1Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
1Aga Antiookias olevas koguduses oli prohveteid ja õpetajaid: Barnabas, Siimeon, keda hüüti Nigeriks, Luukius Küreenest, Manaeen, kes oli kasvanud üles koos nelivürst Heroodesega, ja Saulus.
2Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: "Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia."
2Kui need siis Issandat teenisid ja paastusid, ütles Püha Vaim: 'Eraldage mulle Barnabas ja Saulus tööle, milleks ma olen nad kutsunud!'
3Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
3Siis nad paastusid ja palvetasid, panid oma käed nende peale ning saatsid nad teele.
4Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
4Kui nad olid Püha Vaimu poolt teele saadetud, tulid nad alla Seleukeiasse ja purjetasid Küprosele.
5Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
5Ja kui nad jõudsid Salamisesse, kuulutasid nad Jumala sõna juudi sünagoogides. Neil oli ka Johannes abiliseks.
6Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
6Nad käisid läbi terve saare Pafosest saadik. Seal leidsid nad ühe juudi nõia ning valeprohveti nimega Barjeesus.
7Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
7See oli maavalitseja Sergius Pauluse juures, kes oli mõistlik mees. Too kutsus Barnabase ja Sauluse enese juurde ning soovis kuulata Jumala sõna.
8Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
8Aga neile pani vastu Elümas, 'nõid' - sest nõnda tuleb tõlkida ta nime -, püüdes maavalitsejat usust eemale pöörata.
9Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
9Aga Saulus, keda hüütakse Pauluseks, täis Püha Vaimu, vaatas teda teravalt
10akasema, "Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
10ja ütles: 'Oh sa kuradi poeg, täis kõiksugu kavalust ja kõiksugu kelmust, kõige õiguse vaenlane, kas sa ei lakka Issanda sirgeid teid väänamast?
11Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo." Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
11Ja nüüd, vaata, Issanda käsi tuleb su peale ja sa jääd pimedaks ega näe päikest tükil ajal!' Ja otsekohe langes Elümase üle pimedus ning ringi tammudes otsis ta talutajaid.
12Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
12Kui maavalitseja nägi, mis juhtus, hakkas ta uskuma, olles hämmastunud Issanda õpetusest.
13Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
13Aga Paulus ja tema kaaslased purjetasid edasi Pafosest ja tulid Pergesse, Pamfüüliamaale. Seal Johannes lahkus neist ja pöördus tagasi Jeruusalemma.
14Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
14Aga nemad läksid Pergest edasi ja jõudsid Pisiidia-poolsesse Antiookiasse. Hingamispäeval läksid nad sünagoogi ja istusid maha.
15Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: "Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni."
15Pärast Seaduse ja Prohvetite ettelugemist läkitasid sünagoogi vanemad neile sõna: 'Mehed-vennad, kui teil on mõni julgustussõna rahva jaoks, siis öelge!'
16Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: "Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
16Siis tõusis Paulus üles, viipas käega ja ütles:'Iisraeli mehed ja teie, kes kardate Jumalat, kuulge!
17Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
17Iisraeli rahva Jumal valis ära meie isad ja tegi nendest suure rahva, kui nad olid pagulastena Egiptuses, ja ta tõi nad sealt välja kõrgele tõstetud vägeva käega.
18Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
18Ja ligi nelikümmend aastat talus ta nende kombeid kõrbes;
19Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
19ja ta hävitas seitse rahvast Kaananimaal ja andis nende maa neile pärandiks
20Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
20ligi neljasaja viiekümneks aastaks. Ja pärast seda andis ta neile kohtumõistjaid prohvet Saamueli ajani.
21Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
21Ja seejärel nad palusid endale kuningat, ja Jumal andis neile neljakümneks aastaks Sauli, Kiisi poja, mehe Benjamini suguharust.
22Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
22Ja kui ta selle oli tagandanud, äratas ta neile kuningaks Taaveti, kellest ta ka tunnistas: 'Ma olen leidnud Taaveti, Iisai poja, endale meelepärase mehe, kes teeb kõik mu tahtmist mööda.'
23Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
23Sellesama mehe soost on Jumal oma tõotust mööda toonud Jeesuse Iisraelile Päästjaks.
24Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
24Enne tema tulekut kuulutas Johannes meeleparandusristimist kogu Iisraeli rahvale.
25Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
25Kui Johannes oli oma elukäiku lõpetamas, ütles ta: 'Mina ei ole see, kelle te arvate minu olevat, kuid vaata, pärast mind tuleb see, kelle jalatsit jalast päästma mina ei ole väärt.'
26"Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
26Mehed-vennad, Aabrahami soo lapsed, ja need teie seas, kes Jumalat kardavad: meile on läkitatud see päästesõna.
27Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
27Sest Jeruusalemma elanikud ja nende ülemad ei tundnud teda ära, ja saatsid nõnda oma kohtuotsusega täide prohvetite ütlused, mida igal hingamispäeval loetakse,
28Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
28ja ühtegi surmasüüd leidmata palusid nad Pilaatust, et ta hukataks.
29Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
29Ja kui nad olid täitnud kõik, mis temast oli kirjutatud, võeti ta ristipuult maha ja pandi hauda.
30Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
30Jumal aga äratas ta surnuist üles.
31Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
31Ta oli palju päevi nähtav neile, kes koos temaga olid tulnud Galileast üles Jeruusalemma. Needsamad on nüüd tema tunnistajad rahva ees.
32Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
32Ja meie kuulutame teile rõõmusõnumit isadele antud tõotusest,
33Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
33et Jumal Jeesust üles äratades on täielikult täitnud tõotuse nende lastele, meile - nagu ka teises laulus on kirjutatud: 'Sina oled mu Poeg, täna ma olen su sünnitanud.'
34Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
34Et ta on tema surnuist üles tõusta lasknud, nõnda et ta eales ei pöördu tagasi kõdunemisse, seda on ta öelnud nii: 'Ma täidan teile need Taavetile antud pühad ja kindlad tõotused.'
35Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
35Seepärast ütleb ta ka teisal: 'Sina ei lase oma Pühal näha kõdunemist.'
36Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
36Sest Taavet, kui ta oma sugupõlve ajal Jumala tahtmist oli teeninud, uinus magama ja maeti oma esivanemate juurde ning nägi kõdunemist,
37Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
37see aga, kelle Jumal on üles äratanud, ei näinud kõdunemist.
38Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
38Olgu siis teile teada, mehed-vennad, et tema kaudu kuulutatakse teile pattude andeksandmist, ja see õigeksmõist, mida te ei suutnud leida Moosese Seaduses,
39na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
39on temas, kelles see on täielikult võimalik igale inimesele, kes usub.
40Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
40Vaadake siis, et teile ei juhtuks, mis on öeldud prohvetite kirjades:
41Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni."
41'Vaadake, te põlastajad, ja imestage ja hävige. Sest ma teen ühe teo teie päevil, teo, mida te ei usuks, kui keegi seda teile jutustaks.''
42Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
42Kui nad siis välja läksid, paluti apostleid ka järgmisel hingamispäeval neid asju rääkima.
43Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
43Pärast sünagoogist äraminekut järgnesid paljud juudid ja jumalakartlikud proselüüdid Paulusele ja Barnabasele, kes vestlesid nendega ja veensid neid jääma Jumala armusse.
44Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
44Aga järgmisel hingamispäeval kogunes peaaegu kogu linn Issanda sõna kuulama.
45Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
45Rahvahulki nähes muutusid juudid väga kadedaks ja vaidlesid pilgates vastu Pauluse sõnadele.
46Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, "Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine.
46Paulus ja Barnabas aga ütlesid avalikult: 'Meie kohus oli rääkida Jumala sõna esiteks teile, aga et teie selle enesest ära tõukasite ega arva end igavest elu väärivat, siis vaata, me pöördume paganate poole.
47Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote."
47Sest nõnda on meid Issand käskinud: 'Ma olen su pannud paganate valguseks, et sa oleksid päästeks ilmamaa otsani.''
48Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini.
48Seda kuuldes rõõmustasid paganad ja ülistasid Issanda sõna ning said usklikuks, nii palju kui neid oli määratud igaveseks eluks.
49Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
49Ja Issanda sõna levis üle kogu maakonna.
50Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
50Aga juudid ässitasid kõrgemast seisusest jumalakartlikke naisi ja linna ülikuid, õhutades neid taga kiusama Paulust ja Barnabast, ning kihutasid nad välja oma piirkonnast.
51Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
51Nemad aga raputasid tolmu oma jalgadelt nende peale ja tulid Ikoonioni.
52Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.
52Ja jüngrid said täis rõõmu ja Püha Vaimu.