Swahili: New Testament

Estonian

Acts

18

1Baada ya hayo, Paulo aliondoka Athene, akaenda Korintho.
1Pärast seda lahkus Paulus Ateenast ja tuli Korintosesse.
2Huko Korintho, alimkuta Myahudi mmoja aitwaye Akula, mzaliwa wa Ponto. Akula pamoja na mkewe aitwaye Priskila, walikuwa wamerudi kutoka Italia siku hizohizo kwa sababu Kaisari Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Roma. Paulo alikwenda kuwaona,
2Ja ta leidis juudi, Akvila nimi, Pontosest pärit, kes oli hiljuti tulnud Itaaliast koos oma naise Priskillaga, kuna keiser Klaudius oli käskinud kõigil juutidel Roomast lahkuda. Nende juurde tuli Paulus.
3na kwa vile wao walikuwa mafundi wa kushona mahema kama alivyokuwa yeye, Paulo alikaa nao akafanya kazi.
3Ja et tal oli nendega sama amet, siis ta jäi nende juurde ja nad tegid koos tööd. Nad olid elukutse poolest telgitegijad.
4Kila Sabato alifanya majadiliano katika sunagogi akijaribu kuwavuta Wayahudi na Wagiriki.
4Igal hingamispäeval Paulus arutles ja väitles sünagoogis, püüdes veenda nii juute kui ka kreeklasi.
5Baada ya Sila na Timotheo kuwasili kutoka Makedonia, Paulo alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri, akawathibitishia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo.
5Kui aga Siilas ja Timoteos Makedooniast sinna tulid, pühendus Paulus täielikult sõna kuulutamisele ning tunnistas juutidele, et Jeesus on Messias.
6Walipompinga na kuanza kumtukana, aliyakung'uta mavazi yake mbele yao akisema, "Mkipotea ni shauri lenu wenyewe; mimi sina lawama yoyote juu ya jambo hilo. Na tangu sasa nitawaendea watu na mataifa mengine."
6Aga kui need talle vastu panid ja pilkasid, raputas ta tolmu oma rõivastelt ja ütles neile: 'Teie veri tulgu teie pea peale! Mina olen puhas! Nüüdsest peale lähen ma paganate juurde.'
7Basi, akatoka hapo akaenda kukaa nyumbani kwa mtu mmoja mcha Mungu aitwaye Tito Yusto. Nyumba yake Tito ilikuwa karibu na lile sunagogi.
7Ja ta lahkus nende seast ja tuli ühe jumalakartliku mehe kotta, Titius Justus nimi, kelle koda külgnes sünagoogiga.
8Lakini Krispo, mkuu wa sunagogi, alimwamini Bwana yeye pamoja na jamaa yake yote. Wakorintho wengi waliusikiliza ujumbe huo, wakaamini na kubatizwa.
8Sünagoogi ülem Krispus hakkas kogu oma perega uskuma Issandat ja palju korintlasi hakkas Paulust kuulates uskuma ning nad ristiti.
9Siku moja usiku, Bwana alimwambia Paulo katika maono: "Usiogope, endelea kuhubiri tu bila kufa moyo,
9Aga Issand ütles öösel nägemuses Paulusele: 'Ära karda, vaid räägi, ja ära ole vait!
10maana mimi niko pamoja nawe. Hakuna mtu atakayejaribu kukudhuru maana hapa mjini pana watu wengi walio upande wangu."
10Sest mina olen sinuga ja keegi ei tule sinu kallale sulle kurja tegema, sest mul on palju rahvast siin linnas.'
11Basi, Paulo alikaa huko akifundisha neno la Mungu kati yao kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.
11Siis ta peatus seal ühe aasta ja kuus kuud, õpetades nende seas Jumala sõna.
12Lakini wakati Galio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Akaya, Wayahudi walimvamia Paulo kwa pamoja na kumpeleka mahakamani.
12Aga kui Gallio oli Ahhaia maavalitseja, tõusid juudid üksmeelselt Pauluse vastu, viisid ta kohtujärje ette
13Wakasema, "Tunamshtaki mtu huyu kwa sababu ya kuwashawishi watu wamwabudu Mungu kwa namna inayopingana na Sheria."
13ja ütlesid: 'Tema meelitab inimesi Jumalat teenima Moosese Seaduse vastaselt.'
14Kabla tu Paulo hajaanza kusema, Galio aliwaambia Wayahudi, "Sikilizeni enyi Wayahudi! Kama kweli jambo hili lingekuwa juu ya uhalifu au uovu ningekuwa tayari kuwasikilizeni.
14Aga kui Paulus tahtis oma suu avada, lausus Gallio juutidele: 'Kui see oleks mõni ebaõiglus või kuritöö, oh juudid, siis ma peaksin muidugi teie kaebuse ära kuulama.
