Swahili: New Testament

Estonian

1 Corinthians

5

1Ziko habari za kuaminika kwamba kuna uzinzi miongoni mwenu; tena ni uzinzi mbaya ambao haujapata kuwako hata kati ya watu wasiomjua Mungu. Nimeambiwa eti mmoja wenu anaishi na mke wa baba yake!
1Üldse kuuldub teie seas olevat kõlvatust, ja veel niisugust kõlvatust, mida ei ole paganategi hulgas, et keegi elavat oma võõrasemaga.
2Mnawezaje kujivuna? Ingekuwa afadhali kwenu kuomboleza, na huyo aliyefanya kitu hicho aondolewe miongoni mwenu.
2Ent teie hooplete ega olegi kurvad ja ei kõrvaldagi oma keskelt seda, kes niisugust asja on teinud.
3Nami, kwa upande wangu, ingawa kwa mwili niko mbali nanyi, hata hivyo kwa roho niko hapo pamoja nanyi: na hivyo, kama vile nipo hapo, nimekwisha mhukumu huyo aliyefanya jambo hilo la aibu.
3Sest mina, ehkki ihulikult eemal, ent vaimus kohal, olen otsekui teie juures viibides juba teinud otsuse selle kohta, kes nõnda on elanud:
4Wakati mnapokusanyika pamoja kwa jina la Bwana Yesu, nami nikiwa pamoja nanyi kwa roho, basi, kwa uwezo wa Bwana wetu Yesu,
4meie Issanda Jeesuse nimel, kui teie ja minu vaim on kokku juhitud meie Issanda Jeesuse väega,
5mkabidhini mtu huyo kwa Shetani ili mwili wake uharibiwe na roho yake iweze kuokolewa Siku ile ya Bwana.
5see mees tuleb loovutada saatanale ihu hävitamiseks, et vaim võiks pääseda Issanda päeval.
6Majivuno yenu hayafai! Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge lote la unga?
6Teie kiitlemine ei ole hea. Kas te ei tea, et pisut haputaignat teeb kogu taigna hapuks?
7Jitakaseni, mkatupe mbali chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu kama mnavyopaswa kuwa; maana, Kristo, Pasaka yetu, amekwisha tolewa tambiko.
7Puhastage end vanast haputaignast, et te oleksite uus taigen, nõnda nagu te oletegi hapnemata leivad; sest ka meie paasatall Jeesus Kristus on tapetud.
8Basi, tufanye karamu hiyo si kwa chachu ile ya kale, chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, mkate wa usafi na kweli.
8Pidagem siis pühi kasinuse ja tõe hapnemata leivaga, mitte vana haputaignaga, halbuse ja kurjuse haputaignaga.
9Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi.
9Ma kirjutasin teile ühes kirjas, et ärge suhelge kõlvatutega.
10Ukweli ni kwamba sikuwa na maana ya watu wote duniani walio wazinzi, wachoyo, walaghai na wenye kuabudu sanamu. Maana, ili kuwaepa hao wote ingewalazimu ninyi kuihama dunia hii kabisa!
10Seda ma ei ütle üldiselt selle maailma kõlvatute või ahnete ja riisujate või ebajumalateenijate kohta, sest muidu peaksite maailmast ära minema.
11Nilichoandika ni hiki: msishirikiane na ndugu Mkristo aliye mzinzi, mchoyo, mwenye kuabudu sanamu, mchongezi mlevi na mlaghai. Mtu wa namna hiyo, hata kula msile naye.
11Aga nüüd ma kirjutan teile, et ärge suhelge sellisega, keda nimetatakse vennaks ja kes on kõlvatu või ahne või ebajumalateenija või pilkaja või joodik või riisuja. Niisugusega ärge koos söögegi!
12Je, ni shauri langu kuwahukumu watu walio nje? Hao Mungu atawahukumu. Je, ninyi hampaswi kuwahukumu wale walio katika jamii yenu ninyi wenyewe?
12Sest kas on minu asi kohut mõista nende üle, kes on väljas? Eks te mõista kohut nende üle, kes on sees?
13Mfukuzeni mbali nanyi huyo mwovu!
13Nende üle, kes on väljas, mõistab kohut Jumal. Kõrvaldage siis kuri endi keskelt!