1Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
1Aga Vaim ütleb selge sõnaga, et tulevastel aegadel mõned taganevad usust ja hoiavad eksitajate vaimude ja kurjade vaimude õpetuste poole
2Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
2nende valerääkijate silmakirjalikkuse mõjul, kes on põletanud tulemärgi oma südametunnistusse.
3Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
3Nad keelavad abiellumast ja käsivad hoiduda roogadest, mis Jumal on loonud usklikele ja tõde juba mõistnutele tänuga vastuvõtmiseks.
4Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
4Sest kõik, mis Jumal on loonud, on hea ja miski pole taunitav, mida võetakse vastu tänuga,
5kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
5sest seda pühitsetakse Jumala sõna ja palve läbi.
6Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
6Kui sa seda vendadele õpetad, siis sa oled Kristuse Jeesuse tubli teenija, üles kasvanud usu ja hea õpetuse sõnades, mille järgi sa oled hakanud käima.
7Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
7Aga labased kõned ja vananaistejutud lükka tagasi, harjuta end jumalakartuses!
8Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
8Sest kehalisest harjutamisest on vähe kasu, aga jumalakartus on kasulik kõigeks ning sellel on praeguse ja tulevase elu tõotus.
9Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
9See sõna on ustav ja väärib igati vastuvõtmist:
10Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
10selleks me ju näeme vaeva ja võitleme, sest me oleme oma lootuse pannud elava Jumala peale, kes on kõigi inimeste, iseäranis usklike Päästja.
11Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
11Seda käsi ja õpeta!
12Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
12Ärgu keegi mõtelgu üleolevalt sinu noorusest, vaid saa usklikele eeskujuks kõnes, käitumises, armastuses, usus, puhtuses!
13Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
13Ole hoolas ette lugema, ergutama, õpetama, kuni ma tulen!
14Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
14Ära jäta hooletusse vaimuandi, mis sulle anti ennustuse läbi, kui vanemad panid oma käed sinu peale!
15Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
15Nende asjade peale mõtle, ela selles, et su edenemine oleks avalik kõigile!
16Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.
16Pane tähele iseennast ja õpetust, jää kõigesse sellesse püsima, kui sa seda teed, siis sa päästad enda ja need, kes sind kuulavad.