Swahili: New Testament

Estonian

1 Corinthians

15

1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
1Aga nüüd ma teen teile, vennad, teatavaks evangeeliumi, mida ma teile olen kuulutanud, mille te ka olete vastu võtnud, milles te ka seisate
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
2ja mille läbi te ka pääsete. Kas te peate kinni sõnadest, millega ma teile evangeeliumi kuulutasin? Muidu olete küll ilmaaegu saanud usklikuks.
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
3Ma olen teile ju kõigepealt edasi andnud seda, mida ma ka ise olen vastu võtnud: et Kristus suri meie pattude eest, nagu on kirjutatud pühades kirjades,
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
4ja et ta maeti maha ja äratati kolmandal päeval üles pühade kirjade järgi
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
5ja et ta näitas ennast Keefasele, seejärel neile kaheteistkümnele,
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
6seejärel näitas ta ennast ühtaegu enam kui viiesajale vennale, kellest enamik on veel praegugi elus, mõned aga on läinud magama;
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
7siis näitas ta ennast Jaakobusele, seejärel kõigile apostlitele.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
8Aga kõige viimaks näitas ta ennast ka minule kui äbarikule.
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
9Mina ju olen apostlite seast kõige väiksem, see, keda ei kõlba hüüdagi apostliks, sest ma olen taga kiusanud Jumala kogudust.
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
10Aga Jumala armust olen ma see, kes olen, ja tema arm minu vastu ei ole läinud tühja, vaid ma olen neist kõigist palju rohkem vaeva näinud. Aga seda ei ole teinud mina, vaid Jumala arm, mis on minuga.
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
11Olgu nüüd mina või nemad - nõnda me kuulutame ja nõnda olete teie saanud usklikuks.
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
12Kui aga Kristusest kuulutatakse, et ta on üles äratatud surnuist, kuidas siis mõned teie seast ütlevad, et surnute ülestõusmist ei ole?
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
13Aga kui surnute ülestõusmist ei ole, siis ei ole ka Kristust üles äratatud.
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
14Aga kui Kristust ei ole üles äratatud, siis tähendab see, et ka meie jutlus on tühine ja tühine on ka teie usk.
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
15Ja meid leitakse siis olevat Jumala valetunnistajad, sest me oleme tunnistanud Jumalale vastu, et ta on üles äratanud Kristuse, keda tema ei ole üles äratanud, - sel juhul, kui surnuid üles ei äratata.
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
16Sest kui surnuid üles ei äratata, siis ei ole ka Kristust üles äratatud;
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
17kui aga Kristust ei ole üles äratatud, siis on teie usk tühine, siis te olete alles oma pattudes.
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
18Nii on siis ka hukkunud need, kes on Kristuses magama läinud.
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
19Kui me loodame Kristuse peale üksnes selles elus, siis me oleme kõigist inimestest armetumad.
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
20Nüüd aga on Kristus üles äratatud surnuist, uudseviljana magamaläinutest.
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
21Et surm on tulnud inimese kaudu, siis tuleb ka surnute ülestõusmine inimese kaudu;
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
22sest nõnda nagu kõik inimesed surevad Aadamas, nõnda tehakse ka kõik elavaks Kristuses.
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
23Aga igaüks oma järjekorras: uudseviljana Kristus, pärast seda Kristuse omad tema taastulekul;
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
24ja siis tuleb lõpp, kui ta loovutab kuningriigi Jumalale ja Isale, olles kõrvaldanud iga valitsuse ja iga meelevalla ja väe.
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
25Sest tema peab valitsema kuningana, kuni Jumal paneb kõik vaenlased tema jalge alla.
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
26Viimse vaenlasena kõrvaldatakse surm.
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
27Sest 'Jumal on kõik alistanud tema jalge alla'. Aga kui ta ütleb, et kõik on alistatud, siis on ilmne, et kõik peale selle, kes temale kõik alistas.
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
28Kui aga kõik on alistatud, siis alistub ka Poeg ise sellele, kes temale on kõik alistanud, et Jumal oleks kõik kõiges.
