1Wapenzi wangu, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua hizo mbili nimejaribu kufufua fikira safi akilini mwenu kwa kuwakumbusheni mambo haya.
1Mu armsad, see on nüüd juba teine kiri, mille ma teile kirjutan. Mõlemas ma virgutan meenutamise kaudu teie selget mõistust,
2Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa na mitume wenu.
2et te mäletaksite sõnu, mida pühad prohvetid enne on rääkinud, ning Issanda ja Päästja käsku teie apostlitelt.
3Awali ya yote jueni kwamba siku za mwisho watakuja watu ambao mienendo yao inatawaliwa na tamaa zao mbaya. Watawadhihaki ninyi
3Seda teadke esmalt, et viimseil päevil tuleb pilkesõnadega pilkajaid, kes käivad iseenese himude järgi
4na kusema: "Aliahidi kwamba atakuja! Je, sasa yuko wapi? Mambo ni yaleyale tangu babu zetu walipokufa; hali ya vitu ni ileile kama ilivyokuwa mwanzo wa ulimwengu!"
4ja ütlevad: 'Kus on tema tulemise tõotus? Sest pärast seda, kui isad on läinud magama, on jäänud kõik nõnda nagu loomise algusest peale.'
5Watu hao, kwa makusudi, husahau kwamba zamani Mungu alinena, nazo mbingu na nchi zikaumbwa. Dunia iliumbwa kutoka katika maji na kwa maji;
5Aga seda väites jääb neil kahe silma vahele, et muiste olid olemas taevad ja veest tuli maa, mis püsis koos vee läbi Jumala sõna jõul,
6na kwa maji hayo, yaani yale maji ya gharika kuu, dunia ya wakati ule iliangamizwa.
6mille läbi tookordne maailm hukkus veeuputuses.
7Lakini mbingu na nchi za sasa zahifadhiwa kwa neno la Mungu kwa ajili ya kuharibiwa kwa moto. Zimewekwa kwa ajili ya Siku ile ambapo watu wasiomcha Mungu watahukumiwa na kuangamizwa.
7Aga praegusi taevaid ja maad, mis on säilitatud sellesama sõna jõul, hoitakse tule jaoks jumalakartmatute inimeste kohtu ja hukatuse päevaks.
8Lakini, wapenzi wangu, msisahau kitu kimoja! Mbele ya Bwana, hakuna tofauti kati ya siku moja na miaka elfu; kwake yote ni mamoja.
8Aga selle juures, mu armsad, ärgu jäägu teie eest varjule, et Issanda juures on üks päev nagu tuhat aastat ja tuhat aastat nagu üks päev.
9Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.
9Issand ei viivita tõotust täitmast, nii nagu mõned peavad seda viivitamiseks, vaid tema on teie vastu pikameelne, sest ta ei taha, et keegi hukkuks, vaid et kõik jõuaksid meeleparandusele.
10Siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; vitu vyake vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia itatoweka pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake.
10Aga Issanda päev tuleb nagu varas. Siis hukkuvad taevad raginal, algained lagunevad lõõmates ning maad ja tema tegusid ei leita enam.
11Maadamu kila kitu kitaharibiwa namna hiyo, je, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi kitakatifu na kumcha Mungu,
11Kui see kõik nõnda laguneb - missugused siis peate olema teie pühas eluviisis ja jumalakartuses,
12mkiingojea Siku ile ya Mungu na kuifanya ije upesi--Siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kuharibiwa, na vitu vyake vya asili vitayeyushwa kwa joto.
12oodates ja kiirendades Jumala päeva tulemist, mil taevad põledes lagunevad ja algained lõõmates ära sulavad.
13Lakini sisi, kufuatana na ahadi yake, twangojea mbingu mpya na dunia mpya ambayo imejaa uadilifu.
13Meie ootame aga tema tõotuse järgi uusi taevaid ja uut maad, kus elab õigus.
14Kwa hiyo wapenzi wangu, mkiwa mnangojea Siku ile, fanyeni bidii kuwa safi kabisa bila hatia mbele ya Mungu, na kuwa na amani naye.
14Seepärast, mu armsad, olge seda oodates toimekad, et teid leitaks tema ees veatuina ja laitmatuina rahus.
15Mnapaswa kuuona uvumilivu wa Bwana kuwa ni nafasi anayowapeni mpate kuokolewa, kama Paulo ndugu yetu mpenzi alivyowaandikia akitumia hekima aliyopewa na Mungu.
15Ja meie Issanda pikka meelt pidage päästeks, nõnda kui ka meie armas vend Paulus teile on kirjutanud temale antud tarkust mööda.
16Hayo ndiyo asemayo katika barua zake zote anapozungumzia suala hilo. Yapo mambo kadhaa katika barua zake yaliyo magumu kuyaelewa, mambo ambayo watu wajinga, wasio na msimamo, huyapotosha kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko Matakatifu. Hivyo wanasababisha maangamizi yao wenyewe.
16Sama ütleb ta kõikides kirjades, kus ta räägib neist asjust. Nendes on küll mõndagi raskesti mõistetavat, mida õppimata ja kõikuvad inimesed väänavad nagu muidki raamatuid iseendale hukatuseks.
17Lakini ninyi, wapenzi wangu, mmekwisha jua jambo hili. Basi, muwe na tahadhari msije mkapotoshwa na makosa ya waasi, mkaanguka kutoka katika msimamo wenu imara.
17Mu armsad, et te nüüd seda ette teate, siis olge valvsad, et teid ei kistaks kaasa kõlbluseta inimeste eksitustega ja te ei langeks ära oma kindlalt aluselt.
18Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina.
18Kasvage meie Issanda ja Päästja Jeesuse Kristuse armus ja tundmises! Tema päralt olgu kirkus nüüd ja igaviku päevil! Aamen.