Swahili: New Testament

Estonian

Acts

15

1Basi, watu wengine walifika Antiokia kutoka Yudea wakaanza kuwafundisha wale ndugu wakisema, "Kama hamtatahiriwa kufuatana na mapokeo ya Sheria ya Mose, hamtaweza kuokolewa."
1Siis tulid mõned Juudamaalt alla ja õpetasid vendi: 'Kui te ei lase endid Moosese kombe järgi ümber lõigata, siis te ei või pääseda.'
2Jambo hili lilisababisha ubishi mkubwa, na baada ya Paulo na Barnaba kujadiliana nao, ikaamuliwa Paulo na Barnaba pamoja na waumini kadhaa wa lile kanisa la Antiokia waende Yerusalemu kuwaona wale mitume na wazee kuhusu jambo hilo.
2Et sellest tuli tüli ning Paulusel ja Barnabasel oli nendega palju vaidlemist, siis määrati nii, et Paulus, Barnabas ja mõned muud nende seast lähevad selle tüliküsimuse pärast Jeruusalemma apostlite ja vanemate juurde.
3Basi, kanisa liliwaaga, nao walipokuwa wanapitia Foinike na Samaria waliwaeleza watu jinsi mataifa mengine yalivyomgeukia Mungu. Habari hizo zikawafurahisha sana ndugu hao wote.
3Siis kogudus saatis nad teele ja nad läksid läbi Foiniikia ning Samaaria ja jutustasid paganate pöördumisest, tehes selle sõnumiga suurt rõõmu kõigile vendadele.
4Walipofika Yerusalemu walikaribishwa na kanisa, mitume na wazee; nao wakawapa taarifa juu ya yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.
4Kui nad Jeruusalemma saabusid, võtsid kogudus, apostlid ja vanemad nad vastu. Ja nemad kuulutasid, mida kõike Jumal oli teinud nende juures.
5Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, "Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata Sheria ya Mose."
5Aga mõned variseride hulgast, kes olid saanud usklikuks, tõusid ja ütlesid: 'Neid peab ümber lõikama ja käskima pidada Moosese Seadust.'
6Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalum wa kuchunguza jambo hilo.
6Apostlid ja vanemad tulid nüüd kokku seda kõike arutama.
7Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama, akasema, "Ndugu zangu, ninyi mnafahamu kwamba hapo awali Mungu alipenda kunichagua mimi miongoni mwenu niihubiri Habari Njema, ili watu wa mataifa wapate kusikia na kuamini.
7Kui siis sündis palju vaidlemist, tõusis Peetrus ja ütles neile: 'Mehed-vennad, te teate, et Jumal juba ammusest ajast on valinud teie seast minu, et minu suu läbi paganad kuuleksid evangeeliumi sõna ja saaksid usklikuks.
8Naye Mungu anayejua mioyo ya watu, alithibitisha kwamba amewakubali kwa kuwapa nao Roho Mtakatifu kama alivyotupa sisi.
8Ja südametundja Jumal on nende eest tunnistanud, andes neile Püha Vaimu nagu meilegi,
9Hakufanya ubaguzi wowote kati yetu na wao; aliitakasa mioyo yao kwa imani.
9ja ei ole teinud mingit vahet meie ja nende vahel, olles usu läbi puhastanud nende südamed.
10Sasa basi, kwa nini kumjaribu Mungu kwa kuwatwika hao waumini mzigo ambao wala babu zetu, wala sisi hatukuweza kuubeba?
10Miks te siis nüüd kiusate Jumalat, soovides panna jüngrite kaela iket, mida ei ole jaksanud kanda ei meie isad ega meie?
11Isiwe hivyo, ila tunaamini kwamba, sisi kama vile wao, tunaokolewa kwa njia ya neema ya Bwana Yesu."
11Ent meie usume end päästetud olevat Issanda Jeesuse armu läbi samal kombel nagu nemadki.'
12Kikundi chote kilikaa kimya, kikawasikiliza Barnaba na Paulo wakieleza miujiza na maajabu ambayo Mungu alitenda kwa mikono yao kati ya watu wa mataifa mengine.
