1Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
1Aga Ikoonionis sündis, et nad tulid juudi sünagoogi ja kõnelesid seal nõnda, et suur hulk juute ja kreeklasi sai usklikuks.
2Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
2Aga sõnakuulmatud juudid õhutasid ja ärritasid paganate hinged vendade vastu vihale.
3Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
3Apostlid viibisid seal kauemat aega, kuulutades avalikult Issandat, kes andis tunnistust oma armusõnale ja laskis sündida nende käte läbi tunnustähti ja imetegusid.
4Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
4Aga linna elanikud jagunesid kaheks: ühed olid juutide, teised apostlite poolt.
5Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
5Kui siis paganad ja juudid koos oma ülematega tahtsid apostleid teotada ja kividega surnuks visata,
6Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
6põgenesid nood sellest teada saades Lükaoonia linnadesse Lüstrasse ja Derbesse ja nende ümbruskonda
7wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
7ning kuulutasid seal evangeeliumi.
8Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
8Ja Lüstras istus maas üks vigaste jalgadega mees, emaihust saadik halvatud, kes polnud veel kunagi kõndinud.
9Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
9Too kuulis Paulust rääkimas. Kui Paulus talle otsa vaadates märkas, et mehel on usku saada päästetud,
10akasema kwa sauti kubwa, "Simama wima kwa miguu yako!" Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
10hüüdis ta valju häälega: 'Tõuse püsti! Seisa oma jalgadel!' Ja too hüppas püsti ja kõndis.
11Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: "Miungu imetujia katika sura za binadamu!"
11Rahvahulgad aga, nähes, mis Paulus oli teinud, tõstsid häält ja ütlesid lükaoonia keeles: 'Jumalad on inimeste sarnastena tulnud alla meie juurde.'
12Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
12Nad hüüdsid Barnabast Zeusiks ja Paulust Hermeseks, sest tema pidas kõnet.
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
13Ja linna ääres asuva Zeusi templi preester tõi härgi ja lillevanikuid värava ette ja tahtis koos rahvaga neile ohverdada.
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
14Aga kui apostlid Barnabas ja Paulus seda kuulsid, käristasid nad oma rõivad katki ja tormasid rahvahulga sekka, hüüdes:
15"Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
15'Mehed, miks te seda teete! Meiegi oleme teiesugused nõdrad inimesed, ja me kuulutame teile evangeeliumi, et te pöörduksite tühjadest asjadest elava Jumala poole, kes on teinud taeva ja maa ja mere ning kõik, mis nende sees on,
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
16kes läinud sugupõlvede ajal on lubanud kõigil paganail käia nende oma teedel,
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha."
17ja ometi ei ole jätnud andmata endast tunnistust, tehes head: andnud taevast teile vihma ja viljakaid aegu, kosutanud teid toiduga ja teie südant rõõmuga.'
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
18Ja nii kõneldes suutsid nad vaevu vaigistada rahvahulka, et see neile ei ohverdaks.
19Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
19Aga Antiookiast ja Ikoonionist tuli sinna juute ja need said rahvahulga oma nõusse. Ja nad viskasid Paulust kividega ning lohistasid ta linnast välja, pidades teda surnuks.
20Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
20Aga kui jüngrid olid kogunenud tema ümber, tõusis Paulus püsti ja läks linna. Järgmisel päeval lahkus ta koos Barnabasega Derbesse.
21Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
21Kui nad ka sellele linnale olid evangeeliumi kuulutanud ja paljud olid jüngriteks saanud, pöördusid nad tagasi Lüstrasse ja Ikoonioni ja Antiookiasse
22Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, "Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu."
22ning kinnitasid jüngrite hingi, julgustades neid jääma ususse ja seletades, et meil tuleb paljude viletsuste kaudu sisse minna Jumala riiki.
23Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
23Kui nad siis igale kogudusele siin ja seal olid käte pealepanemisega vanemad seadnud, jätsid nad pärast palvetamist ja paastumisi nemad Issanda hooleks, kellesse need olid hakanud uskuma.
24Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
24Ja läbinud Pisiidiamaa, saabusid nad Pamfüüliasse.
25Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
25Ja kui nad Perges olid sõna kuulutanud, läksid nad edasi Ataaliasse.
26Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
26Sealt nad purjetasid Antiookiasse, kus nad olid antud Jumala armu hooleks selle töö tarvis, mille nad nüüd olid lõpetanud.
27Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
27Pärale jõudnud ja koguduse kokku kutsunud, kuulutasid nad, mida kõike Jumal oli teinud nende juures ja et ta oli paganatele avanud usu ukse.
28Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.
28Ja nad viibisid seal jüngrite keskel kauemat aega.