1Ndugu, mimi nilipokuja kwenu sikuwahubiria siri ya ujumbe wa Mungu kwa ufasaha wa lugha, au kwa hekima ya binadamu.
1Kui ma teie juurde tulin, vennad, ei tulnud ma eriti üleva kõne või tarkusega kuulutama teile Jumala saladust.
2Nilipokuwa kwenu niliamua kutojua chochote kile isipokuwa tu kumjua Yesu Kristo; naam, Kristo aliyesulubiwa.
2Sest ma otsustasin teada teie keskel ainuüksi Jeesusest Kristusest ja temast kui ristilöödust.
3Nilipokuwa kwenu nilikuwa dhaifu, natetemeka kwa hofu nyingi.
3Ja ma olin teie juures nõtruses ja kartuses ja suures värinas
4Hotuba zangu na mahubiri yangu sikuyatoa kwa maneno ya kuvutia na ya hekima, bali kwa uthibitisho mwingi na nguvu ya Roho.
4ning mu kõne ja mu kuulutus ei püüdnud veenda tarkusega, vaid Vaimu ja väe osutamisega,
5Nilifanya hivyo kusudi imani yenu ipate kutegemea nguvu ya Mungu, na si hekima ya binadamu.
5et teie usk ei oleks inimlikus tarkuses, vaid Jumala väes.
6Hata hivyo, sisi tunatumia lugha ya hekima kwa wale waliokomaa kiroho; lakini hekima hiyo si ya hapa duniani, wala si ya watawala wa dunia hii ambao wako katika mkumbo wa kupotea.
6Tarkusest me kõneleme täiuslike seas; ent mitte praeguse ajastu ega selle kaduvate valitsejate tarkusest,
7Hekima tunayotumia ni hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichika, ambayo Mungu aliiazimia tangu mwanzo kwa ajili ya utukufu wetu.
7vaid me kõneleme Jumala saladusse peidetud tarkusest, mille Jumal on ette määranud meie kirkuseks enne ajastuid.
8Ni hekima ambayo watawala wa dunia hii hawakuielewa; maana wangalielewa, hawangalimsulubisha Bwana wa utukufu.
8Ükski praeguse ajastu valitsejaist ei ole seda ära tundnud, sest kui nad seda oleksid tundnud, ei oleks nad kirkuse Issandat risti löönud.
9Lakini, ni kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mambo ambayo jicho halijapata kuyaona wala sikio kuyasikia, mambo ambayo binadamu hajapata kuyafikiria moyoni, hayo ndiyo Mungu aliyowatayarishia wale wampendao."
9Kuid nõnda nagu on kirjutatud: 'Mida silm ei ole näinud ega kõrv kuulnud ja mis inimsüdamesse ei ole tõusnud - selle on Jumal valmistanud neile, kes teda armastavad.'
10Hayo ndiyo mambo Mungu aliyotufunulia kwa njia ya Roho wake. Maana Roho huchunguza kila kitu hata mambo ya ndani kabisa ya Mungu.
10Aga meile on Jumal selle ilmutanud Vaimu kaudu, kuna Vaim uurib läbi kõik, ka Jumala sügavused.
11Nani awezaye kujua mambo ya ndani ya mtu isipokuwa roho yake mtu huyo? Hali kadhalika, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
11Sest kes inimestest teab inimese mõtteid peale inimese vaimu, kes temas on? Samuti ei tea ükski Jumala mõtteid peale Jumala Vaimu.
12Sasa sisi hatukuipokea roho ya ulimwengu, bali tumepokea Roho atokaye kwa Mungu ili atuwezeshe kujua yale tuliyojaliwa na Mungu.
12Aga meie ei ole saanud maailma vaimu, vaid Vaimu, kes on Jumalast, et me võiksime teada, mida Jumal meile armust kingib.
13Basi sisi twafundisha, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya binadamu, bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua mambo ya kiroho kwa walio na huyo Roho.
13Seda me siis ka räägime mitte inimtarkuse õpetatud sõnadega, vaid Vaimu õpetatud sõnadega, võrreldes vaimseid asju vaimsetega.
14Mtu wa kidunia hapokei mambo ya Roho wa Mungu. Kwake mtu huyo mambo hayo ni upumbavu mtupu; yanapita akili yake; maana yanaweza tu kutambuliwa kwa msaada wa Roho.
14Aga maine inimene ei võta vastu midagi, mis on Jumala Vaimust, sest see on temale narrus ja ta ei suuda seda tunnetada, sest seda tuleb mõista vaimselt.
15Lakini mtu aliye na huyo Roho anaweza kubainisha ubora wa kila kitu, naye mwenyewe hahukumiwi na mtu mwingine.
15Kuid vaimne inimene mõistab kõike, ent teda ennast ei suuda mõista keegi.
16Maandiko yasema: "Nani awezaye kuifahamu akili ya Bwana? Nani awezaye kumshauri?" Lakini sisi tunayo akili ya Kristo.
16Sest kes on tundnud Issanda meelt, kes võib teda juhatada? Aga meil on Kristuse meel.