12Siis jäi kogu hulk vait ja kuulas, kuidas Barnabas ja Paulus jutustasid, kui palju tunnustähti ja imetegusid Jumal oli teinud paganate seas nende kaudu.
13Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: "Ndugu zangu, nisikilizeni!
13Pärast, kui nad olid lõpetanud, hakkas Jaakobus kõnelema: 'Mehed-vennad, kuulge mind!
14Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.
14Siimeon on rääkinud, kuidas Jumal algusest peale on pidanud hoolt, et koguda paganate seast endale rahvast.
15Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
15Sellega sobivad kokku prohvetite sõnad, nagu on kirjutatud:
16Baada ya mambo haya nitarudi. Nitaijenga tena ile nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitayatengeneza magofu yake na kuijenga tena.
16'Pärast seda ma pöördun tagasi ja ehitan üles Taaveti mahalangenud telgi ja ehitan üles selle varemed ja püstitan selle uuesti,
17Hapo watu wengine wote, watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu, watamtafuta Bwana.
17et muudki inimesed otsiksid Issandat ja kõik rahvad, kelle üle on hüütud minu nime. Nii ütleb Issand, kes teeb seda,
18Ndivyo asemavyo Bwana, aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale.
18mis on teada igavikust alates.'
19"Kwa hiyo, uamuzi wangu ni huu: tusiwataabishe watu wa mataifa wanomgeukia Mungu.
19Seepärast otsustan mina, et neile, kes paganate seast pöörduvad Jumala poole, ei valmistataks raskusi,
20Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa najisi kwa kutambikiwa sanamu za miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.
20vaid neile tuleb kirja teel teatada, et nad hoiduksid ebajumalate rüvedusest ja pilastusest ning lämbunud loomadest ja verest.
21Kwa maana kwa muda mrefu maneno ya Mose yamekuwa yakihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masunagogi yote kila siku ya Sabato."
21Sest Moosesel on ammusest ajast kõigis linnades küllalt kuulutajaid ja teda loetakse sünagoogides igal hingamispäeval.'
22Mitume, wazee na kanisa lote waliamua kuwachagua watu fulani miongoni mwao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Basi, wakamchagua Yuda aitwaye pia Barsaba, na Sila ambao wote walikuwa wanajulikana zaidi kati ya ndugu.
22Siis apostlid ja vanemad koos terve kogudusega arvasid heaks valida endi seast mehi ja saata need Antiookiasse koos Pauluse ja Barnabasega, nimelt Juuda, hüüdnimega Barsabas, ja Siilase, kes mõlemad olid juhid vendade hulgas.
23Wakawapa barua hii: "Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, tunawasalimuni ninyi ndugu wa mataifa mengine mlioko huko Antiokia, Siria na Kilikia.
23Nendega nad saatsid järgmise kirja: 'Apostlid ja vanemad, teie vennad, tervitavad vendi paganate seast, kes elavad Antiookias ja Süüria- ja Kiliikiamaal!
24Tumesikia kwamba watu wengine kutoka huku kwetu waliwavurugeni kwa maneno yao, wakaitia mioyo yenu katika wasiwasi. Lakini wamefanya hivyo bila ya idhini yoyote kutoka kwetu.
24Et me oleme kuulnud, et mõned, kes meie seast on välja läinud, kuigi meie neid ei ole volitanud, on oma kõnedega teid rahutuks teinud ja teie hinged kitsikusse viinud,
25Hivyo, tumeamua kwa pamoja kuwachagua watu kadhaa na kuwatuma kwenu pamoja na wapenzi wetu Barnaba na Paulo,
25siis oleme meie üksmeelselt arvanud heaks valida mehi ja saata need teie juurde koos meie armsate Barnabase ja Paulusega,
26ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
26meestega, kes on pannud oma elu kaalule meie Issanda Jeesuse Kristuse nime pärast.
