Swahili: New Testament

Estonian

1 John

3

1Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
1Vaadake, kui suure armastuse Isa on meile andnud: meid hüütakse Jumala lasteks ja need me olemegi. Maailm ei tunne meid, sest ta ei tunne teda.
2Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
2Armsad, me oleme nüüd Jumala lapsed, ja veel ei ole saanud avalikuks, kes me ükskord oleme. Me teame, et kui tema saab avalikuks, siis me oleme tema sarnased, sest siis me näeme teda, nii nagu ta on.
3Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
3Igaüks, kellel on selline lootus tema peale, puhastab ennast, just nagu tema on puhas.
4Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
4Igaüks, kes teeb pattu, rikub ka seadust, ning patt on seaduserikkumine.
5Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
5Te teate, et tema on ilmunud patte ära kandma ning temas endas ei ole pattu.
6Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
6Ükski, kes püsib temas, ei tee pattu; ükski, kes teeb pattu, ei ole näinud ega mõistnud teda.
7Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
7Lapsed, ärgu keegi eksitagu teid! Kes teeb õigust, on õige, nii nagu tema on õige.
8Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
8Kes teeb pattu, on kuradist, sest kurat teeb pattu algusest peale. Selleks ongi Jumala Poeg saanud avalikuks, et ta tühistaks kuradi teod.
9Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
9Ükski, kes on sündinud Jumalast, ei tee pattu, sest Jumala seeme püsib temas ja ta ei saa teha pattu, sest ta on sündinud Jumalast.
10Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
10Sellest on näha, kes on Jumala lapsed ja kes kuradi lapsed: ükski, kes ei tee õigust, ei ole Jumalast, nagu ka mitte see, kes ei armasta oma venda.
11Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
11Jah, see ongi sõnum, mida te olete kuulnud algusest peale, et me peame üksteist armastama.
12Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
12Mitte nii nagu Kain, kes oli kurjast ja lõi maha oma venna. Ja mispärast ta lõi tema maha? Sellepärast, et tema teod olid kurjad, aga ta venna omad õiged.
13Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
13Ärge imestage, vennad, kui maailm teid vihkab.
14Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
14Me teame, et oleme tulnud surmast ellu, sest me armastame vendi. Kes ei armasta, see jääb surma.
15Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake.
15Igaüks, kes vihkab oma venda, on mõrvar, ja te teate, et ühelgi mõrvaril ei ole igavest elu, mis temasse jääks.
16Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
16Armastuse me oleme ära tundnud sellest, et Kristus on jätnud oma elu meie eest; ning meie oleme kohustatud jätma oma elu vendade eest.
17Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
17Kui nüüd kellelgi on selle maailma vara ja ta näeb oma venna olevat puuduses, ent lukustab oma südame tema eest - kuidas saab Jumala armastus jääda temasse?
18Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
18Lapsed, ärgem armastagem sõnaga ja keelega, vaid teoga ja tõega!
19Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
19Sellest me tunneme, et oleme pärit tõest. Ja me võime kinnitada tema ees oma südant,
20Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
20et olgu mis tahes, milles meie süda meid süüdistab, Jumal on siiski meie südamest suurem ja tema teab kõik.
21Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
21Armsad, kui meie süda ei süüdista, siis on meil julgus Jumala ees
22na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
22ja mida me iganes palume, seda me saame temalt, sest me peame tema käske ja teeme, mis on tema silmis meelepärane.
23Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
23Ja see on tema käsk, et me usuksime tema Poja Jeesuse Kristuse nimesse ja armastaksime üksteist, nii nagu tema meile on käsu andnud.
24Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.
24Ja kes peab tema käske, püsib Jumalas ja Jumal temas. Ja sellest me tunneme ära, et tema püsib meis - Vaimust, kelle ta meile on andnud.