Swahili: New Testament

Estonian

2 Corinthians

1

1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo, tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho, na watu wote wa Mungu kila mahali katika Akaya.
1Paulus, Kristuse Jeesuse apostel Jumala tahtmisel, ja vend Timoteos - Korintoses olevale Jumala kogudusele ning kõigile pühadele kogu Ahhaias:
2Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
2Armu teile ja rahu Jumalalt, meie Isalt, ja Issandalt Jeesuselt Kristuselt!
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote.
3Kiidetud olgu Jumal ja meie Issanda Jeesuse Kristuse Isa, halastuse Isa ja kõige julgustuse Jumal!
4Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu.
4Tema julgustab meid igas meie ahistuses, et me suudaksime julgustada neid, kes on mis tahes ahistuses, julgustusega, millega Jumal meid endid julgustab.
5Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye.
5Sest otsekui meil on küllaga Kristuse kannatusi, nõnda on meil küllaga ka julgustust Kristuse kaudu.
6Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji ninyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi.
6Kui meid nüüd ahistatakse, siis sünnib see teie julgustamiseks ja päästmiseks; kui meid julgustatakse, siis sünnib seegi teie julgustamiseks; see saab teoks, kui te vapralt talute neidsamu kannatusi, mida meiegi kannatame.
7Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.
7Ja meie lootus teie peale on kindel, kuna me teame, et nii nagu teil on osa meie kannatustest, nõnda ka meie julgustusest.
8Ndugu, tunataka kuwajulisheni taabu zilizotupata kule Asia; taabu hizo zilitulemea kupita kiasi, hata tukakata matumaini yote ya kuendelea kuishi.
8Me ei taha ju, vennad, et teile jääks teadmata, kuidas meid Aasias ahistati: meid koormati üliväga üle meie jõu, nii et me koguni kahtlesime oma ellujäämises.
9Naam, tulikuwa kama watu waliohukumiwa kuuawa, ili tufundishwe kumtegemea Mungu mwenye kuwafufua wafu, badala ya kutegemea nguvu zetu sisi wenyewe.
9Jah, meil oli meie endi arvates surmakäsk juba käes, et me ei loodaks endi, vaid Jumala peale, kes surnud üles äratab.
10Yeye alituokoa katika hatari kubwa ya kifo, na anaendelea kutuokoa; sisi tumemwekea tumaini letu kwamba atatuokoa tena,
10Tema päästis meid sellest määratu suurest surmast ja päästab veelgi - tema, kelle peale me loodame. Jah, ta päästab edaspidigi,
11ninyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.
11kui ka teie eestpalvetega meile appi tulete, nii et paljud tänaksid meile paljude inimeste eestpalvete tõttu Jumalalt osaks saanud armuanni eest.
12Sisi tunajivunia kitu kimoja: dhamiri yetu inatuhakikishia kwamba tumeishi ulimwenguni hapa, na hasa kati yenu, kwa unyenyekevu na unyofu tuliojaliwa na Mungu; hatukuongozwa na hekima ya kibinadamu bali neema ya Mungu.
12Meie kiitlemine on just see: meie südametunnistus võib tõendada, et oleme käitunud siin maailmas, eriti aga teiega suheldes, Jumalalt saadud siiras ja selges meeles, mitte lihalikus tarkuses, vaid Jumala armus.
13Tunawaandikia ninyi mambo mnayoweza kuyasoma na kuyaelewa. Ninatumaini kwamba mtaelewa vizuri kabisa,
13Me ei kirjuta teile ju midagi muud peale selle, mida te siit loete ja ehk ka mõistate. Ent ma loodan, et te kunagi täielikult mõistate seda,
14maana mpaka sasa mmenielewa kiasi fulani tu. Tunajua kwamba katika ile Siku ya Bwana Yesu mtaweza kutuonea sisi fahari kama nasi tunavyowaonea ninyi fahari.
14mida te praegu vaid osaliselt olete mõistnud, nii et te võite meie Issanda Jeesuse päeval kiidelda meist, nagu meie kiitleme teist.
15Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu.
15Ja selle meelekindlusega ma tahtsingi esmalt tulla teie juurde, et te saaksite teistkordselt armu,
16Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia, na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea.
16ja teie kaudu matkata Makedooniasse ja Makedooniast tulla tagasi teie juurde ning lasta teil mind saata teele Juudamaale.
17Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema "Ndiyo" na "Siyo" papo hapo?
17Tahtes nüüd seda, kas ma ei toiminud ehk kergemeelselt? Ehk ma kavatsen loomu järgi seda, mida kavatsen, et minu juures oleks 'jah, jah' ja 'ei, ei' ühtaegu?
18Mungu ni ukweli mtupu; basi, kile tulichowaambia ninyi si jambo la "Ndiyo" na "Siyo".
18Kui aga Jumal on ustav, siis meie sõna teie vastu ei ole ühtaegu 'jah' ja 'ei'.
19Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa "Ndiyo" na "Siyo"; bali yeye daima ni "Ndiyo" ya Mungu.
19Sest Jumala Poeg Jeesus Kristus, keda meie, mina, Silvanus ja Timoteos, oleme teie seas kuulutanud, ei olnud 'jah' ja 'ei', vaid temas oli 'jah'.
20Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa "Ndiyo". Kwa sababu hiyo, "Amina" yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
20Sest Jumala tõotused, millised iganes need olid, on Kristuses 'jah'. Seepärast tulgu ka meie suust tema läbi 'aamen' Jumalale kiituseks.
21Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na ninyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu;
21Aga see, kes meid koos teiega on kinnitanud Kristusesse ja kes meid on võidnud, on Jumal,
22ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
22kes on meid ka pitseriga kinnitanud ning meile andnud käsirahaks Vaimu südamesse.
23Mungu ndiye shahidi wangu--yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho, kwa sababu tu ya kuwahurumieni.
23Mina aga kutsun Jumala tunnistajaks oma hinge vastu, et ainult teie säästmise pärast ei ole ma enam Korintosesse tulnud.
24Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; ninyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.
24See pole nii. Meie ei taha ju olla isandad teie usu üle - usus te püsite niigi -, vaid me tahame olla kaasosalised teie rõõmus.