josip uze tijelo, povi ga u čisto platno
60akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
60i položi u svoj novi grob koji bijaše isklesao u stijeni. Dokotrlja velik kamen na grobna vrata i otiđe.
61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
61A bijahu ondje Marija Magdalena i druga Marija: sjedile su nasuprot grobu.
62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
62Sutradan, to jest dan nakon Priprave, sabraše se glavari svećenički i farizeji kod Pilata
63Wakasema, "Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
63te mu rekoše: "Gospodaru, sjetismo se da onaj varalica još za života kaza: 'Nakon tri dana uskrsnut ću.'
64Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali."
64Zapovjedi dakle da se grob osigura sve do trećega dana da ne bi možda došli njegovi učenici, ukrali ga pa rekli narodu: 'Uskrsnuo je od mrtvih!' I bit će posljednja prijevara gora od prve."
65Pilato akawaambia, "Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo."
65Reče im Pilat: "Imate stražu! Idite i osigurajte kako znate!"
66Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
66Nato oni odu i osiguraju grob: zapečate kamen i postave stražu.