1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
1Aga sel ajal hakkas kuningas Heroodes mõnele kogudusest kurja tegema.
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
2Ta tappis mõõgaga Jaakobuse, Johannese venna.
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
3Aga nähes, et see juutidele meeldis, võttis ta kinni ka Peetruse. See oli just hapnemata leibade pühal.
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
4Heroodes vahistas Peetruse ja pani ta vanglasse ning andis nelja neljamehelise sõdurite salga valvata, kavatsedes ta pärast paasapühi rahva ette tuua.
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
5Nii peeti siis Peetrust vangis, aga kogudus palvetas lakkamatult Jumala poole tema pärast.
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
6Ööl enne seda, kui Heroodes tahtis Peetruse enese ette tuua, magas Peetrus kahe sõduri vahel kahe ketiga aheldatult, ja vahimehed ukse ees valvasid vanglat.
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
7Ja ennäe, Issanda ingel seisis seal ning valgus helkis vangikongis. Ingel lõi Peetrust vastu külge, äratas ta üles ja ütles: 'Tõuse kiiresti!' Ja Peetruse ahelad langesid käte ümbert maha.
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
8Ingel aga ütles talle: 'Pane vöö vööle ja seo oma jalatsid jalga!' Tema tegigi nõnda. Ja ingel ütles talle: 'Pane oma kuub selga ja tule minu järele.'
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
9Ja Peetrus tuli välja ja käis tema järel ega teadnud, et see, mis ingel tegi, on tõsi, vaid arvas end nägevat nägemust.
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
10Ja nad läbisid esimese ja teise vahiposti ning tulid linna viiva raudvärava ette. See avanes neile iseenesest ja nad väljusid ja läksid edasi üht tänavat pidi. Ja järsku lahkus ingel tema juurest.
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
11Ja kui Peetrus jälle hakkas aru saama, lausus ta: 'Nüüd ma tean, et Issand on tõesti oma ingli läkitanud ja mu välja kiskunud Heroodese käest ning kõigest, mida juuda rahvas ootab.'
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
12Ja märgates, kus ta on, tuli ta selle Maarja koja juurde, kes on Markuseks hüütava Johannese ema. Sinna oli suur hulk rahvast kokku tulnud palvetama.
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
13Kui ta siis hooviväravale koputas, tuli sinna kuulatama tüdruk, Roode nimi.
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
14Kui ta Peetruse hääle järgi ära tundis, siis rõõmu tõttu ei avanud ta väravat, vaid jooksis sisse ja teatas, et Peetrus seisab värava taga.
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
15Nemad ütlesid talle: 'Sa jampsid!' Tema aga kinnitas, et see on nõnda. Siis nad ütlesid: 'See on tema ingel.'
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
16Peetrus koputas üha edasi. Kui nad nüüd avasid, nägid nad teda ja jahmusid.
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
17Peetrus aga viipas neile käega, et nad vait jääksid, ning jutustas, kuidas Issand oli ta vanglast välja toonud, ning ütles: 'Teatage seda Jaakobusele ja vendadele!' Ja ta väljus ning läks sealt ära teise paika.
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
18Aga päeva saabudes olid sõdurid suures ärevuses selle pärast, mis Peetrusega oli juhtunud.
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
19Kui Heroodes teda otsis ega leidnud, kuulas ta vangivalvurid üle ja käskis need viia hukkamisele. Ise ta läks Juudamaalt alla Kaisareasse ja jäi sinna.
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
20Ent Heroodes kandis viha Tüürose ja Siidoni rahva peale. Nood tulid ühel meelel tema juurde ja, saanud nõusse kuninga kambriülema Blastose, palusid rahu; sest nende maa sai oma toiduse kuninga alalt.
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
21Määratud päeval pani Heroodes selga kuninglikud rõivad, istus kohtujärjele ja pidas neile kõne.
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
22Rahvas aga hüüdis: 'See ei ole inimese, vaid Jumala hääl!'
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
23Aga otsekohe lõi teda Issanda ingel, seepärast et ta ei andnud au Jumalale. Ja ussidest sööduna heitis Heroodes hinge.
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
24Aga Jumala sõna kasvas ja levis.
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.
25Ent Barnabas ja Saulus, olles lõpetanud oma teenistuse Jeruusalemmas, tulid tagasi ja võtsid enestega kaasa Johannese, keda hüüti Markuseks.