1Mimi Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo, nawaandikia ninyi ambao, kwa wema wake Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo, mmejaliwa imani ileile ya thamani kuu tuliyojaliwa sisi.
1Siimeon Peetrus, Jeesuse Kristuse sulane ja apostel - neile, kelle osaks on saanud meie omaga sama kallis usk meie Jumala ja Päästja Jeesuse Kristuse õiguse läbi:
2Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
2Armu ja rahu saagu teile rohkesti Jumala ja Jeesuse, meie Issanda tundmise kaudu!
3Kwa uwezo wake wa kimungu, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji, ili tuishi maisha ya kumcha Mungu kwa kumjua yeye aliyetuita tuushiriki utukufu na wema wake yeye mwenyewe.
3Tema jumalik vägi on meile kinkinud kõik, mis on vajalik eluks ja vagaduseks, tema tundmise kaudu, kes meid on kutsunud omaenese kirkuse ja väärikusega.
4Kwa namna hiyo ametujalia zawadi kuu na za thamani ambazo alituahidia, ili kwa zawadi hizo mpate kuziepa kabisa tamaa mbaya zilizomo duniani, na mpate kuishiriki hali yake ya kimungu.
4Sel viisil on meile kingitud kõige kallimad ja suuremad tõotused, et te nende kaudu võiksite põgeneda kaduvusest, mis valitseb maailmas himude tõttu, ja saada jumaliku loomuse osaliseks.
5Kwa sababu hiyo, fanyeni bidii ya kuongeza fadhila katika imani yenu: ongezeni elimu katika fadhila yenu,
5Just seepärast te peategi olema kõigiti valmis arendama oma usus voorust, vooruses tunnetust,
6kuwa na kiasi katika elimu yenu, uvumilivu katika kuwa na kiasi, uchaji wa Mungu katika uvumilivu wenu,
6tunnetuses kasinust, kasinuses kannatlikkust, kannatlikkuses vagadust,
7udugu katika uchaji wenu, na mapendo katika udugu wenu.
7vagaduses vennalikkust, vennalikkuses armastust,
8Mkiwa na sifa hizo zote kwa wingi, zitawawezesheni kuwa watendaji na kupata faida katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
8sest kui teil seda kõike on, ja veel rikkalikult, siis te ei jää laisaks ega viljatuks meie Issanda Jeesuse Kristuse tundmises;
9Lakini mtu asiye na sifa hizo ni kipofu, hawezi kuona na amesahau kwamba alikwisha takaswa dhambi zake za zamani.
9kuid kellel seda pole, on pime ja lühinägelik; ta on unustanud, et on puhastatud oma endistest pattudest.
10Kwa hiyo basi, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuufanya huo wito wenu mlioitiwa na Mungu uwe jambo la kudumu katika maisha yenu; kama mkiishi namna hiyo hamtaanguka kamwe.
10Seepärast, vennad, olge veelgi innukamad kindlustama oma kutsumist ja äravalimist, sest kui te seda teete, ei väärata te iial.
11Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
11Sest nõnda võimaldatakse teile takistamatu sissepääs meie Issanda ja Päästja Jeesuse Kristuse igavesse kuningriiki.
12Kwa hiyo nitaendelea kuwakumbusheni daima mambo haya, ingawa mmekwisha yafahamu, na mko imara katika ukweli mlioupokea.
12Seepärast ma tahan teile kõike seda üha meelde tuletada, kuigi te seda küll teate ja olete kinnitatud teile antud tões.
13Nadhani ni jambo jema kwangu, muda wote niishio hapa duniani, kuwapeni moyo na kuwakumbusheni juu ya mambo haya.
13Ma pean aga õigeks teid meenutamise abil virgutada, niikaua kui ma olen selles telgis,
14Najua kwamba karibu nitauweka kando mwili huu wenye kufa, kama Bwana alivyoniambia waziwazi.
14teades, et mu telgi mahavõtmine on varsti käes, nagu ka meie Issand Jeesus Kristus on mulle seda teatanud.
15Basi, nitajitahidi kuwapatieni njia ya kuyakumbuka mambo haya kila wakati, baada ya kufariki kwangu.
15Aga ma tahan hoolt kanda, et teie igal ajal ka pärast minu lahkumist võiksite neid asju mäletada.
16Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe.
16Meie Issanda Jeesuse Kristuse väge ja tulemist ei ole me teile teatanud mingeid targutavaid müüte jäljendades, vaid me oleme tema suurust näinud oma silmaga.
17Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na kutukuzwa na Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: "Huyu ni Mwanangu mpenzi, nimependezwa naye."
17Sest ta sai au ja kirkust Jumalalt Isalt, kui ilmvõrratult kirkuselt kostis talle hääl: 'See on minu armas Poeg, temast on mul hea meel!' -
18Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
18Ja seda häält me kuulsime tulevat taevast, kui me olime koos temaga pühal mäel.
19Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka Siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
19Ja nii on meil midagi kindlamat prohvetisõnast ja te teete hästi, kui panete tähele seda nagu lampi, mis paistab hämaras paigas, kuni päev hakkab hahetama ning koidutäht tõuseb teie südameis.
20Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu.
20Seda mõistke esmalt, et ühtki prohvetiennustust Pühakirjas ei või omapäi seletada,
21Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
21sest iialgi pole ühtegi prohvetiennustust esile toodud inimese tahtel, vaid Pühast Vaimust kantuina on inimesed rääkinud, saades sõnumi Jumala käest.