1Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
1Nad matkasid läbi Amfipolise ja Apolloonia ning tulid Tessaloonikasse, kus oli juudi sünagoog.
2Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
2Ja Paulus astus oma harjumust mööda nende juurde sisse ning arutles ja väitles nendega kolmel hingamispäeval Pühakirja üle,
3Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, "Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo."
3selgitades ja tõestades, et Messias pidi kannatama ja surnuist üles tõusma: 'Tema ongi Messias - see Jeesus, keda mina teile kuulutan.'
4Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
4Ja mõned neist lasksid end veenda ja liitusid Pauluse ja Siilasega, samuti suur hulk jumalakartlikke kreeklasi ja rohkesti suursuguseid naisi.
5Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
5Juudid läksid aga kadedaks ja võtsid enestega turuplatsidelt mõningaid nurjatuid mehi ja rahvahulki koondades muutsid linna rahutuks. Rünnates Jaasoni koda, püüdsid nad apostleid rahva ette tuua.
6Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: "Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
6Aga kui neid ei leitud, siis nad vedasid Jaasoni ja mõned vennad linna ülemate ette ning hüüdsid: 'Need, kes kogu maal rahutusi tekitavad, need on ka siia tulnud.
7Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu."
7Jaason on nad vastu võtnud; ja nad kõik rikuvad keisri korraldusi, öeldes ühe teise olevat kuninga, kellegi Jeesuse.'
8Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
8Seda kuuldes rahvas ja linna ülemad ärritusid,
9Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
9kuid saades Jaasonilt ja teistelt tagatise, lasksid nad nemad vabaks.
10Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
10Vennad saatsid siis kohe Pauluse ja Siilase öö varjus Beroiasse. Kui nad olid sinna jõudnud, läksid nad juudi sünagoogi.
11Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
11Sealsed olid üllameelsemad kui Tessaloonika omad, nemad võtsid sõna vastu täie innuga ja uurisid iga päev Pühakirjast, kas see on nõnda.
12Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
12Paljud neist hakkasid uskuma, samuti rohkesti kõrgemast seisusest kreeka naisi ja mehi.
13Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
13Kui aga Tessaloonika juudid said teada, et Paulus ka Beroias kuulutab Jumala sõna, tulid nad sinnagi rahvast ässitama ja segadusse ajama.
14Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
14Siis saatsid vennad Pauluse kohe mere äärde, Siilas ja Timoteos jäid aga paigale.
15Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
15Pauluse saatjad viisid ta Ateenani ja läksid ise ära, kui nad olid saanud Siilase ja Timoteose jaoks käsu, et need võimalikult ruttu tuleksid Pauluse juurde.
16Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
16Aga kui Paulus neid Ateenas ootas, siis ta ärritus vaimus, nähes linna ebajumalakujusid täis olevat.
17Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
17Ta arutles ja väitles nüüd sünagoogis juutide ja proselüütidega ning turul iga päev nendega, kes tema juurde juhtusid.
18Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, "Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?" Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, "Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni."
18Aga mõned epikuurlaste ja stoikute mõttetargad vaidlesid temaga. Ühed ütlesid: 'Mida see lobasuu tahab öelda?' Teised aga: 'Tema näib kuulutavat võõraid vaime.' Sest ta kuulutas neile evangeeliumi Jeesusest ja ülestõusmisest.
19Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, "Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
19Ja nad võtsid ta kinni ja viisid Areopaagile, sõnades: 'Kas me võime teada saada, mis uus õpetus see on, mida sa räägid?
20Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani."
20Sest sa tood meie kõrvu võõrastavaid asju. Me tahame nüüd teada saada, mis need õige on.'
21Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
21Kõigil ateenlastel ja seal elavatel muulastel ei olnud ju muuks aega, kui vaid rääkida ja kuulata midagi uut.
22Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, "Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
22Paulus jäi seisma keset Areopaagi ja ütles: 'Ateena mehed, ma näen, et te olete haruldaselt jumalakartlikud,
23Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
23sest kui ma läksin läbi linna ja teie pühamuid silmitsesin, leidsin ka sellise altari, millele on kirjutatud: 'Tundmatule Jumalale.' Keda teie nüüd kui tundmatut teenite, teda kuulutan mina teile.
24Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
24Jumal, kes on teinud maailma ja kõik, mis siin sees, kes taeva ja maa Issandana ei ela templites, mis on kätega tehtud,
25Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
25ega lase ennast ka inimkätega teenida, nagu oleks tal midagi vaja, - tema ise annab kõikidele elu ja õhu ja kõik.
26Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
26Tema on teinud ühestainsast terve inimkonna elama kogu ilmamaa peal ning on neile seadnud ettemääratud ajad ja nende asukohtade piirid,
27Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
27et nad otsiksid Jumalat, kas nad ehk saaksid teda käega katsuda ja leida, kuigi tema küll ei ole kaugel ühestki meist,
28Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
28sest tema sees meie elame ja liigume ja oleme, nagu ka mõned teie luuletajaist on öelnud: 'Sest ka meie oleme tema sugu.'
29Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
29Kui me nüüd oleme Jumala sugu, siis ei tohi me arvata, et jumalus on kulla või hõbeda või kivi sarnane või nagu inimeste oskuse ja kujutluse loodud.
30Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
30Jumal on küll selliseid teadmatuse aegu sallinud, kuid nüüd käsib ta kõigil inimestel kõigis paigus meelt parandada.
31Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!"
31Sest ta on seadnud ühe päeva, mil ta mõistab õiglaselt kohut kogu ilmamaa üle mehe läbi, kelle ta on määranud, ja ta on pakkunud kõigile tõestuse sellega, et on tema üles äratanud surnuist.'
32Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, "Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!"
32Kuuldes surnute ülestõusmisest, hakkasid mõned pilkama, teised aga ütlesid: 'Me tahame sinult selle kohta veel teinegi kord kuulda.'
33Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
33Nõnda läks Paulus nende keskelt ära.
34Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.
34Aga mõned mehed ühinesid temaga ja said usklikuks, nende seas ka Areopaagi liige Dionüüsios, ja üks naine, Damaris nimi, ja teisigi koos nendega.