1Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
1Paulus saabus Derbesse ja Lüstrasse. Ja vaata, seal oli jünger, uskliku juudi naise poeg, aga kreeka isast, Timoteos nimi,
2Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
2kelle kohta Lüstra ja Ikoonioni vennad andsid hea tunnistuse.
3Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
3Paulus tahtis teda enesega teele kaasa. Ja ta võttis ning lõikas tema ümber kohalike juutide pärast, sest need kõik teadsid, et Timoteose isa oli olnud kreeklane.
4Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
4Kui nad siis linnu mööda käisid, andsid nad kogudustele täitmiseks need korraldused, mis apostlid ja vanemad Jeruusalemmas olid otsustanud.
5Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
5Nõnda siis kinnitati kogudusi usus ja nende arv kasvas päevast päeva.
6Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
6Ja nemad läksid läbi Früügia- ja Galaatiamaa, sest Püha Vaim oli keelanud neil sõna rääkimast Aasias.
7Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
7Kui nad jõudsid Müüsiani, püüdsid nad matkata Bitüüniasse, aga Jeesuse Vaim ei lubanud.
8Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
8Nii tulid nad Müüsiast möödudes alla Troasesse.
9Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: "Vuka, uje Makedonia ukatusaidie."
9Ja Paulus nägi öösel nägemuse: üks makedoonia mees seisis ja palus teda: 'Tule meie juurde Makedooniasse ja aita meid!'
10Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
10Kui ta oli seda nägemust näinud, püüdsime kohe minna Makedooniasse, olles veendunud, et Issand on meid kutsunud neile evangeeliumi kuulutama.
11Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
11Siis me purjetasime Troasest välja ja tulime otseteed Samotraakesse, järgmisel päeval aga Neapolisse
12Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
12ja sealt Filippisse, mis on tähtsaim linn tolles Makedoonia osas, Rooma koloonia. Selles linnas me viibisime mõned päevad.
13Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
13Ja hingamispäeval me läksime linnaväravast välja jõe äärde, kus me arvasime olevat palvepaiga. Me istusime maha ja rääkisime kokkutulnud naistega.
14Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
14Ka üks jumalakartlik naine, Lüüdia nimi, purpurimüüja Tüatiira linnast, kuulas, ning Issand avas tema südame, nii et ta pani tähele, mida Paulus rääkis.
15Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, "Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae." Akatuhimiza twende.
15Aga kui Lüüdia ja ta pere olid ristitud, palus ta meid: 'Tulge minu kotta ja jääge sinna, kui te arvate, et ma olen ustav Issandale!' Ja ta käis meile peale.
16Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
16Aga sündis, et kui me läksime palvepaika, tuli meile vastu orjatar, kellel oli lausuja vaim, see tõi oma isandatele palju kasu ennustamisega.
17Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, "Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu."
17Tema käis Pauluse ja meie kannul ning hüüdis: 'Need inimesed on kõigekõrgema Jumala sulased, kes kuulutavad teile päästmise teed.'
18Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, "Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!" Mara huyo pepo akamtoka.
18Seda tegi ta mitu päeva. Aga Paulus ägestus, pöördus ümber ja ütles vaimule: 'Ma käsin sind Jeesuse Kristuse nimel: mine temast välja!' Ja vaim läks välja samal tunnil.
19Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
19Kui nüüd orjatari isandad nägid, et nende kasulootus on kustunud, haarasid nad Pauluse ja Siilase ning vedasid nad turule ülemate juurde.
20Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, "Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
20Nad viisid nad võimukandjate ette ja ütlesid: 'Need inimesed tekitavad meie linnas segadust. Nad on juudid
21Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata."
21ja kuulutavad kombeid, mida meie kui roomlased ei tohi omaks võtta ega järgida.'
22Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
22Ja rahvahulk tõusis nende vastu. Võimukandjad kiskusid rõivad nende seljast ja käskisid neid keppidega peksta.
23Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
23Ja kui nad olid neile palju hoope andnud, heitsid nad apostlid vangi ja käskisid vangivalvurit neid hoolsalt valvata.
24Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
24Niisuguse range käsu saanud, heitis valvur nad sisemisse vangikongi ja pani nende jalad pakku.
25Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
25Kesköö paiku Paulus ja Siilas palvetasid ja laulsid Jumalat kiites, ning vangid kuulasid neid.
26Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
26Aga äkitselt sündis nii suur maavärisemine, et vangihoone alused vappusid. Ja otsekohe avanesid kõik uksed ja kõikide köidikud pääsesid valla.
27Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
27Kui nüüd vangivalvur unest ärkas ja nägi vanglaukse lahti olevat, tõmbas ta mõõga ja tahtis end tappa, arvates, et vangid on põgenenud.
28Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: "Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa."
28Paulus hüüdis aga valju häälega: 'Ära tee enesele kurja, sest me kõik oleme siin!'
29Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
29Siis palus valvur tuld, tormas sisse ja heitis värisedes Pauluse ja Siilase ette maha,
30Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, "Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?"
30tõi nad välja ning ütles: 'Isandad, mis ma pean tegema, et pääseda?'
31Wao wakamjibu, "Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote."
31Aga nemad ütlesid: 'Usu Issandasse Jeesusesse, siis pääsed sina ja su pere!'
32Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
32Ja nad rääkisid Issanda sõna temale ja kõigile, kes olid tema kojas.
33Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
33Ja vangivalvur võttis nad tollel öötunnil enda juurde ja pesi nende haavad. Ning otsekohe ristiti tema ja kõik ta omaksed.
34Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
34Siis ta viis nad oma kotta, kattis neile laua ja oli ülirõõmus, et ta kogu perega oli hakanud uskuma Jumalasse.
35Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, "Wafungueni wale watu."
35Kui valgeks läks, läkitasid võimukandjad kohtuteenrid ütlema: 'Lase need inimesed vabaks!'
36Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: "Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani."
36Vangivalvur teatas need sõnad Paulusele: 'Võimukandjad on saatnud sõna, et teid vabaks lastaks. Tulge siis nüüd välja ja minge rahuga!'
37Lakini Paulo alimjibu, "Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie."
37Paulus aga vastas neile: 'Nad on meid avalikult peksnud ilma kohut mõistmata, ent meie oleme Rooma kodanikud; nad on meid vangi heitnud ja tahavad nüüd meid salaja välja ajada?! Nii see ikka ei lähe! Tulgu nad ise ja viigu meid välja!'
38Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
38Kohtuteenrid andsid need sõnad võimukandjaile edasi. Kui nood kuulsid, et apostlid on Rooma kodanikud, lõid nad kartma
39Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
39ning tulid ja palusid neilt vabandust, tõid nad välja ja palusid linnast lahkuda.
40Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.
40Siis tulid apostlid vanglast välja ja läksid Lüüdia poole. Ja kui nad vendi olid näinud ja julgustanud, läksid nad minema.