1Msemo huu ni wa kweli: mtu akitaka kuwa kiongozi katika kanisa, huyo anatamani kazi nzuri.
1See on ustav sõna. Kui keegi igatseb ülevaatajaametit, siis ta igatseb üllast tööd.
2Basi, kiongozi wa kanisa anapaswa awe mtu asiye na lawama; anapaswa awe na mke mmoja tu, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu; ni lazima awe mkarimu na anayeweza kufundisha;
2Ülevaataja peab siis olema laitmatu: ühenaisemees, kaine, mõõdukas, kombekas, külalislahke, osav õpetama,
3asiwe mlevi au mtu wa matata, bali awe mpole, apendaye amani; asiwe mtu wa kupenda fedha;
3kes ei ole joomar ega kakleja, vaid leebe, rahupüüdlik ja rahahimuta,
4anapaswa awe mtu awezaye kuongoza vema nyumba yake, na kuwafanya watoto wake wawe watii kwa heshima yote.
4kes oma peret hästi juhatab ja kelle lapsed elavad kuulekuses ja kõigiti väärikalt.
5Maana kama mtu hawezi kuongoza vema nyumba yake, atawezaje kulitunza kanisa la Mungu?
5Sest kui keegi ei oska juhatada oma peret, kuidas ta võib kanda hoolt Jumala koguduse eest?
6Mtu ambaye hajakomaa bado katika imani asifanywe kuwa kiongozi katika kanisa, asije akajaa majivuno na kuhukumiwa kama vile Ibilisi alivyohukumiwa.
6Ta ärgu olgu ka vastpöördunu, et ta ei läheks upsakaks ega langeks sama süü sisse kui kurat.
7Anapaswa awe mwenye sifa njema kati ya watu walio nje ya kanisa, ili asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa Ibilisi.
7Tal peab olema hea tunnistus ka neilt, kes on väljaspool kogudust, et ta ei langeks hurjutamise alla ega kuradi silmusesse.
8Wasaidizi katika kanisa wanapaswa pia kuwa watu wenye tabia njema na wanyofu; wasiwe wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha;
8Niisamuti peavad abilised olema väärikad, kes ei ole kahekeelsed, kes ei tarvita liialt veini, kes ei ole liigkasuvõtjad,
9wanapaswa kuzingatia kwa dhamiri njema ukweli wa ndani wa imani.
9vaid kellel usu saladus on puhtas südametunnistuses.
10Ni lazima kwanza wathibitishwe, na wakionekana kuwa wanafaa, basi, watoe huduma yao.
10Neidki aga katsutagu enne läbi ja seejärel nad asugu teenima, kui on laitmatud.
11Wake zao wanapaswa pia kuwa na tabia njema, wasiowasengenya watu, wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote.
11Niisamuti olgu naised väärikad, mitte keelepeksjad, vaid kained, ustavad kõigis asjus.
12Msaidizi katika kanisa lazima awe na mke moja tu, na awezaye kuongoza vema watoto wake na nyumba yake.
12Abilised olgu ühenaisemehed, kes lapsi ja oma peret hästi juhatavad.
13Maana wasaidizi wanaofanya kazi yao vizuri hujipatia msimamo mzuri, na wanaweza kusema bila hofu juu ya imani yao katika Kristo Yesu.
13Sest kes hästi peavad oma ametit, saavad tunnustuse ja rohkesti julgust usus Kristusesse Jeesusesse.
14Ninakuandikia barua hii nikiwa na matumaini ya kuja kwako hivi karibuni.
14Seda ma kirjutan sulle, lootes ise peatselt tulla sinu juurde.
15Lakini kama nikicheleweshwa, basi, barua hii itakufahamisha mwenendo tunaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, na ambalo ni nguzo na msingi wa ukweli.
15Kui mu tulek siiski viibib, sa teaksid, milline peab olema eluviis Jumala kojas, mis on elava Jumala kogudus, tõe sammas ja alustugi.
16Hakuna mashaka yoyote juu ya ukuu wa siri ya dini yetu: Alionekana katika umbo la kibinadamu alithibitishwa na Roho kuwa ni mwadilifu, akaonekana na malaika. Alihubiriwa kati ya mataifa, aliaminiwa popote ulimwenguni, akachukuliwa juu mbinguni katika utukufu.
16Tunnistatavalt suur on jumalakartuse saladus: Jumal on avalikuks saanud lihas, õigeks tunnistatud vaimus, nähtav olnud inglitele, kuulutatud paganatele, usutud maailmas, võetud üles kirkusesse.