Swahili: New Testament

Estonian

Acts

27

1Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho "Kikosi cha Augusto."
1Kui oli otsustatud, et me purjetame Itaaliasse, anti Paulus ja mõned teised vangid üle keiserliku väesalga pealikule nimega Julius.
2Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
2Me astusime siis Adramüttioni laevale, mis pidi purjetama Aasia sadamate kaudu, ja läksime merele. Meiega oli ka makedoonlane Aristarhos Tessaloonikast.
3Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
3Ja teisel päeval me randusime Siidonis. Julius kohtles Paulust lahkesti ning andis talle loa minna oma sõprade juurde, et need saaksid tema eest hoolitseda.
4Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
4Ja kui me sealt olime läinud merele, purjetasime Küprose alt mööda, sest tuuled olid vastu.
5Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
5Ja purjetades üle avamere, mis on Kiliikia ja Pamfüülia kohal, me saabusime Lüükia Mürrasse.
6Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
6Ja kui pealik leidis sealt Aleksandria laeva, mis purjetas Itaaliasse, pani ta meid selle pardale.
7Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
7Aga kui me mitmeid päevi olime vähehaaval edasi purjetanud ja vaevaga saanud Knidose kohale, sest tuul ei lasknud meid lähemale, siis me purjetasime Kreeta varju Salmoone kohal,
8Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo "Bandari Nzuri", karibu na mji wa Lasea.
8loovisime vaevaga sealt mööda ning saabusime paika, mida hüütakse Heaks Sadamaks ja mille lähedal on Lasaia linn.
9Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
9Et aga üsna palju aega oli kulunud ja laevasõit läks juba kardetavaks, kuna ka lepituspäev oli möödas, manitses Paulus neid:
10"Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu."
10'Mehed, ma näen, et edasipurjetamine muutub ohtlikuks ja võib suurt kahju tuua mitte ainult lastile ja laevale, vaid ka meie elule.'
11Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
11Aga pealik võttis kapteni ja tüürimehe nõu enam kuulda kui seda, mida Paulus ütles.
12Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
12Ja et sadam oli talvitamiseks sobimatu, siis võttis enamik nõuks minna sealt merele ja kui võimalik, jõuda talvitama Foiniksisse, sellesse Kreeta sadamasse, mis on lahti edelasse ja loodesse.
13Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
13Kui siis nõrk lõunatuul hakkas puhuma, arvasid nad end eesmärgile jõudvat, hiivasid ankru ja loovisid piki Kreeta rannikut.
14Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao "Upepo wa Kaskazi" ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
14Ent üsna varsti sööstis saare poolt alla marutuul, mida hüütakse kirdemaruks.
15Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
15Kui see laeva kaasa kiskus ja me ei suutnud enam käila vastu tuult keerata, andsime end tuule ajada.
16Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
16Sattudes siis ühe saarekese varju, mida hüütakse Kaudaks, suutsime vaevalt tulla toime päästepaadiga.
17Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
17Kui see oli üles tõmmatud, kasutati kaitsevõtteid ja vöötati laev köitega. Ja et kardeti paiskuda Sürti madalale, heideti sisse triivankur ning jäeti laev triivima.
18Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
18Kui aga raju meid väga vintsutas, loopisid nad järgmisel päeval osa lasti üle parda.
19Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
19Ja kolmandal päeval heitsid nad oma käega merre ka laeva varustuse.
20Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
20Kui nüüd mitu päeva ei paistnud ei päikest ega tähti ja kange raju võimutses, lõppes meil viimaks igasugune lootus pääseda.
21Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, "Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
21Kuna kellelgi ei olnud enam mingit tahtmist süüa, siis tõusis Paulus nende keskel püsti ja ütles: 'Mehed, te oleksite pidanud minu sõna kuulama ja jätma Kreetalt merele minemata, siis te oleksite vältinud seda hädaohtu ja kahju.
22Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
22Nüüd ma aga manitsen teid olema julged, sest ükski hing teie seast ei hukku, hukkub vaid laev.
23Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
23Täna öösel seisis minu juures selle Jumala ingel, kelle päralt ma olen ja keda ma ka teenin,
24akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
24ning ütles: 'Ära karda, Paulus! Sa pead jõudma keisri ette, ja vaata, Jumal on sulle kinkinud kõik su kaasreisijad.'
25Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
25Seepärast, mehed, olge julged, sest ma usun Jumalat, et kõik läheb nõnda, nagu mulle on räägitud.
26Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani."
26Aga me peame jõudma mingile saarele.'
27Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
27Kui siis jõudis kätte neljateistkümnes öö, mil meid Aadria merel aeti sinna ja tänna, siis tundus laevameestele kesköö paiku, et läheneb mingi maa.
28Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
28Loodimisel leidsid nad vett olevat kakskümmend sülda; kui nad siis natuke edasi liikusid ja jälle loodisid, leidsid nad viisteist sülda vett.
29Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
29Kartes, et me paiskume karidele, heitsid nad laeva ahtrist välja neli ankrut ja jäid ootama päevavalgust.
30Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
30Aga kui laevamehed püüdsid laevast põgeneda ja hakkasid paati merre laskma ettekäändel, nagu tahaksid nad laeva käilast ankrut sisse lasta,
31Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, "Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka."
31ütles Paulus pealikule ja sõduritele: 'Kui need ei jää laeva, siis te ei pääse!'
32Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
32Siis raiusid sõdurid paadi köied katki ja lasksid selle merre kukkuda.
33Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: "Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
33Aga enne kui valgeks läks, julgustas Paulus kõiki sööma, üteldes: 'Täna on neljateistkümnes päev, mil te oodates püsite söömata ega ole midagi suhu võtnud.
34Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea."
34Seepärast ma manitsen teid leiba võtma, sest see on tarvilik teie pääsemiseks. Ei lähe ju teie ühegi peast juuksekarvagi kaotsi!'
35Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
35Nende sõnade järel võttis Paulus leiva, tänas Jumalat kõigi ees, murdis ja hakkas sööma.
36Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
36Ja kõigi meeleolu läks paremaks ja nemadki võtsid leiba.
37Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
37Ühtekokku oli meid laeval kakssada seitsekümmend kuus hinge.
38Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
38Kui nende kõhud said täis, siis nad kergendasid veel laeva, heites vilja merre.
39Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
39Kui valgeks läks, siis nad ei tundnud, mis maa see oli; aga nad märkasid ühte sobiva rannaga lahte, kuhu nad tahtsid, kui võimalik, laeva ajada.
40Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
40Nad vabastasid ankrud ja lasksid need merre vajuda, samal ajal nad vallandasid tüüriaerud köitest ja seadsid esipurje tuulde ning püüdsid liikuda ranna poole.
41Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
41Aga nad sattusid liivaseljakule ja ajasid laeva sinna kinni. Laeva käil tungis sinna sisse ja jäi liikumatult paigale, ahter purunes aga lainete möllus.
42Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
42Sõdurid võtsid nõuks vangid ära tappa, et ükski neist ei pääseks ujudes põgenema.
43Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
43Kuid pealik, tahtes päästa Paulust, takistas neid seda nõu täitmast. Ta käskis neil, kes oskavad ujuda, esimestena vette hüpata ja püüda maale jõuda,
44na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.
44ja teistel käskis neile järgneda kas laudadel või laevarusudel. Ja nõnda sündis, et kõik pääsesid tervelt maale.