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
29Mida teeksid muidu need, keda surnute eest ristitakse? Kui surnuid üldse üles ei äratata, milleks nad lasevad end ristida surnute eest?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
30Ja milleks ma siis olen iga päev surmasuus?
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
31Ma suren iga päev, nii tõesti kui teie, vennad, olete mu kiitlemine, mis mul on Kristuses Jeesuses, meie Issandas.
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
32Kui ma võitlesin metsalistega Efesoses inimese kombel - mis kasu ma sellest sain? Kui surnuid üles ei äratata, siis 'söögem ja joogem, sest homme sureme nagunii'!
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
33Ärge eksige!'Halb seltskond rikub head kombed.'
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
34Saage täiesti kaineks ja ärge tehke pattu! Jah, mõnel ei ole üldse jumalatunnetust. Seda ma ütlen teile häbiks.
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
35Nüüd aga küsib mõni: 'Kuidas siis surnud üles äratatakse? Millise ihuga nad tulevad?'
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
36Rumal! See, mida sa külvad, ei saa elavaks, kui ta ei sure.
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
37Ja see, mida sa külvad - sa ei külva seda ihu, mis peab tõusma, vaid palja iva, olgu see siis nisu või mingi muu vili.
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
38Aga Jumal annab talle ihu, nõnda nagu ta on tahtnud, ning igale seemnele tema eriomase ihu.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
39Kõik liha ei ole sama liha, vaid isesugune on inimese liha ja isesugune veiste liha, isesugune lindude ja isesugune kalade liha.
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
40On taevalikke ihusid ja maapealseid ihusid, kuid taevalike hiilgus on teistsugune kui maapealsete oma,
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
41isesugune on päikese kirkus ja isesugune kuu kirkus ja isesugune tähtede kirkus, sest ka täht erineb tähest kirkuse poolest.
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
42Nõnda on ka surnute ülestõusmine: kaduvuses külvatakse, kadumatuses äratatakse üles,
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
43autuses külvatakse, kirkuses äratatakse üles, nõtruses külvatakse, väes äratatakse üles,
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
44maine ihu külvatakse, vaimne ihu äratatakse üles. Kui juba on olemas maine ihu, siis on olemas ka vaimne ihu.
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
45Nõnda on ka kirjutatud: 'Esimene inimene Aadam sai elavaks hingeks.' Viimne Aadam sai vaimuks, kes elustab.
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
46Kuid esmalt ei ole vaimne, vaid maine, siis alles tuleb vaimne.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
47Esimene inimene oli maast muldne, teine inimene oli taevast.
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
48Milline oli muldne, sellised on ka muldsed, ja milline oli taevane, sellised on ka taevased.
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
49Ja nii nagu me kandsime muldset kuju, nii kanname kord ka taevast kuju.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
50Aga seda ma ütlen, vennad: liha ja veri ei või pärida Jumala riiki ega kaduvus pärida kadumatust.
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
51Vaadake, ma ütlen teile saladuse: meie kõik ei lähegi magama, aga meid kõiki muudetakse,
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
52äkitselt, ühe silmapilguga, viimse pasuna hüüdes, sest pasun hüüab ja surnud äratatakse üles kadumatutena, ning meid muudetakse.
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
53Sest see kaduv peab riietuma kadumatusega ja see surelik riietuma surematusega.
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
54Aga kui see kaduv riietub kadumatusega ja see surelik riietub surematusega, siis läheb täide sõna, mis on kirjutatud: 'Surm on neelatud võidusse!
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
55Surm, kus on sinu võit? Surm, kus on sinu astel?'
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
56Aga surma astel on patt, ent patu vägi on Seadus.
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
57Aga tänu olgu Jumalale, kes meile võidu annab meie Issanda Jeesuse Kristuse läbi!
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.
58Niisiis, mu armsad vennad, olge kindlad, kõigutamatud ning ikka innukad Issanda töös, teades, et teie vaevanägemine Issandas ei ole tühine.