Swahili: New Testament

Estonian

1 Timothy

2

1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
1Ma kutsun siis üles anuma, palvetama, tegema eestpalveid ja tänupalveid kõigi inimeste eest,
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
2kuningate ja kõigi ülemuste eest, et me võiksime elada vaikset ja rahulikku elu kõiges jumalakartuses ja väärikuses.
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
3See on hea ja meeldiv Jumala, meie Päästja silmis,
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
4kes tahab, et kõik inimesed pääseksid ja tuleksid tõe tundmisele.
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
5Sest üks on Jumal, üks on ka vahemees Jumala ja inimeste vahel: inimene Kristus Jeesus,
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
6kes on iseenese loovutanud lunastushinnaks kõikide eest, tunnistusena selleks määratud ajal.
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
7Selle sõnumi kuulutajaks ja apostliks olen ma pandud - ma räägin tõtt, ma ei valeta -, paganate õpetajaks usus ja tões.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
8Ma tahan siis, et mehed igal pool palvetaksid, tõstes üles pühad käed ilma viha ja kahtlemiseta.
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
9Niisamuti ka naised, kombekalt rõivastatuna, ehtigu end häbelikkuse ja mõõdukusega, mitte soengute ega kulla ega pärlite ega kallite riietega,
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
10vaid heade tegudega, nagu on kohane naistele, kes end tunnistavad jumalakartlikeks.
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
11Naine õppigu vaikselt täielikus alistumises;
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
12ma ei luba naisel õpetada ega mehe üle valitseda, vaid ta olgu vaikne.
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
13Sest Aadam loodi enne, seejärel Eeva,
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
14ka ei petetud Aadamat, vaid naine peteti ära ja ta sattus üleastumisse,
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.
15ent ta pääseb lastesünnitamise kaudu, kui ta mõõdukuses jääb usku ja armastusse ja pühitsusse.