15Lakini kama ni shauri la ubishi kuhusu maneno na majina ya Sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitaki kuwa hakimu wa mambo haya!"
15Aga kui need on vaidlusküsimused õpetuse ja nimede ja teie Seaduse pärast, siis katsuge ise toime tulla. Neis asjus ei taha mina olla kohtumõistja.'
16Basi, akawafukuza kutoka mahakamani.
16Ja ta ajas nad ära kohtujärje eest.
17Nao wote wakamkamata Sosthene ambaye alikuwa kiongozi wa sunagogi, wakampiga palepale mbele ya mahakama. Lakini Galio hakujali kitendo hicho hata kidogo.
17Aga nemad kõik haarasid kinni sünagoogi ülemast Soostenesest ja peksid teda kohtujärje ees. Gallio ei hoolinud aga sellest vähimatki.
18Paulo alikaa bado na wale ndugu huko Korintho kwa siku nyingi. Kisha aliwaaga, akapanda meli kwenda Siria pamoja na Priskila na Akula. Huko Kenkrea, alinyoa nywele zake kwa sababu ya nadhiri aliyokuwa ameweka.
18Paulus jäi sinna veel mitmeks päevaks. Siis ta jättis vennad jumalaga ja purjetas koos Priskilla ja Akvilaga Süüriasse. Kenkreas oli ta lasknud oma juuksed maha lõigata, sest ta oli andnud tõotuse.
19Walifika Efeso na hapo Paulo aliwaacha Priskila na Akula, akaenda katika sunagogi, akajadiliana na Wayahudi.
19Nad saabusid Efesosse ja ta jättis nad sinna. Ta ise läks aga sünagoogi ning arutles ja väitles juutidega.
20Walimwomba akae nao muda mrefu zaidi, lakini hakupenda.
20Aga kui nood palusid teda jääda kauemaks, siis Paulus ei olnud nõus,
21Bali alipokuwa anaondoka, alisema, "Mungu akipenda nitakuja kwenu tena." Akaondoka Efeso kwa meli.
21vaid jättis nad jumalaga ja ütles: 'Ma tulen tagasi teie juurde, kui Jumal tahab.' Ja ta purjetas Efesosest ära.
22Meli ilitia nanga Kaisarea, naye Paulo akaenda Yerusalemu kulisalimia lile kanisa, kisha akaenda Antiokia.
22Kui nad maabusid Kaisareas, läks ta Jeruusalemma, tervitas kogudust ja läks edasi Antiookiasse.
23Alikaa huko muda mfupi, halafu akaendelea na safari kwa kupitia sehemu za Galatia na Frugia akiwatia moyo wafuasi wote.
23Kui ta oli seal mõnda aega olnud, läks ta ära ja käis järjest läbi Galaatia maakonna ja Früügia, kinnitades kõiki jüngreid.
24Myahudi mmoja aitwaye Apolo, mzaliwa wa Aleksandria, alifika Efeso. Alikuwa mtu mwenye ufasaha wa kuongea na mwenye ujuzi mkubwa wa Maandiko Matakatifu.
24Aga keegi juut, Apollos nimi, Aleksandriast pärit, vahva kõnemees ja vägev kirjaseletaja, tuli Efesosse.
25Alikuwa amefundishwa juu ya hiyo njia ya Bwana, na akiwa motomoto, aliongea juu ya habari za Yesu. Akafundisha kwa usahihi ingawa alikuwa amepata ubatizo wa Yohane tu.
25Teda oli õpetatud tundma Issanda teed ja vaimult keevalisena ta rääkis ja õpetas täpselt Jeesusest, aga teadis ainult Johannese ristimist.
26Priskila na Akula walipomsikia akiongea kwa uhodari ndani ya sunagogi, walimchukua kwao wakamfundisha hiyo Njia ya Mungu kwa usahihi zaidi.
26Tema hakkas siis julgesti sünagoogis kõnelema. Kui aga Priskilla ja Akvila teda kuulsid, võtsid nad ta enda juurde ja seletasid talle Jumala tee täpsemini ära.
27Apolo alipoamua kwenda Akaya, wale ndugu walimtia moyo kwa kuwaandikia wafuasi kule Akaya wampokee. Alipofika huko, aliweza kwa msaada wa neema ya Mungu, kuwasaidia sana wale ndugu waliopata kuwa waumini;
27Aga kui ta tahtis minna Ahhaiasse, kirjutasid vennad teda julgustades jüngritele, et nad ta vastu võtaksid. Kui Apollos sinna jõudis, siis ta tõi palju kasu neile, kes olid hakanud uskuma armu läbi.
28kwa maana aliendelea kwa uhodari kuwashinda Wayahudi hadharani akithibitisha kwa Maandiko Matakatifu kuwa Yesu ni Kristo.
28Sest ta kummutas osavalt juutide väited, näidates avalikult Pühakirjast, et Jeesus on Messias.