Swahili: New Testament

Croatian

Matthew

28

1Baada ya Sabato, karibu na mapambazuko ya siku ile ya Jumapili, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kutazama lile kaburi.
1Po suboti, u osvit prvoga dana u tjednu, dođe Marija Magdalena i druga Marija pogledati grob.
2Ghafla kutatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.
2I gle, nastade žestok potres jer anđeo Gospodnji siđe s neba, pristupi, otkotrlja kamen i sjede na nj.
3Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.
3Lice mu bijaše kao munja, a odjeća bijela kao snijeg.
4Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.
4Od straha pred njim zadrhtaše stražari i obamriješe.
5Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, "Ninyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.
5A anđeo progovori ženama: "Vi se ne bojte! Ta znam: Isusa Raspetoga tražite!
6Hayupo hapa maana amefufuka kama alivyosema. Njoni mkaone mahali alipokuwa amelala.
6Nije ovdje! Uskrsnu kako reče. Hajde, vidite mjesto gdje je ležao
7Basi, nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuka kutoka wafu, na sasa anawatangulieni kule Galilaya; huko mtamwona. Haya, mimi nimekwisha waambieni."
7pa pođite žurno i javite njegovim učenicima da uskrsnu od mrtvih. I evo, ide pred vama u Galileju. Ondje ćete ga vidjeti. Evo, rekoh vam."
8Wakiwa wenye hofu na furaha kubwa, hao wanawake walitoka upesi kaburini, wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi wake.
8One otiđoše žurno s groba te sa strahom i velikom radošću otrčaše javiti njegovim učenicima.
9Mara, Yesu akakutana nao, akawasalimu: "Salamu." Hao wanawake wakamwendea, wakapiga magoti mbele yake, wakashika miguu yake.
9Kad eto im Isusa u susret! Reče im: "Zdravo!" One polete k njemu, obujme mu noge i ničice mu se poklone.
10Kisha Yesu akawaambia, "Msiogope! Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, na huko wataniona."
10Tada im Isus reče: "Ne bojte se! Idite, javite mojoj braći da pođu u Galileju! Ondje će me vidjeti!"
11Wale wanawake walipokuwa wanakwenda zao, baadhi ya walinzi wa lile kaburi walikwenda mjini kutoa taarifa kwa makuhani wakuu juu ya mambo yote yaliyotukia.
11Dok su one odlazile, gle, neki od straže dođoše u grad i javiše glavarima svećeničkim sve što se dogodilo.
12Basi, wakakutana pamoja na wazee, na baada ya kushauriana, wakawapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha
12Oni se sabraše sa starješinama na vijećanje, uzeše mnogo novaca i dadoše vojnicima
13wakisema, "Ninyi mtasema hivi: Wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba sisi tukiwa tumelala.
13govoreći: "Recite: 'Noću dok smo mi spavali, dođoše njegovi učenici i ukradoše ga.'
14Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa ninyi hamtapata matatizo."
14Ako to dočuje upravitelj, mi ćemo ga uvjeriti i sve učiniti da vi budete bez brige."
15Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.
15Oni uzeše novac i učiniše kako bijahu poučeni. I razglasilo se to među Židovima - sve do danas.
16Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagiza Yesu.
16Jedanaestorica pođoše u Galileju na goru kamo im je naredio Isus.
17Walipomwona, wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.
17Kad ga ugledaše, padoše ničice preda nj. A neki posumnjaše.
18Yesu akaja karibu, akawaambia, "Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
18Isus im pristupi i prozbori: "Dana mi je sva vlast na nebu i na zemlji!
19Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu; mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
19Pođite dakle i učinite mojim učenicima sve narode krsteći ih u ime Oca i Sina i Duha Svetoga
20Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati."
20i učeći ih čuvati sve što sam vam zapovjedio!" "I evo, ja sam s vama u sve dane - do svršetka svijeta."