1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
1Paulus, Kristuse Jeesuse apostliks kutsutud Jumala tahtmisel, ja vend Soostenes -
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
2Korintoses olevale Jumala kogudusele, Kristuses Jeesuses pühitsetuile, kutsutud pühadele ning kõigile neile, kes kõigis paigus appi hüüavad meie Issanda Jeesuse Kristuse nime, kes on nende ja meie Issand:
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
3Armu teile ja rahu Jumalalt, meie Isalt, ja Issandalt Jeesuselt Kristuselt!
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
4Ma tänan alati oma Jumalat teie pärast Jumala armu eest, mis teile on antud Kristuses Jeesuses!
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
5Te olete ju kõige poolest saanud rikkaks temas, igasuguses sõnas ja igasuguses mõistmises,
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
6kuna tunnistus Kristusest on teis kinnitatud,
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
7nii et teil ei ole puudu ühestki armuannist, oodates meie Issanda Jeesuse Kristuse ilmumist.
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
8Tema kinnitab teid ka lõpuni, et te oleksite laitmatult puhtad meie Issanda Jeesuse Kristuse päeval.
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
9Ustav on Jumal, kelle poolt te olete kutsutud osadusse tema Poja Jeesuse Kristuse, meie Issandaga.
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
10Ma kutsun teid üles, vennad, meie Issanda Jeesuse Kristuse nime pärast, et te kõik räägiksite ühtviisi ja et teie seas ei oleks lõhesid, vaid et te oleksite ühte liidetud samas meeles ja samas nõus.
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
11Kuid Kloe pere, mu vennad, on mulle teie kohta teatanud, et teie seas on riidu.
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
12Ma räägin sellest, et igaüks teist ütleb: 'Mina olen Pauluse poolel!' või: 'Mina olen Apollose poolel!' või: 'Mina olen Keefase poolel!' või: 'Mina olen Kristuse poolel!'
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
13Kas Kristus on mitmeks jagatud?! Kas Paulus löödi risti teie eest? Või ristiti teid Pauluse nimesse?
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
14Ma tänan Jumalat, et ma ei ole teie seast kedagi ristinud peale Krispuse ja Gaiuse,
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
15nii et keegi ei saa öelda teid olevat ristitud minu nimesse.
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
16Siiski ma ristisin ka Stefanase pere; kedagi muud ei tea ma olevat ristinud.
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
17Sest Kristus ei läkitanud mind ristima, vaid evangeeliumi kuulutama, mitte aga inimliku tarkuse sõnadega, et Kristuse rist ei muutuks tühiseks.
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
18Jah, sõna ristist on narrus neile, kes hukkuvad, aga meile, kes päästetakse, on see Jumala vägi,
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
19sest kirjutatud on: 'Ma hävitan tarkade tarkuse ja teen olematuks mõistlike mõistuse.'
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
20Kus on tark? Kus on õpetlane? Kus on selle ajastu arutleja? Kas mitte Jumal pole teinud maailma tarkuse narruseks?
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
21Kuna maailm Jumala tarkuses ei tundnud Jumalat ära tarkuse abil, siis oli Jumalale meelepärane päästa selle narri kuulutuse kaudu need, kes usuvad.
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
22Sest juudid nõuavad tunnustähti ja kreeklased otsivad tarkust,
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
23meie aga kuulutame ristilöödud Kristust, kes on juutidele ärrituseks ja paganaile narruseks,
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
24ent neile, kes on kutsutud, olgu juutidele või kreeklastele, on ta Kristus, Jumala vägi ja Jumala tarkus.
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
25Sest Jumala narrus on inimestest targem ja Jumala nõtrus inimestest tugevam.
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
26Vaadake, vennad, iseendid, millistena te olete kutsutud: mitte palju tarku inimeste meelest, mitte palju vägevaid, mitte palju kõrgest soost.
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
27Kuid Jumal on valinud maailma meelest narrid, et häbistada tarku, ja Jumal on valinud maailma meelest nõrgad, et häbistada tugevaid.
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
28Jumal on valinud need, kes maailma meelest on alamast soost ja halvakspandud, need, kes midagi ei ole, et teha tühiseks need, kes midagi on,
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
29et ükski inimene ei kiitleks Jumala ees.
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
30Aga teie olete tema tõttu Kristuses Jeesuses, kes on saanud meile tarkuseks Jumalalt ning õiguseks ja pühitsuseks ja lunastuseks,
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."
31et läheks täide, nagu on kirjutatud: 'Kes tahab kiidelda, kiidelgu Issanda üle!'