Swahili: New Testament

Estonian

1 Corinthians

16

1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
1Korjandusest pühade jaoks: nii nagu ma olen korraldanud selle Galaatia kogudustes, nõnda tehke ka teie.
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
2Iga nädala esimesel päeval pangu igaüks teist midagi tallele oma jõudu mööda, kuidas ta käsi lubab, et raha ei korjataks alles siis, kui ma tulen.
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
3Aga kui ma olen pärale jõudnud, siis ma saadan kirjadega need, keda te iganes arvate kõlbavat, viima teie anni Jeruusalemma,
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
4aga kui on sünnis, et minagi sinna lähen, tulgu nad minuga kaasa.
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
5Aga ma tulen teie juurde, kui ma lähen läbi Makedoonia, sest mu tee läheb Makedoonia kaudu.
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
6Teie juurde jään ma vahest kauemakski, ehk veedan ka talve, et te siis mind teele saadaksite, kuhu ma iganes lähen.
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
7Sest praegu ma ei taha teid ainult möödumisi näha, vaid loodan mõneks ajaks jääda teie juurde, kui Issand lubab.
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
8Efesosse jään ma aga nelipühani,
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
9sest mulle on siin avanenud uks suureks ja tõhusaks tööks, ent vastaseid on palju.
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
10Aga kui Timoteos tuleb, siis vaadake, et ta võiks teie juures olla kartmata, ta ju teeb Issanda tööd nagu minagi.
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
11Ärgu siis keegi pidagu teda halvaks, vaid saatke ta rahus teele, et ta tuleks minu juurde, sest mina koos vendadega ootan teda.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
12Vend Apollose kohta: olen teda tihti õhutanud, et ta koos vendadega tuleks teie juurde, aga tal polnud põrmugi tahtmist nüüd tulla; ent ta tuleb, kui ta leiab mahti.
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
13Valvake, seiske usus, olge mehised, saage tugevaks!
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
14Kõik teie teod sündigu armastuses!
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
15Aga ma palun teid, vennad: te teate Stefanase peret, et see pere oli Ahhaias esimene pöörduma Kristuse poole. Nemad on pühendunud pühade abistamisele.
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
16Alistuge teiegi niisugustele ja kõigile, kes aitavad kaasa ja näevad vaeva.
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
17Ent ma rõõmustan Stefanase ja Fortunatuse ja Ahhaikose tulekust, sest nemad on täitnud teie aset,
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
18nad on ju andnud hingamist minu ja teie vaimule. Tunnustage siis niisuguseid!
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
19Aasia kogudused tervitavad teid! Palju tervitusi teile Issandas Akvilalt ja Priskalt koos kogudusega nende kojas.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
20Kõik vennad tervitavad teid! Tervitage üksteist püha suudlusega!
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
21Tervitus on minu, Pauluse oma käega!
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
22Kui keegi ei armasta Issandat, olgu ta ära neetud! Maaranata!
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
23Issanda Jeesuse arm olgu teiega!
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.
24Minu armastus on teie kõikidega Kristuses Jeesuses!