Swahili: New Testament

Estonian

1 Corinthians

6

1Anathubutuje mmoja wenu kumshtaki ndugu muumini mbele ya mahakama ya watu wasiomjua Mungu badala ya kumshtaki mbele ya watu wa Mungu?
1Kui kellelgi teie seast on teisega sekeldusi, kuidas ta julgeb lasta kohut mõista ülekohtustel ja mitte pühadel?
2Je, hamjui kwamba watu wa Mungu watauhukumu ulimwengu? Ikiwa basi, ulimwengu utahukumiwa nanyi, kwa nini hamstahili kuhukumu hata katika mambo madogo?
2Või ei tea teie, et ükskord mõistavad pühad kohut kogu maailma üle? Ja kui te maailma üle kohut mõistate, kas te siis ei ole pädevad otsustama pisiasjus?
3Je, hamjui kwamba, licha ya kuhukumu mambo ya kawaida ya kila siku, tutawahukumu hata malaika?
3Kas te ei tea, et ükskord me mõistame kohut inglitegi üle, miks siis mitte argielu asjus?
4Mnapokuwa na mizozo juu ya mambo ya kawaida, je, mnawaita wawe mahakimu watu ambao hata hawalijali kanisa?
4Kui teil nüüd on sekeldusi argielus, kuidas te siis võite panna kohtumõistjateks neid, kellest kogudus ei pea üldse lugu?
5Aibu kwenu! Ndiyo kusema hakuna hata mmoja miongoni mwenu mwenye hekima kiasi cha kuweza kutatua tatizo kati ya ndugu waumini?
5Seda ma ütlen teile häbistuseks. Kas siis teie seas ei ole ühtainsatki tarka, kes suudaks otsustada venna ja venna vahel?
6Badala yake, kweli imekuwa mtindo ndugu kumpeleka ndugu yake mahakamani, tena mbele ya mahakimu wasioamini.
6Vaid vend käib kohut vennaga, ja seda uskmatute ees!
7Kwa kweli huko kushtakiana tu wenyewe kwa wenyewe kwabainisha kwamba mmeshindwa kabisa! Je, haingekuwa jambo bora zaidi kwenu kudhulumiwa! Haingekuwa bora zaidi kwenu kunyang'anywa mali yenu?
7Juba see on halb, et te käite kohut üksteisega. Miks te pigem ei kannata ülekohut? Miks te pigem ei lase enesele kahju teha?
8Lakini, badala yake, ninyi ndio mnaodhulumu na kunyang'anya; tena, hayo mnawafanyia ndugu zenu!
8Vaid teie ise teete ülekohut ja teete kahju, ja seda vendadele!
9Au je, hamjui kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msijidanganye! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti,
9Või te ei tea, et ülekohtused ei päri Jumala riiki? Ärge eksige: ei kõlvatud ega ebajumalateenijad, ei abielurikkujad ega lõbupoisid ega meestepilastajad,
10wevi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang'anyi, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu.
10ei vargad ega ahned, ei joodikud ega pilkajad ega riisujad päri Jumala riiki!
11Baadhi yenu mlikuwa hivyo; lakini sasa mmeoshwa, mkafanywa watakatifu, na kupatanishwa na Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.
11Ja sellised olid mõned teiegi seast. Kuid teie olete puhtaks pestud, te olete pühitsetud, te olete õigeks tehtud Issanda Jeesuse Kristuse nimes ja meie Jumala Vaimus.
12Mtu anaweza kusema: "Kwangu mimi kila kitu ni halali." Sawa; lakini si kila kitu kinafaa. Nakubali kwamba kila kitu ni halali kwangu lakini sitaki kutawaliwa na kitu chochote.
12Öeldakse: 'Mulle on kõik lubatud!' - Siiski kõigest ei ole kasu. 'Mulle on kõik lubatud!' - Siiski miski ärgu saagu meelevalda minu üle!
13Unaweza kusema: "Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula." Sawa; lakini Mungu ataviharibu vyote viwili. Mwili wa mtu si kwa ajili ya uzinzi bali ni kwa ajili ya kumtumikia Bwana, naye Bwana ni kwa ajili ya mwili.
13'Toit on kõhu jaoks ja kõht toidu jaoks.' - Siiski Jumal teeb lõpu nii sellele kui tollele. Aga ihu ei ole hooruse jaoks, vaid Issanda jaoks ja Issand ihu jaoks.
14Basi, Mungu aliyemfufua Bwana kutoka wafu atatufufua nasi pia kwa nguvu yake.
14Ent Jumal on Issanda üles äratanud ja äratab meidki üles oma väe läbi.
15Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya mwili wa Kristo? Je, mnadhani naweza kuchukua sehemu ya mwili wa Kristo na kuifanya kuwa sehemu ya mwili wa kahaba? Hata kidogo!
15Kas te ei tea, et teie ihud on Kristuse ihu liikmed? Kas ma võiksin siis võtta Kristuse liikmed ning teha nad hoora liikmeteks? Ei mingil juhul!
16Maana, kama mjuavyo, anayeungana na kahaba huwa mwili mmoja naye--kama ilivyoandikwa: "Nao wawili watakuwa mwili mmoja."
16Või kas te ei tea, et see, kes hoiab hoora poole, on temaga üks ihu? Sest nagu Jumal ütleb: 'Need kaks saavad üheks.'
17Lakini aliyejiunga na Bwana huwa roho moja naye.
17Aga kes hoiab Issanda poole, see on temaga üks vaim.
18Jiepusheni kabisa na uzinzi. Dhambi nyingine zote hutendwa nje ya mwili lakini mzinzi hutenda dhambi dhidi ya mwili wake mwenyewe.
18Põgenege kõlvatuse eest! Mis tahes patt, mida inimene iganes teeks, on väljaspool tema ihu. Kuid kes hoorab, see patustab iseenese ihu vastu.
19Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, ambaye mlimpokea kutoka kwa Mungu? Ninyi basi, si mali yenu wenyewe.
19Või kas te ei tea, et teie ihu on teis oleva Püha Vaimu tempel, kelle te olete saanud Jumalalt, ning et teie ei ole iseenese päralt?
20Mlinunuliwa kwa bei kubwa. Kwa hiyo, itumieni miili yenu kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
20Sest te olete kallilt ostetud. Austage siis Jumalat oma ihus!