1Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena.
1Pange siis maha kogu kurjus ja kogu kavalus ja silmakirjatsemine, kadetsemine ja mis tahes keelepeks!
2Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.
2Nagu äsjasündinud lapsed igatsege vaimulikku selget piima, et te selle varal kasvaksite pääste poole,
3Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mmegundua kwamba Bwana ni mwema."
3kui te olete tunda saanud, et Issand on helde.
4Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule, na la thamani kubwa.
4Tulles tema, elava kivi juurde, kes küll inimeste poolt on tunnistatud kõlbmatuks, ent Jumala silmis on valitud ja hinnaline,
5Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho, ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea dhabihu za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
5laske ka endid ehitada elavate kividena vaimulikuks kojaks. Saage pühaks preesterkonnaks, kes toob vaimulikke ohvreid, mis on Jumalale meelepärased Jeesuse Kristuse kaudu.
6Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Tazama! Naweka huko sioni jiwe kuu la msingi, jiwe la thamani kubwa nililoliteua. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa."
6Seepärast seisabki Pühakirjas: 'Ennäe, ma panen Siionisse kivi, valitud, hinnalise nurgakivi, ja see, kes usub temasse, ei jää iial häbisse.'
7Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini, "Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi."
7Teile siis, kes te usute, on see au, uskmatuile aga 'kivi, mille ehitajad tunnistasid kõlbmatuks, ning just see on saanud nurgakiviks',
8Tena Maandiko yasema: "Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa, mwamba wa kuwaangusha watu." Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.
8ning 'komistuskiviks' ja 'pahanduskaljuks'. Uskmatud komistavad, sest nad on sõnale allumatud ja selleks nad ongi määratud.
9Lakini ninyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani akawaingizeni katika mwanga wake mkuu.
9Teie aga olete 'valitud sugu, kuninglik preesterkond, püha rahvas, omandrahvas, et te kuulutaksite tema kiidetavust', kes teid on kutsunud pimedusest oma imelisse valgusse -
10Wakati mmoja ninyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa ninyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmeipokea.
10teid, kes te muiste polnud rahvas, nüüd aga olete Jumala rahvas, teie, kelle peale polnud halastatud, nüüd aga on.
11Wapenzi wangu, nawasihi ninyi kama wageni na wakimbizi hapa duniani! Achaneni na tamaa za mwili ambazo hupingana na roho.
11Armsad, ma manitsen teid kui majalisi ja võõraid siin ilmas - hoiduge lihalikest himudest, mis sõdivad hinge vastu!
12Mwenendo wenu kati ya watu wasiomjua Mungu unapaswa kuwa mwema kabisa, ili hata watakapowasingizieni kwamba mnatenda mabaya, waweze kutambua matendo yenu mema na hivyo wamtukuze Mungu Siku ya kuja kwake.
12Käituge hästi paganate keskel, et kuigi nad teist räägivad paha kui kurjategijaist, siiski, pannes tähele teie häid tegusid, annaksid nad Jumalale au aruandmise päeval.
13Basi, jiwekeni chini ya mamlaka yote ya kibinadamu, kwa ajili ya Bwana: utii kwa mfalme aliye mtawala mkuu,
13Alistuge Issanda pärast kogu inimlikule korrale, olgu kuningale kui kõige ülemale,
14utii kwa wakuu wa mikoa ambao wameteuliwa naye kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema.
14olgu maavalitsejale kui tema poolt saadetule kurjategijaid karistama, aga heategijaid kiitma.
15Maana Mungu anataka mweze kuyakomesha maneno ya kijinga ya watu wasio na akili kwa matendo mema mnayofanya.
15Selline on ju Jumala tahtmine, et te head tehes paneksite vaikima rumalate inimeste arutuse.
16Ishini kama watu huru; lakini msiutumie uhuru wenu kuuficha ubaya, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
16Elage otsekui vabad, ent ärge kasutage oma vabadust kurjuse katteks, vaid olge nagu Jumala sulased!
17Waheshimuni watu wote, wapendeni ndugu zenu waumini, mcheni Mungu, mheshimuni mfalme.
17Austage kõiki, armastage vendi, kartke Jumalat ja austage kuningat!
18Enyi watumishi wa nyumbani, watiini wakuu wenu kwa heshima yote, wawe wema na wapole au wenye kuchukiza.
18Orjad, alistuge täie aukartusega peremeestele, mitte üksnes headele ja leebetele, vaid ka tujukatele.
19Maana kama mnavumilia maumivu ya mateso msiyostahili kwa sababu mwajua kwamba Mungu anataka hivyo, basi Mungu atawafadhili.
19Sest see on arm, kui keegi südametunnistuse pärast Jumala ees talub viletsust, kannatades süütult.
20Maana, mtapata tuzo gani mkivumilia mapigo mnayostahili kwa sababu ya makosa yenu? Lakini kama mnavumilia mateso hata ingawa mmetenda mema, Mungu atawapeni baraka kwa ajili hiyo.
20Sest mis kuulsus see on, kui teid süü pärast pekstakse ja teie seda peate taluma? Aga kui te head tehes ja kannatades talute peksu, siis on see arm Jumalalt.
21Hayo ndiyo mliyoitiwa; maana Kristo mwenyewe aliteseka kwa ajili yenu, akawaachieni mfano, ili muufuate mwenendo wake.
21Selleks te olete kutsutud, sest ka Kristus kannatas teie eest, jättes teile eeskuju, et te käiksite tema jälgedes.
22Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake.
22'Tema ei teinud pattu ega leitud pettust tema suust';
23Alipotukanwa yeye hakujibu kwa tukano; alipoteseka yeye hakutoa vitisho, bali aliyaweka matumaini yake kwa Mungu, hakimu mwenye haki.
23ta ei sõimanud vastu, kui teda sõimati; ta kannatas ega ähvardanud, vaid jättis kõik selle hoolde, kes mõistab kohut õiglaselt;
24Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake juu ya msalaba, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake, ninyi mmeponywa.
24ta kandis ise meie patud oma ihus üles ristipuule, et meie, olles surnud pattudele, elaksime õigusele; tema vermete varal te olete saanud terveks.
25Ninyi mlikuwa kama kondoo waliokuwa wamepotea; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.
25Teie olite ju 'nagu lambad ekslemas', kuid nüüd te olete pöördunud oma hingede Karjase ja Ülevaataja poole.