1Yahusu sasa vyakula vilivyotambikiwa sanamu: Tunajua kwamba sisi sote tuna ujuzi, lakini ujuzi huo huwafanya watu wawe na majivuno; lakini mapendo hujenga.
1Ebajumalatele ohverdatud liha kohta te ütlete: 'Me teame, et meil kõigil on tunnetus.' Tunnetus teeb suureliseks, aga armastus ehitab.
2Anayefikiri kwamba anajua kitu, kwa kweli hajui chochote kama inavyompasa.
2Kui kellelegi tundub, et ta on midagi tunnetanud, siis ta pole veel tunnetanud, kuidas peab tunnetama.
3Lakini anayempenda Mungu huyo anajulikana naye.
3Aga kui keegi armastab Jumalat, selle on Jumal ära tundnud.
4Kwa hiyo, kuhusu vyakula vilivyotambikiwa sanamu, twajua kwamba sanamu si kitu duniani; twajua kwamba Mungu ni mmoja tu.
4Ebajumalatele ohverdatud liha söömise kohta te ütlete: 'Me teame, et maailmas ei ole olemas ühtegi ebajumalat ning et ei ole muud Jumalat kui üks.'
5Hata kama viko vitu viitwavyo miungu duniani au mbinguni, na hata kama wako miungu na mabwana wengi,
5Jah, kui olekski nõndanimetatud jumalaid, olgu taevas või maa peal, nõnda nagu inimeste meelest on jumalaid palju ja isandaid palju,
6hata hivyo, kwetu sisi yuko Mungu mmoja tu: Baba, Muumba wa vyote, ambaye kwa ajili yake sisi tuko. Pia yuko Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, na sisi twaishi kwa njia yake.
6siis meie jaoks on ometi ainult üks Jumal, Isa, kellest on kõik asjad, ja meie tema juurde teel, ning üks Issand, Jeesus Kristus, kelle läbi on kõik, ja ka meie tema läbi.
7Lakini, si kila mtu anao ujuzi huu. Maana wako watu wengine waliokwisha zoea sanamu, watu ambao mpaka hivi sasa wanapokula vyakula huviona bado kama vyakula vilivyotambikiwa sanamu. Na kwa vile dhamiri zao ni dhaifu, hutiwa unajisi.
7Kuid kõikidel ei ole seda tunnetust. Mõned ju söövad harjumusest ebajumalatega tänini seda liha just nagu ebajumalale ohverdatut, ja nende sisetunne, nõrk nagu see on, saab määritud.
8Lakini chakula hakiwezi kutupeleka karibu zaidi na Mungu. Tukiacha kukila hatupungukiwi kitu, tukikila hatuongezewi kitu.
8Söök ei vii meid Jumalale lähemale. Kui me ei söö, ei jää me millestki ilma, ega saa me mingit kasu, kui sööme.
9Lakini, jihadharini: huu uhuru wenu usiwafanye walio na imani dhaifu waanguke katika dhambi.
9Vaadake aga, et see teie meelevald kuidagi ei saaks komistuseks nõrkadele!
10Maana, mtu ambaye dhamiri yake ni dhaifu, akikuona wewe mwenye ujuzi unakula vyakula hivyo ndani ya hekalu la sanamu, je, hatatiwa moyo wa kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu?
10Sest kui sind, kellel on tunnetus, näeb ebajumala kojas lauas istuvat keegi, eks siis tema sisetunnet, nõrka nagu see on, juhatata ebajumalate ohvriliha söömisele?
11Hivyo, huyo ndugu yako dhaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea kwa sababu ya ujuzi wako.
11Siis hukkub ju sinu tunnetuse tõttu nõrk vend, kelle pärast Kristus on surnud.
12Kama mkiwakosesha ndugu zenu jinsi hiyo na kuzijeruhi dhamiri zao dhaifu, mtakuwa mmemkosea Kristo.
12Aga kui te nõnda patustate vendade vastu ja haavate nende nõrka sisetunnet, siis te patustate Kristuse vastu.
13Kwa hiyo, ikiwa chakula husababisha kuanguka kwa ndugu yangu, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi.
13Seepärast, kui söök viib kiusatusse mu venna, siis ma enam kunagi ei söö liha, et ma oma venda ei viiks kiusatusse.