1Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
1Aga kui Apollos oli Korintoses, sündis, et Paulus käis läbi ülamaakonnad ja tuli alla Efesosse. Ja leides sealt mõned jüngrid,
2Akauliza, "Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?" Nao wakamjibu, "La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia."
2küsis ta neilt: 'Kas te võtsite vastu Püha Vaimu, kui te saite usklikuks?' Nemad aga vastasid: 'Me ei ole kuulnudki, et Püha Vaim on.'
3Naye akasema, "Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?" Wakamjibu, "Ubatizo wa Yohane."
3Ja tema ütles: 'Millesse siis teie olete ristitud?' Nemad vastasid: 'Johannese ristimisse.'
4Naye Paulo akasema, "Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu."
4Aga Paulus ütles: 'Johannes ristis meeleparandusristimisega, öeldes rahvale, et nad usuksid sellesse, kes tuleb pärast teda, see tähendab Jeesusesse.'
5Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
5Seda kuuldes lasksid nad endid ristida Issanda Jeesuse nimesse.
6Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
6Ja kui Paulus pani oma käed nende peale, tuli neile Püha Vaim ja nad rääkisid võõraid keeli ja ennustasid.
7Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
7Neid oli kokku umbes tosin meest.
8Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
8Paulus läks siis sünagoogi ning rääkis julgesti kolm kuud, väideldes ja veendes inimesi Jumala riigi asjus.
9Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
9Aga kui mõned tegid südame kõvaks, ei võtnud sõna vastu ja halvustasid usuteed kogukonna silmis, siis ta eemaldus nende juurest ja eraldas ka jüngrid ning pidas iga päev arutlusi Türannose koolis.
10Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
10See kestis kaks aastat, nii et kõik, kes Aasias elasid, nii juudid kui kreeklased, said kuulda Issanda sõna.
11Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
11Ja Jumal tegi iseäralikke vägevaid tegusid Pauluse käte läbi,
12Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
12nii et ka tema naha pealt võetud higirätikuid ja põllesid viidi haigete peale ja tõved lahkusid neist ning kurjad vaimud läksid välja.
13Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: "Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri."
13Aga mõned rändajad juudid, kes vaime välja ajasid, katsusid lausuda Issanda Jeesuse nime nende üle, kelles oli kurje vaime, üteldes: 'Ma vannutan teid Jeesuse nimel, keda Paulus kuulutab!'
14Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
14Seda tegid ühe juudi ülempreestri Skeua seitse poega.
15Lakini pepo mbaya aliwajibu, "Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?"
15Ent kuri vaim kostis neile: 'Jeesust ma tunnen ja Paulust ma tean, aga kes teie olete?'
16Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
16Ja inimene, kelles oli kuri vaim, kargas neile kallale, sai võimust nende üle ja võitis nad ära, nii et nad alasti ja haavatuna põgenesid sellest kojast.
17Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
17See lugu sai teatavaks kõigile juutidele ja kreeklastele, kes elasid Efesoses, ja hirm langes nende kõikide peale ja Issanda Jeesuse nime kiideti suureks.
18Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
18Ja paljud nendest, kes olid saanud usklikuks, tulid ning tunnistasid ja rääkisid oma tegudest.
19Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
19Aga paljud neist, kes olid tegelnud nõiakunstiga, tõid oma raamatud kokku ja põletasid need ära kõikide silma all. Ja kui nende hind kokku arvestati, leiti see olevat viiskümmend tuhat hõberaha.
20Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
20Nõnda võimsalt kasvas ja tugevnes Issanda sõna.
21Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, "Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia."
21Pärast neid sündmusi võttis Paulus vaimus ette minna Makedoonia ja Ahhaia kaudu Jeruusalemma ja ütles: 'Kui ma seal olen ära käinud, pean ma nägema ka Rooma linna.'
22Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
22Ta läkitas Makedooniasse kaks oma abilist, Timoteose ja Erastose, ise jäi aga veel mõneks ajaks Aasiasse.
23Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
23Aga tol ajal tekkis usutee pärast suur rahutus.
24Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
24Sest üks hõbesepp, Demeetrios nimi, tegi Artemise templi hõbekujukesi ja muretses sellega käsitöölistele rohkesti tööd.
25Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, "Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
25Ta kogus kokku nood ning muud oma ärile kaasaaitajad ja ütles: 'Mehed, te teate, et meie heaolu sõltub sellest tööst,
26Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
26ja te näete ja kuulete, et see Paulus veenab ja juhib kõrvale rohkesti rahvast mitte ainult Efesoses, vaid peaaegu kogu Aasia provintsis, öeldes, et kätega valmistatud asjad ei ole jumalad.
27Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha."
27Ja nõnda ähvardab põlu alla sattumine mitte üksnes seda meie tööala, vaid ka suure jumalanna Artemise templit ei peeta enam millekski ja kaob tema suur ülevus, ehkki teda kummardab kogu Aasia ja ilmamaa.'
28Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: "Mkuu ni Artemi, wa Efeso!"
28Seda kuuldes said nad täis raevu ja hakkasid hüüdma: 'Suur on efeslaste Artemis!'
29Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
29Ja terve linn hakkas mässama ja nad sööstsid üksmeelselt teatrisse, lohistades kaasa makedoonlased Gaiuse ja Aristarhose, Pauluse matkakaaslased.
30Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
30Aga kui Paulus tahtis rahvakoosolekule minna, ei lasknud jüngrid teda.
31Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
31Isegi mõned Aasiamaa ülemad, kes olid ta sõbrad, saatsid mehi ta juurde paluma, et ta ei näitaks end teatris.
32Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
32Ühed karjusid nüüd üht, teised teist, sest rahvakogu oli segaduses, suurem hulk ei teadnudki, misjaoks nad olid kokku tulnud.
33Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
33Siis mõned rahva hulgast selgitasid olukorda Aleksandrosele, kelle juudid olid ette lükanud. Aleksandros aga viipas käega, tahtes pidada rahvakoosoleku ees kaitsekõnet.
34Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: "Mkuu ni Artemi wa Efeso!" Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
34Aga kui nad mõistsid, et ta on juut, tõstsid nad kisa ja karjusid kõik nagu ühest suust ligi kaks tundi: 'Suur on efeslaste Artemis!'
35Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, "Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
35Aga linnakirjutaja vaigistas viimaks rahva ja lausus: 'Efesose mehed, kas on ühtegi inimest, kes ei tea, et efeslaste linn on suure Artemise ja tema taevast mahalangenud kuju hoidja?
36Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
36Et see on vaieldamatu tõsiasi, siis on teie kohus vait olla ja mitte midagi ennatlikult ette võtta.
37Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
37Te ju olete siia toonud need mehed, kes ei ole templiriisujad ega meie jumalanna teotajad.
38Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
38Kui nüüd Demeetriosel ja temaga koos olevatel käsitöölistel on kellegi peale kaebamist, siis selleks peetakse kohtupäevi ja on olemas maavalitsejad; süüdistagu nad seal üksteist.
39Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
39Ja kui teil on veel mingeid nõudmisi, siis arutatakse seda korralisel rahvakoosolekul.
40Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo."
40Meie oleme ju ohus, et meid tänase kokkutormamise pärast süüdistatakse mässutõstmises, milleks ei olnud mingit põhjust ja millest me ei suuda aru anda.' Ja nende sõnadega õnnestus tal rahvakoosolek laiali saata.
41Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.