1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
1Ka mina, vennad, ei võinud rääkida teile kui vaimsetele, vaid pidin rääkima kui lihalikele, nagu väetitele lastele Kristuses.
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
2Ma jootsin teile piima ega andnud tahket rooga, sest seda te ei oleks veel talunud. Kuid ega te nüüdki veel talu,
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
3sest et olete ju alles lihalikud. Kui teie seas on kiivust ja riidu - eks te siis ole lihalikud ja eks te käitu inimlikult?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
4Sest kui üks ütleb: 'Mina olen Pauluse poolel!', teine aga: 'Mina Apollose!' - eks te siis ole nagu inimesed ikka?
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
5Mis on siis Apollos? Mis on Paulus? Teenrid, kelle kaudu te olete saanud usklikuks, nõnda nagu Issand igaühele on andnud.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
6Mina istutasin, Apollos kastis, kuid Jumal laskis kasvada.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
7Nõnda siis ei ole midagi see, kes istutab, ega see, kes kastab, vaid Jumal, kes kasvatab.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
8Istutaja ja kastja teevad sama tööd, aga kumbki saab oma palga vastavalt oma vaevanägemisele.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
9Sest Jumala kaastöölised oleme meie; Jumala põllumaa, Jumala hoone olete teie.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
10Mulle antud Jumala armu järgi olen ma kui tark hooneehitaja rajanud aluse, aga teine ehitab sellele. Igaüks vaadaku siis, kuidas ta ehitab!
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
11Jah, teist alust ei saa keegi rajada selle kõrvale, mis on juba olemas - see on Jeesus Kristus.
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
12Kas keegi ehitab sellele alusele hoone kullast, hõbedast, kalliskividest, puudest, heintest või õlgedest -
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
13kord saab igaühe töö avalikuks. Issanda päev teeb selle teatavaks, sest see ilmub tules, ja tuli katsub läbi igaühe töö, missugune see on.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
14Kui kellegi töö, mis ta on ehitanud, jääb püsima, siis ta saab palga.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
15Kui kellegi töö põleb ära, siis ta saab kahju, aga ta ise päästetakse otsekui läbi tule.
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
16Eks te tea, et te olete Jumala tempel ja teie sees elab Jumala Vaim?
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
17Kui keegi rikub Jumala templi, siis Jumal rikub ka tema, sest Jumala tempel on püha, ja see olete teie.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
18Ärgu ükski petku ennast! Kes teie seas tundub endale targana selles maailmas, see saagu narriks, et ta saaks targaks!
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
19Jumala juures on ju praeguse maailma tarkus narrus, sest on kirjutatud: 'Tema tabab targad nende riugastelt.'
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
20Ja taas: 'Issand tunneb ära tarkade arutlused, et need on tühised.'
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
21Nõnda ärgu siis ükski kiidelgu inimestest, sest teie päralt on kõik:
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
22olgu Paulus, olgu Apollos, olgu Keefas, olgu maailm, olgu elu, olgu surm, olgu käesolev, olgu tulev - kõik on teie päralt,
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.
23teie olete aga Kristuse päralt ja Kristus on Jumala päralt.