1"Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni sasa nikijitetea mbele yenu!"
1'Mehed, vennad ja isad, kuulake nüüd, mida ma teile enese kaitseks räägin!'
2Waliposikia akiongea nao kwa Kiebrania wakazidi kukaa kimya zaidi kuliko hapo awali. Naye Paulo akaendelea kusema,
2Kui nad kuulsid, et ta peab neile kõnet heebrea keeles, jäid nad veel rahulikumaks. Ja Paulus ütles:
3"Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia. Lakini nililelewa papa hapa mjini Yerusalemu chini ya mkufunzi Gamalieli. Nilifundishwa kufuata kwa uthabiti Sheria ya wazee wetu. Nilijitolea kwa moyo wote kwa Mungu kama ninyi wenyewe mlivyo hivi leo.
3'Mina olen Juuda mees, sündinud Tarsoses Kiliikiamaal ja üles kasvatatud siinsamas linnas, Gamalieli jalgade ees, õpetatud täpselt esiisade Seadust mööda, olles innukas Jumala nõudja, nii nagu teie kõik tänapäeval olete.
4Niliwatesa hata kuwaua wale watu waliofuata Njia hii. Niliwatia nguvuni wanaume kwa wanawake na kuwafunga gerezani.
4Sellisena ma kiusasin surmani taga usuteed, pannes ahelaisse ja toimetades vanglasse nii mehi kui naisi.
5Kuhani Mkuu na baraza lote la wazee wanaweza kushuhudia jambo hilo. Kutoka kwao nilipokea barua walioandikiwa wale ndugu Wayahudi waliokuwa huko Damasko. Nilikwenda Damasko ili niwatie nguvuni watu hao na kuwaleta wamefungwa mpaka Yerusalemu ili waadhibiwe.
5Nõnda võivad mu kohta tunnistada ka ülempreester ja vanemad, kelle käest ma sain kirju viimiseks nende vendade kätte Damaskusesse. Ja ma kavatsesin ka sealseid usklikke tuua aheldatult Jeruusalemma, et neid karistataks.
6"Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana, mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote.
6Aga sündis, kui ma olin teel ja lähenesin Damaskusele, et lõuna ajal välgatas äkitselt mu ümber ere valgus taevast.
7Hapo nilianguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?
7Ma kukkusin maha ja kuulsin üht häält mulle ütlevat: 'Saul, Saul, miks sa mind taga kiusad?'
8Nami nikauliza: Nani wewe, Bwana? Naye akaniambia: Mimi ni Yesu wa Nazareti ambaye wewe unamtesa.
8Mina aga vastasin: 'Kes sa oled, isand?' Tema ütles mulle: 'Mina olen Jeesus Naatsaretlane, keda sina taga kiusad!'
9Wale wenzangu waliuona ule mwanga lakini hawakusikia sauti ya yule aliyeongea nami.
9Minu kaaslased nägid küll valgust, aga nad ei kuulnud tema häält, kes minuga rääkis.
10Basi, mimi nikauliza: Nifanye nini Bwana? Naye Bwana akaniambia: Simama, nenda Damasko na huko utaambiwa yote ambayo umepangiwa kufanya.
10Siis ma ütlesin: 'Mis ma pean tegema, Issand?' Issand aga ütles mulle: 'Tõuse püsti, mine Damaskusesse, seal öeldakse sulle kõik, mis sul on määratud teha.'
11Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko.
11Aga kuna ma selle valguse kirkuse tõttu ei näinud, talutasid mu kaaslased mind kättpidi, ja ma jõudsin Damaskusesse.
12"Huko kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Anania, mtu mcha Mungu, mwenye kuitii Sheria yetu na aliyeheshimika sana mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaishi Damasko.
12Aga keegi Hananias, Seaduse järgi vaga mees, kel oli hea tunnistus kõigi sealsete juutide poolt,
13Yeye alikuja kuniona, akasimama karibu nami, akasema: Ndugu Saulo! Ona tena. Papo hapo nikaona tena, nikamwangalia.
13tuli minu juurde. Ta seisatas mu kõrval ja ütles: 'Vend Saul, näe jälle!' Ja selsamal hetkel ma nägin jälle ja vaatasin talle otsa.
14Halafu Anania akasema: Mungu wa babu zetu amekuchagua upate kujua matakwa yake na kumwona yule mtumishi wake mwadilifu na kumsikia yeye mwenyewe akiongea.
14Tema aga ütles: 'Meie isade Jumal on su määranud tunnetama tema tahtmist ja nägema seda Õiget ning kuulma häält tema suust,
15Kwa maana utamshuhudia kwa watu wote ukiwaambia yale uliyoyaona na kuyasikia.
15sest sina saad tema tunnistajaks kõigile inimestele selles, mida sa oled näinud ja kuulnud.
16Sasa basi, ya nini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewe dhambi zako kwa kuliungama jina lake.
16Ja mida sa nüüd ootad? Tõuse ja lase ennast ristida ning oma patud ära pesta, appi hüüdes tema nime!'
17"Basi, nilirudi Yerusalemu, na nilipokuwa nikisali Hekaluni, niliona maono.
