1Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
1Aga apostlid ja vennad, kes elasid mööda Juudamaad laiali, said kuulda, et ka paganad olid Jumala sõna vastu võtnud.
2Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
2Kui nüüd Peetrus tuli üles Jeruusalemma, riidlesid ümberlõigatud temaga:
3"Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
3'Sina oled astunud sisse ümberlõikamata meeste juurde ja söönud koos nendega!'
4Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
4Siis Peetrus hakkas rääkima ja seletas neile järgemööda kõik:
5"Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
5'Mina olin Joppe linnas palvetamas ja nägin nagu endast ära olles nägemuse: üks anum, mida lasti nelja nurka pidi taevast maa peale, laskus nagu suur lina ja tuli otse minu ette.
6Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
6Ja kui ma seda ainiti vaatasin, nägin ma ilmamaa neljajalgseid ja metsloomi ja roomajaid ja taeva linde.
7Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
7Aga ma kuulsin ka häält mulle ütlevat: 'Tõuse, Peetrus, tapa ja söö!'
8Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
8Aga mina ütlesin: 'Ei ilmaski, Issand, sest minu suust ei ole veel kunagi sisse läinud midagi keelatut ega rüvedat!'
9Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
9Hääl taevast ütles aga teist korda: 'Mida Jumal on puhtaks tunnistanud, seda sina ära pea keelatuks!'
10Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
10See sündis kolm korda, ja kõik tõmmati jälle üles taevasse.
11Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
11Ja ennäe, otsekohe seisis koja ees, kus me olime, kolm meest, kes olid läkitatud Kaisareast minu juurde.
12Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
12Aga Vaim ütles mulle, et ma läheksin nendega kaasa ilma kõhklemata. Minuga tulid koos ka need kuus venda ja me läksime selle mehe majja.
13Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
13Ja tema jutustas meile, kuidas ta oli näinud inglit oma majas seismas ja ütlemas: 'Läkita mehi Joppesse ja kutsu Siimon, kelle hüüdnimi on Peetrus.
14Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
14Tema räägib sulle sõnu, mille läbi sina ja kogu su pere saate päästetud.'
15Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
15Kui ma siis hakkasin rääkima, langes Püha Vaim nende peale nii nagu meiegi peale alguses.
16Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
16Siis tuli mulle meelde Issanda sõna, kuidas ta ütles: 'Johannes ristis küll veega, aga teid ristitakse Püha Vaimuga.'
17Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?"
17Kui nüüd Jumal on andnud neile samasuguse anni kui meilegi, kes me usume Issandasse Jeesusesse Kristusesse, kes olen siis mina, et ma oleksin võinud Jumalat keelata?'
18Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, "Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!"
18Seda kuuldes nad rahunesid ja andsid Jumalale au, üteldes: 'Siis on Jumal ka paganatele andnud meeleparanduse eluks.'
19Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
19Need, kes olid Stefanose pärast tekkinud viletsuses hajutatud, käisid mööda maad Foiniikiani ja Küprose saareni ja Antiookiani, rääkides sõna ainuüksi juutidele.
20Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
20Nende hulgas oli ka Küprose ja Küreene mehi, need rääkisid pärast Antiookiasse jõudmist ka kreeklastele, kuulutades neile evangeeliumi Issandast Jeesusest.
21Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
21Issanda käsi oli nendega, ja suur oli nende arv, kes uskuma hakates pöördusid Issanda poole.
22Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
22Aga jutt nendest kostis Jeruusalemmas oleva koguduse kõrvu ja nad läkitasid Barnabase Antiookiasse.
23Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
23Kui ta pärale jõudis ja nägi Jumala armu, sai ta rõõmsaks ja julgustas kõiki jääma kindlameelselt Issanda omaks.
24Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
24Sest ta oli hea mees, täis Püha Vaimu ja usku. Ja palju rahvast lisati Issanda omade hulka.
25Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
25Siis läks Barnabas Tarsosesse Saulust otsima,
26Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
26ja kui ta leidis tema, tõi ta tema Antiookiasse. Ning nad käisid terve aasta koos koguduses ja õpetasid suurt hulka rahvast. Ja see oli Antiookias, kus jüngreid esimest korda hakati nimetama kristlasteks.
27Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
27Noil päevil tuli prohveteid Jeruusalemmast Antiookiasse.
28Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
28Üks neist, Agabos nimi, tõusis ja andis Vaimu läbi teada, et suur nälg on tulemas kogu riigis. Nõnda ka sündis keiser Klaudiuse ajal.
29Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
29Aga iga jünger otsustas saata Juudamaal elavatele vendadele abi, nii kuidas kellegi käekäik lubas.
30Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.
30Seda nad tegidki, läkitades annid Barnabase ja Sauluse kaudu vanematele.