1Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
1Aga kui see sündis, et meie neist lahkusime ja merele läksime, siis tulime otseteed sõites Koosi saarele, teisel päeval aga Roodosele ja sealt Patarasse.
2Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
2Seal me leidsime laeva, mis suundus Foiniikiasse, astusime sellele ja sõitsime minema.
3Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
3Aga kui Küpros paistma hakkas, jätsime selle pahemat kätt, purjetasime Süüriasse ja randusime Tüüroses, sest seal pidi laev lossitama.
4Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
4Seal me leidsime jüngreid ja jäime nende juurde seitsmeks päevaks. Nemad ütlesid Paulusele Vaimu mõjul, et ta ei läheks Jeruusalemma.
5Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
5Kui me need päevad seal olime mööda saatnud, asusime teele; ja nemad kõik naiste ja lastega saatsid meid linnast välja. Ja ranna ääres me laskusime põlvili ning, olles palvetanud,
6Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
6andsime üksteisele jumalagajätuks suud. Ja meie astusime laevale, nemad aga pöördusid tagasi koju.
7Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
7Meie jätkasime aga purjetamist ning saabusime Tüürosest Ptolemaisi, teretasime vendi ning jäime üheks päevaks nende juurde.
8Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
8Järgmisel päeval me lahkusime sealt, jõudsime Kaisareasse ja astusime sisse evangelist Filippuse kotta, kes oli üks neist seitsmest, ja jäime tema juurde.
9Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
9Temal oli neli tütart, kes olid neitsid ja kõnelesid prohvetlikult.
10Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
10Kui me mõneks päevaks sinna jäime, tuli Juudamaalt prohvet, Agabos nimi.
11Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema "Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa."
11Ja ta tuli meie juurde, võttis Pauluse vöö, sidus oma käed ja jalad kinni ning ütles: 'Nii ütleb Püha Vaim: Mehe, kelle oma on see vöö, aheldavad juudid nõnda Jeruusalemmas ja annavad paganate kätte.'
12Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
12Seda kuuldes palusime meie ja ka sealsed vennad Paulust, et ta ei läheks Jeruusalemma.
13Lakini yeye alijibu, "Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu."
13Seepeale vastas Paulus: 'Mis te teete, et te nutate ja vaevate mu südant! Sest ma olen valmis mitte üksnes laskma ennast Jeruusalemmas aheldada, vaid ka surema Issanda Jeesuse nime pärast.'
14Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: "Mapenzi ya Bwana yafanyike"
14Aga kui ta ei lasknud end ümber veenda, rahunesime ja ütlesime: 'Sündigu Issanda tahtmine!'
15Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
15Pärast neid päevi me valmistusime teeleminekuks ja läksime Jeruusalemma.
16Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
16Meiega tulid ka mõned jüngrid Kaisareast, kes viisid meid ühe ammuse jüngri Mnaasoni, Küprose mehe juurde, kelle külalisteks me pidime jääma.
17Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
17Kui me Jeruusalemma jõudsime, võtsid vennad meid vastu rõõmsa meelega.
18Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
18Järgmisel päeval läks Paulus meiega Jaakobuse juurde ja kõik vanemad tulid ka sinna.
19Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
19Ta tervitas neid ja kirjeldas siis üksikasjalikult kõike, mis Jumal tema teenimise läbi oli paganate seas teinud.
20Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, "Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
20Seda kuuldes ülistasid nad Jumalat ning ütlesid Paulusele: 'Vend, sa näed, kui mitukümmend tuhat juuti on saanud usklikuks ja need kõik on innukad Moosese Seaduse pidajad.
21Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
21Nende kõrvu on kostnud, et sina õpetavat paganate seas elavaid juute Moosesest ära taganema, öeldes, et neil ei ole vaja lapsi ümber lõigata ega elada meie tavade järgi.
22Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
22Mida nüüd teha? Muidugi nad saavad kuulda, et sa oled tulnud.
23Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
23Tee nüüd seda, mis me sulle ütleme! Meil on neli meest, kelle peal on tõotus.
24Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
24Võta need enesega ja puhasta ennast koos nendega ja kanna nende eest nende kulud, et nad oma pea võiksid pügada, ja siis saavad kõik aru, et see on tühi jutt, mis nad sinust on kuulnud, ning et ka sina ise elad Seadust pidades.
25Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati."
25Aga usklikuks saanud paganate kohta me oleme saatnud kirja, otsustades, et nad peavad hoiduma ebajumalate ohvriliha ja vere ja lämbunu söömisest ning pilastusest.'
26Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
26Järgmisel päeval võttis Paulus mehed ja laskis enda koos nendega puhastada. Siis ta läks pühakotta, et teatada, millal puhastuspäevad lõpevad ja nende igaühe eest tuuakse ohver.
27Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
27Aga kui need seitse päeva hakkasid lõpule jõudma, nägid Aasiast tulnud juudid Paulust pühakojas. Need ajasid möllama kogu rahva ja pistsid oma käed tema külge,
28wakipiga kelele: "Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu."
28hüüdes: 'Iisraeli mehed, tulge appi! See ongi see inimene, kes kõigis paigus õpetab meie rahva ja Seaduse ja selle paiga vastu. Ja nüüd on ta veel kreeklasigi toonud pühakotta ja selle püha paiga rüvetanud!'
29Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
29Sest nad olid enne linnas näinud temaga koos efeslast Trofimost ning arvasid, et Paulus oli ta toonud pühakotta.
30Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
30Siis tõusis kogu linn liikvele ning rahvas jooksis kokku. Ja nad haarasid Paulusest kinni ja vedasid ta pühakojast välja, ja otsekohe lukustati uksed.
31Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
31Ja kui nad püüdsid teda tappa, läks sõnum sealse väeosa ülempealikule, et kogu Jeruusalemm on möllamas.
32Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
32See võttis otsekohe sõdureid ja pealikuid kaasa ja tuli jooksujalu nende juurde. Kui rahvas nägi ülempealikut ja sõdureid, lõpetasid nad Pauluse peksmise.
33Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, "Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?"
33Siis ülempealik astus ligi, võttis Pauluse oma hoole alla, käskis ta kahe ketiga aheldada ning küsis, kes ta on ja mis ta on teinud.
34Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
34Aga rahvahulgast karjusid ühed ühte, teised teist. Kuna ülempealik ei suutnud lärmi pärast midagi selgemalt teada saada, siis laskis ta Pauluse viia kindlusse.
35Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
35Aga kui ta treppide juurde jõudis, tuli sõduritel rahva vägivallatsemise pärast Paulust kanda,
36Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, "Muulie mbali!"
36sest suur rahvahulk järgnes neile, hüüdes: 'Hukka ta ära!'
37Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, "Naweza kukwambia kitu?" Yule mkuu wa jeshi akamjibu, "Je unajua Kigiriki?
37Kui Paulust oldi juba kindlusse viimas, lausus ta ülempealikule: 'Kas ma tohin sulle midagi öelda?' Aga tema ütles: 'Kas sa oskad kreeka keelt?
38Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?"
38Kas sa ei olegi see egiptlane, kes mõni aeg tagasi ässitas ja viis kõrbe neli tuhat sikariooti?'
39Paulo akajibu, "Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
39Paulus ütles: 'Mina olen juut Tarsosest, kuulsa Kiliikia linna kodanik. Ma palun sind väga, luba mul rahvale kõnelda!'
40Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.
40Kui ta lubas, astus Paulus trepiastmeile ning viipas rahvale käega. Kui kõik jäid vait, hakkas ta heebrea keeles kõnet pidama ja ütles: