Swahili: New Testament

Estonian

2 Corinthians

11

1Laiti mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni kidogo.
1Oh et te salliksite ometi pisut minu rumalust! Te ju sallite mind!
2Ninawaoneeni wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
2Sest ma olen kiivas teie pärast jumaliku kiivusega, kuna ma olen teid kihlanud üheleainsale mehele, et teid puhta neitsina esitada Kristusele.
3Lakini naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa, fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
3Ma kardan aga, et nõnda nagu madu pettis Eevat oma kurikavaluses, nii rikutakse ka teie lihtne ja puhas Kristusest arusaamise võime.
4Maana mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa na ile mliyopokea kutoka kwetu!
4Sest kui keegi tuleb ja kuulutab mingit teist Jeesust, keda meie ei ole kuulutanud, või kui te saate teise vaimu, keda te ei ole saanud, või teise evangeeliumi, mida te ei ole vastu võtnud, siis te sallite seda küll.
5Sidhani kwamba mimi ni mdogo kuliko hao "mitume wakuu."
5Ma arvan ometi, et mina ei ole milleski kehvem neist 'ülivõrratuist apostleist'.
6Labda sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi kwenu, kila mahali na kila wakati.
6Kui ma olengi koolitamata kõnekunstis, ei ole ma seda tunnetuses, mille me oleme teile alati kõiges teatavaks teinud.
7Mimi niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
7Kas ma olen teinud pattu, kui ma ennast alandasin, et teid ülendataks, ja kuulutasin teile Jumala evangeeliumi päris muidu?
8Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine. Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
8Teisi kogudusi ma riisusin neilt palka võttes, et teenida teid,
9Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
9ja kui ma tundsingi teie juures olles puudust, ei olnud ma kellelegi vaevaks, sest mis mul puudu jäi, seda leevendasid vennad, kes tulid Makedooniast. Ja ma olen kõigiti püüdnud mitte olla teile koormaks ning püüan edaspidigi.
10Naahidi kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
10Nii tõesti kui Kristuse tõde on minus, ei vaigistata seda mu kiitlemist Ahhaia maakohtades.
11Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba nawapenda!
11Miks? Kas ma siis teid ei armasta? Küll Jumal teab!
12Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
12Aga nagu ma praegu ei võta midagi teie käest, nii ma teen ka edaspidi, et kõrvaldada neil valevendadel mis tahes võimalus kiidelda ja väita endid olevat niisugused nagu meie.
13Maana, hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa Kristo.
13Sest niisugused inimesed on valeapostlid, petised töötegijad, kes on moondanud ennast Kristuse apostleiks.
14Wala si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
14Ja see ei ole ime, sest saatan ise moondab ennast valguse ingliks.
15Kwa hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo yao.
15Seepärast ei ole midagi erilist, kui ka tema teenrid endid moondavad õiguse teenriteks. Nende eluots tuleb nende tegude järgi!
16Tena nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi, nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
16Taas ma ütlen: Ärgu keegi arvaku mind rumala olevat! Ja kui ometi, siis võtke mind vastu kui rumalat, et ka mina võiksin pisut kiidelda.
17Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna, nasema tu kama mtu mpumbavu.
17Mida ma nüüd räägin, seda ma ei räägi kui Issandalt saadut, vaid otsekui rumaluses, olles kindel, et mul on õigus kiitlemiseks.
18Maadam wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
18Aga et paljud kiitlevad lihaliku loomuse poolest, siis kiitlen minagi.
19Ninyi ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
19Te sallite meeleldi rumalust, olles ise arukad.
20Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
20Te ju sallite, kui keegi teid orjastab, kui keegi teid paljaks sööb, kui keegi teid koorib, kui keegi ülbitseb, kui keegi lööb teid näkku.
21Kwa aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu yeyote anayethubutu kujivunia kitu--nasema kama mtu mpumbavu--mimi nathubutu pia.
21Häbi pärast tunnistan, et meie oleme olnud liiga nõdrad.Mida aga keegi söandab - ma räägin rumaluses -, seda söandan minagi.
22Je, wao ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa Abrahamu? Hata mimi.
22Nemad on heebrea mehed. Mina ka. Nemad on Iisraeli lapsed. Mina ka. Nemad on Aabrahami sugu. Mina ka.
23Wao ni watumishi wa Kristo? Hata mimi--nanena hayo kiwazimu--ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
23Nemad on Kristuse teenrid. Ma räägin pööraselt - mina olen rohkem. Ma olen palju rohkem vaeva näinud, palju rohkem vangis olnud, saanud palju enam hoope, tihti olnud surmasuus.
24Mara tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
24Ma olen juutide käest viis korda saanud ühe hoobi vähem kui nelikümmend,
25Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
25mind on kolm korda keppidega pekstud, üks kord püütud kividega surnuks visata, kolm korda olen üle elanud laevahuku, terve öö ja päeva olen olnud veevoogudes;
26Kila mara safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama; hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine; hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu wa uongo
26tihti olen olnud teekondadel, ohus jõgedel, ohus teeröövlite käes, ohus oma rahva seas, ohus paganate seas, ohus linnades, ohus kõrbes, ohus merel, ohus valevendade käes,
27Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
27töös ja vaevas, tihti valvamises, näljas ja janus, tihti paastumises, külmas ja alasti;
28Na, licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
28peale kõige muu päevast päeva rahva kokkuvool minu juurde, mure kõigi koguduste pärast.
29Kama mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa na wasiwasi.
29Kes on nõder, ja mina ei oleks nõder? Keda kiusatakse, ja mina ei süttiks?
30Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
30Kui tuleb kiidelda, siis ma kiitlen oma nõtruse üle.
31Mungu na Baba wa Bwana Yesu--jina lake litukuzwe milele--yeye anajua kwamba sisemi uongo.
31Jumal ja meie Issanda Jeesuse Kristuse Isa, kes olgu kiidetud igavesti, teab, et ma ei valeta.
32Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
32Damaskuses valvas kuningas Aretase ametimees damasklaste linna, et mind kinni võtta,
33Lakini, ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani, nikachopoka mikononi mwake.
33ja mind lasti korviga läbi müüriakna alla ning ma pääsesin tema käest.