27Kwa hiyo, tunawatuma Yuda na Sila kwenu; hawa watawaambieni wao wenyewe haya tuliyoandika.
27Nii me siis läkitasime Juuda ja Siilase, et need teile ka suusõnal teataksid sedasama.
28Basi, Roho Mtakatifu na sisi tumekubali tusiwatwike mzigo zaidi ya mambo haya muhimu:
28Sest Püha Vaim ja meie oleme arvanud heaks, et teie peale ei tohi panna ühtegi muud koormat kui need hädavajalikud -
29Msile vyakula vilivyotambikiwa sanamu; msinywe damu; msile nyama ya mnyama aliyenyongwa; na mjiepushe na uasherati. Mtakuwa mmefanya vema kama mkiepa kufanya mambo hayo. Wasalaam!"
29hoiduda ebajumalate ohvriliha ja vere ja lämbunu söömisest ning pilastusest. Teete hästi, kui te neist hoidute! Jääge terveks!'
30Baada ya kuwaaga, hao wajumbe walielekea Antiokia ambako waliita mkutano wa waumini, wakawapa hiyo barua.
30Nii nad saadeti teele ja nad tulid Antiookiasse, kutsusid kokku rahvahulga ja andsid kirja edasi.
31Walipoisoma hiyo barua, maneno yake yaliwatia moyo, wakafurahi sana.
31Kui nood olid selle läbi lugenud, rõõmustasid nad saadud julgustuse pärast.
32Yuda na Sila, ambao nao walikuwa manabii, walizungumza na hao ndugu kwa muda mrefu wakiwatia moyo na kuwaimarisha.
32Juudas ja Siilas, kes ka ise olid prohvetid, julgustasid vendi mitmete sõnadega ja kinnitasid neid.
33Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu wa Antiokia waliwaaga wakiwatakia amani, kisha wakarudi kwa wale waliokuwa wamewatuma.
33Aga kui nad seal mõnda aega olid viibinud, lasksid vennad nad rahuga minema nende juurde, kes neid olid läkitanud.
34Lakini Sila aliamua kubaki.
34[Siilas arvas aga heaks jääda nende juurde.]
35Paulo na Barnaba walibaki huko Antiokia kwa muda; wakafundisha na kuhubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.
35Paulus ja Barnabas jäid Antiookiasse, õpetades ja kuulutades koos paljude teistega Issanda evangeeliumi sõna.
36Baada ya siku kadhaa, Paulo alimwambia Barnaba, "Turudi tukawatembelee wale ndugu katika kila mji tulikolihubiri neno la Bwana tukajionee jinsi wanavyoendelea."
36Mõne päeva pärast ütles Paulus Barnabasele: 'Läki jälle vaatama vendi kõikides linnades, kus me oleme kuulutanud Issanda sõna, kuidas nende käsi käib.'
37Barnaba alitaka wamchukue pia Yohane aitwaye Marko.
37Barnabas andis nõu võtta kaasa ka Johannes, keda kutsutakse Markuseks.
38Lakini Paulo hakupendelea kumchukua Marko, ambaye awali aliwaacha kule Pamfulia na kukataa kushiriki katika kazi yao.
38Aga Paulus pidas õigeks mitte võtta enesega kaasa teda, kes neist Pamfüülias oli lahkunud ega olnud nendega koos tööle läinud.
39Basi kukatokea ubishi mkali kati yao, na wakaachana. Barnaba akamchukua Marko, wakapanda meli kwenda Kupro.
39Sellest tekkis nii suur tüli, et nad teineteisest lahkusid. Barnabas võttis enesega Markuse ja purjetas Küprosele.
40Naye Paulo akamchagua Sila, na baada ya ndugu wa mahali hapo kumweka chini ya ulinzi wa neema ya Bwana, akaondoka.
40Paulus valis aga Siilase ja läks teele, ning vennad andsid ta Issanda armu hooleks.
41Katika safari hiyo alipitia Siria na Kilikia akiyaimarisha makanisa.
41Ja ta käis läbi Süüria- ja Kiliikiamaa, kinnitades kogudusi.