1Maadamu Kristo aliteseka kimwili, nanyi pia mnapaswa kujiimarisha kwa nia hiyo yake; maana mtu akisha teseka kimwili hahusiki tena na dhambi.
1Et nüüd Kristus on ihulikult kannatanud, relvastuge teiegi sellesama meelsusega, sest kes on kannatanud ihulikult, see on lakanud patustamast,
2Tangu sasa, basi, maisha yaliowabakia kuishi hapa duniani yanapaswa kuongozwa na matakwa ya Mungu, si na tamaa za kibinadamu.
2nii et ta maises elus allesjäänud aega ei ela enam inimlike himude, vaid Jumala tahtmise järgi.
3Wakati uliopita mlikuwa na muda mrefu wa kufanya mambo wanayofanya watu wasiomjua Mungu. Mliishi maisha ya anasa, ubinafsi, ulevi, ugomvi, kunywa mno na ya ibada haramu za sanamu.
3Sest te olete minevikus küllalt palju aega mööda saatnud paganate tahtmist täites, elades kõlvatuses, himudes, purjutamises, prassimistes, joomingutes ja sündsusetutes ebajumalateenistustes.
4Sasa, watu hao wasiomjua Mungu wanashangaa wanapoona kwamba hamwandamani nao tena katika hali ya kuishi vibaya, na hivyo wanawatukaneni.
4Just seepärast nad võõrastavad, et te nendega ei jookse kaasa sellesama ulaelu voolus ja teotavad teid,
5Lakini watapaswa kutoa hoja juu ya jambo hilo mbele yake Mungu aliye tayari kuwahukumu wazima na wafu!
5nemad, kes peavad aru andma sellele, kes on juba valmis tulema kohut mõistma elavate ja surnute üle.
6Kwa sababu hiyo, hao waliokufa ambao walikuwa wamehukumiwa katika maisha yao ya kimwili kama anavyohukumiwa kila mmoja, walihubiriwa Habari Njema kusudi katika maisha yao ya kiroho waishi kama aishivyo Mungu.
6Sest just selleks on ka surnutele kuulutatud evangeeliumi, et nende üle mõistetaks kohut küll nagu inimeste üle lihas, aga nad elaksid vaimus nagu Jumal.
7Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na nidhamu, ili mweze kusali.
7Aga kõigi asjade lõpp on lähedal. Olge siis arukad ja kained palveteks.
8Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi.
8Üle kõige olgu püsiv teie omavaheline armastus, sest 'armastus katab kinni pattude hulga'.
9Muwe na ukarimu ninyi kwa ninyi bila kunung'unika.
9Olge üksteise vastu külalislahked ilma nurisemata!
10Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile uwakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu.
10Teenigu igaüks teisi selle andega, mille ta on saanud, nagu Jumala mitmesuguse armu head majapidajad.
11Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumika anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina.
11Kui keegi räägib, siis ta rääkigu nagu Jumala sõnul, kui keegi teenib, siis teenigu nagu selle jõuga, mille Jumal annab, nõnda et Jumal saaks kõigiti austust Jeesuse Kristuse kaudu, kelle päralt on kirkus ja võimus igavesest ajast igavesti! Aamen.
12Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida.
12Armsad, ärge võõrastage enestes tulekuumust, millega teid pannakse proovile, nii nagu sünniks teile midagi võõrast,
13Ila furahini kwamba mnashiriki mateso ya Kristo ili mweze kuwa na furaha tele wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
13vaid rõõmustage, et nii nagu te olete Kristuse kannatuste osalised, võite rõõmuga hõisata ka tema kirkuse ilmumisel.
14Heri yenu ikiwa mnatukanwa kwa sababu ya jina la Kristo; jambo hilo lamaanisha kwamba Roho mtukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yetu.
14Õndsad olete teie, kui teid teotatakse Kristuse nime pärast, sest siis hingab teie peal kirkuse Vaim, Jumala Vaim.
15Asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu ambaye anapaswa kuteseka kwa sababu ni muuaji, mwizi, mhalifu au mwovu.
15Ärgu aga keegi teie seast kannatagu mõrtsukana või vargana või kurjategijana või teiste ellu sekkujana!
16Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo.
16Aga kes kannatab kristlasena, ärgu häbenegu, vaid andku Jumalale au selle nimega!
17Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu?
17Sest käes on aeg kohtumõistmisel alata Jumala kojast; aga kui esmalt meist, missugune lõpp ootab siis neid, kes ei võta kuulda Jumala evangeeliumi?
18Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa; itakuwaje basi kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?"
18Ja kui juba õige pääseb vaevu, kuhu siis satub jumalakartmatu ja patune?
19Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.
19Sellepärast ka need, kes kannatavad Jumala tahtmise järgi, usaldagu oma hinged head tehes tema, ustava Looja hoolde.