17Aga sündis, et kui ma tagasi pöördusin Jeruusalemma ja pühakojas palvetasin, olin ma nagu endast ära
18Nilimwona Bwana akiniambia: Haraka! Ondoka Yerusalemu upesi kwa maana watu wa hapa binadamu hawataukubali ushuhuda wako juu yangu.
18ja nägin teda mulle ütlevat: 'Tõtta ja mine kiiresti Jeruusalemmast ära, sest nad ei võta vastu sinu tunnistust minu kohta.'
19Nami nikamjibu: Bwana, wao wanajua wazi kwamba mimi ni yule aliyekuwa anapitapita katika masunagogi na kuwatia nguvuni na kuwapiga wale waliokuwa wanakuamini.
19Ja mina ütlesin: 'Issand, nad ise ju teavad, et ma viisin vangi ja peksin sünagoogides neid, kes sinusse usuvad.
20Na kwamba wakati shahidi wako Stefano alipouawa, mimi binafsi nilikuwako pale nikakubaliana na kitendo hicho na kuyalinda makoti ya wale waliokuwa wanamuua.
20Ja kui sinu tunnistaja Stefanose verd valati, seisin minagi seal juures ja kiitsin selle heaks ning valvasin nende rõivaid, kes ta hukkasid.'
21Naye Bwana akaniambia: Nenda; ninakutuma mbali kwa mataifa mengine."
21Ja tema ütles mulle: 'Mine, sest ma läkitan su kaugele paganate sekka!''
22Mpaka hapa, wale watu walikuwa wanamsikiza, lakini aliposema maneno haya, walianza kusema kwa sauti kubwa, "Mwondoe duniani! Mtu wa namna hiyo hastahili kuishi."
22Kuni selle sõnani nad kuulasid teda, siis aga tõstsid oma häält: 'Hukka niisugune ära maa pealt! Ta ei tohi ellu jääda!'
23Waliendelea kupayukapayuka huku wakitikisa makoti yao na kurusha vumbi angani.
23Ja kui nad karjusid ja rõivaid seljast kiskusid ning tolmu vastu taevast loopisid,
24Mkuu wa jeshi aliwaamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome, akawaambia wamchape viboko ili wapate kujua kisa cha Wayahudi kumpigia kelele.
24käskis ülempealik Pauluse viia kindlusse ning ütles, et teda tuleb piitsa varal üle kuulata; sest ta tahtis teada, mispärast nad tema peale nõnda karjusid.
25Lakini walipokwisha mfunga ili wamchape viboko, Paulo alimwuliza jemadari mmoja aliyesimama hapo, "Je, ni halali kwenu kumpiga viboko raia wa Roma kabla hajahukumiwa?"
25Aga kui nad olid tema rihmutamiseks kinni sidunud, ütles Paulus pealikule, kes seal juures seisis: 'Kas teie tohite Rooma kodanikku piitsaga peksta ja pealegi ilma kohtuotsuseta?'
26Yule jemadari aliposikia hayo, alimpasha habari mkuu wa jeshi akisema, "Unataka kufanya nini? Mtu huyu ni raia wa Roma!"
26Kui pealik seda kuulis, läks ta ja teatas ülempealikule: 'Vaata ette, mida sa teed! See inimene on ju Rooma kodanik.'
27Basi, mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamwambia, "Niambie; je, wewe ni raia wa Roma?" Paulo akamjibu, "Naam."
27Siis tuli ülempealik Pauluse juurde ning küsis: 'Ütle mulle, kas sa oled Rooma kodanik?' Tema ütles: 'Olen küll.'
28Mkuu wa jeshi akasema, "Mimi nami nimekuwa raia wa Roma kwa kulipa gharama kubwa." Paulo akasema, "Lakini mimi ni raia wa Roma kwa kuzaliwa."
28Ülempealik vastas: 'Mina olen endale Rooma kodakondsuse hankinud suure raha eest.' Paulus aga ütles: 'Ent mina olen sellesse sündinud.'
29Wale watu ambao walikuwa tayari kumchunguza Paulo walitoweka mara. Hata yule mkuu wa jeshi aliogopa alipojua kwamba Paulo ni raia wa Roma na kwamba alikuwa amekwisha mfunga minyororo.
29Siis jätsid ülekuulajad ta kohe rahule. Ülempealik lõi aga kartma, kui ta sai teada, et Paulus on Rooma kodanik ja et ta oli tema ahelaisse pannud.
30Kesho yake, mkuu wa jeshi alitaka kujua mashtaka kamili ambayo Wayahudi walikuwa wamemwekea Paulo. Hivyo, alimfungua Paulo minyororo, akaamuru makuhani wakuu na Baraza lote wafanye kikao. Kisha alimleta Paulo, akamsimamisha mbele ya Baraza.
30Aga teisel päeval, soovides selgemalt teada saada, milles juudid Paulust süüdistavad, päästis ülempealik ta ahelatest valla ja käskis ülempreestreid ja kogu Suurkohtu kokku tulla ning viis Pauluse nende ette.