1Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
1Aga rahva seas oli ka valeprohveteid, nõnda nagu teiegi sekka tuleb valeõpetajaid, kes vargsi toovad sisse hukutavaid eksiõpetusi ja salgavad ära Issanda, kes on nad vabaks ostnud. Nad tõmbavad iseeneste peale äkilise hukatuse.
2Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
2Ja paljud järgivad neid nende kõlvatuses ning nende tõttu teotatakse tõe teed.
3Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
3Ja ahnitsedes püüavad nad teid võltside sõnadega ära osta. Nende mõõt on ammu juba täis ja nende hukatus ei tuku.
4Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu.
4Jah, Jumal ei säästnud patustanud ingleidki, vaid tõukas nad põrgupimeduse soppidesse kinnipidamiseks kuni kohtuni.
5Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
5Ta ei säästnud muistset maailma, vaid, saates jumalakartmatute maailma peale veeuputuse, kaitses üksnes õigusekuulutajat Noad ning tema omasid, kokku kaheksat;
6Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
6ta muutis tuhaks Soodoma ja Gomorra linnad, mõistes need hukka hävinguks ja pannes hoiatustähiseks tulevastele jumalakartmatutele.
7Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
7Ta kiskus hukatusest välja õige mehe Loti, keda kõlvatud inimesed vaevasid oma liiderliku eluviisiga,
8Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
8sest nende seas elades ning kõike seda nähes ja kuuldes oli see õige piinanud oma õiglast hinge päevast päeva ülekohtuste tegude pärast.
9Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
9Nii oskab Issand küll jumalakartlikke kiusatusest välja kiskuda, ülekohtusi aga nuhtlemiseks kinni pidada kohtupäevani.
10hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
10Iseäranis nuhtleb Issand neid, kes rüvedas himus elavad lihaliku loomuse järgi ning põlgavad Issanda valitsust. Need on jultunud ja ennast täis ega põrka tagasi teotamast kirkuseingleid,
11Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
11kuigi isegi inglid, kellel on rohkem jõudu ja väge, ei lausu nende kohta teotavat otsust Issanda ees.
12Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
12Ent need on nagu mõistmatud loomad, kes on loomu poolest sündinud püüdmiseks ja hukkamiseks; nad teotavad seda, mida nad ei mõista, ja hukkuvad oma hukatuses,
13na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
13karistatuna ülekohtu eest ülekohtu palgaga. Nad peavad lõbuks priisata päise päeva ajal, need mustuse- ja häbiplekid, kes turgutavad end oma lõbudes, kui nad pidutsevad koos teiega.
14Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
14Nende silmad on täis abielurikkumist ning neil ei saa kunagi patust küllalt, nad ahvatlevad kõikuvaid hingi, neil on ahnitsema harjunud süda, nad on needuse lapsed.
15Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
15Nad on loobunud otseteest ja eksinud ära, järgides teed, mida läks Beori poeg Bileam, kes armastas ülekohtu palka,
16akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
16sai aga noomida oma üleastumise pärast: hääletu koormaloom rääkis inimhäälega ja takistas prohveti meeletust.
17Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
17Need on veeta allikad, marust aetavad udupilved, neile on määratud pilkane pimedus.
18Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
18Sest rääkides tühiseid ja õõnsaid sõnu, ahvatlevad nad kõlvatute lihahimudega neid, kes hiljuti on jõudnud ära põgeneda eksituses elavate seast,
19Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu--maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
19kes, tõotades teistele vabadust, on ise kaduvuse orjad; sest kellele on keegi alistatud, selle orjaks ta on saanud.
20Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
20Kui nad on kord ära põgenenud maailma saastast meie Issanda ja Päästja Jeesuse Kristuse tunnetuse kaudu, pärast aga jälle vajuvad sellesse saasta ja jäävad alla, siis on ju nende viimane lugu halvem kui esimene.
21Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
21Sest neile oleks olnud parem, et õiguse tee oleks neile jäänud tundmata, kui et seda äratundnuna pöörata selg nende kätte antud pühale käsule.
22Ipo mithali isemayo: "Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe," na nyingine isemayo: "Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!" Ndivyo ilivyo kwao sasa.
22Nendele on tulnud kätte see, mida tõeline vanasõna ütleb: 'Koer pöördub tagasi oma okse juurde' ja 'Pestud emis läheb porisse püherdama'.