Swahili: New Testament

Estonian

Acts

7

1Basi, Kuhani Mkuu akamwuliza, "Je, mambo haya ni kweli?"
1Ülempreester küsis: 'Kas see on nõnda?'
2Naye Stefano akasema, "Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
2Aga Stefanos ütles: 'Mehed, vennad ja isad, kuulge! Kirkuse Jumal näitas ennast meie isale Aabrahamile, kui ta oli Mesopotaamias, enne Haaranisse elama asumist,
3Mungu alimwambia: Ondoka katika nchi yako; waache watu wa ukoo wako; nenda katika nchi nitakayokuonyesha!
3ning ütles talle: 'Mine välja oma maalt ja oma sugulaste seast ja siirdu sinna maale, mille ma sulle näitan!'
4Kwa hivyo, Abrahamu alihama nchi ya Kaldayo, akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu alimtoa tena Harani akaja kukaa katika nchi hii mnayokaa sasa.
4Siis ta lahkus kaldealaste maalt ja asus elama Haaranisse. Ja pärast oma isa surma asus ta sealt ümber sellele maale, kus te nüüd elate.
5Mungu hakumpa hata sehemu moja ya nchi hii iwe mali yake; hata hivyo, alimwahidia kumpa nchi hii iwe yake na ya wazawa wake, ingawaje wakati huu hakuwa na mtoto.
5Ja Jumal ei andnud Aabrahamile siin jalatäitki maad pärandiks, ent tõotas selle anda omandiks talle ja ta järglastele - kuigi tal ei olnud last.
6Mungu alimwambia hivi: Wazao wako watapelekwa katika nchi inayotawaliwa na watu wengine, na huko watafanywa watumwa na kutendewa vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
6Jumal rääkis nõnda: Tema järglased elavad võõrana võõral maal ja nad orjastatakse ja neile tehakse kurja nelisada aastat,
7Lakini mimi nitalihukumu taifa hilo litakalowafanya watumwa. Kisha nitawatoa katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.
7ja rahvast, kes nad orjastab, mina karistan, ütles Jumal, ja pärast seda nad lähevad välja ja teenivad mind selles paigas.
8Halafu Mungu aliifanya tohara iwe ishara ya agano. Hivyo, Abrahamu alimtahiri mtoto wake Isaka, siku ya nane baada ya kuzaliwa. Na Isaka, vivyo hivyo, alimtahiri Yakobo. Naye Yakobo aliwatendea wale mababu kumi na wawili vivyo hivyo.
8Ja Jumal andis talle ümberlõikamislepingu. Ja nii sündis talle Iisak ja ta lõikas tema ümber kaheksandal päeval. Ja Iisakile sündis Jaakob, ja Jaakobile need kaksteist peavanemat.
9"Wale mababu walimwonea wivu Yosefu, wakamuuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,
9Ja peavanemad kadestasid Joosepit ja müüsid ta ära Egiptusesse, ent Jumal oli temaga
10akamwokoa katika taabu zake zote. Mungu alimjalia fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri, hata Farao akamweka awe mkuu wa ile nchi na nyumba ya kifalme.
10ja kiskus ta välja kõigist ta viletsustest ning andis talle armu ja tarkust vaarao, Egiptuse kuninga ees, ning see tõstis ta kogu Egiptusemaa ja terve oma koja ülemaks.
11Kisha, kulizuka njaa kubwa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa. Babu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.
11Aga siis tuli nälg kogu Egiptuse- ja Kaananimaale ja suur viletsus ning meie isad ei leidnud toidupoolist.
12Basi, Yakobo alipopata habari kwamba huko Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma watoto wake, yaani babu zetu, waende huko Misri mara ya kwanza.
12Aga kui Jaakob sai kuulda, et Egiptuses on vilja, läkitas ta meie isad sinna esimest korda.
13Katika safari yao ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, na Farao akaifahamu jamaa ya Yosefu.
13Ja teisel korral andis Joosep ennast tunda oma vendadele, ja vaaraole sai teatavaks Joosepi päritolu.
14Yosefu alituma ujumbe kwa baba yake na jamaa yote, jumla watu sabini na tano, waje Misri.
14Siis Joosep laskis kutsuda enda juurde oma isa Jaakobi ja kogu oma suguvõsa, seitsekümmend viis hinge.
15Hivyo, Yakobo alikwenda Misri ambako yeye na babu zetu wengine walikufa.
15Ja Jaakob läks alla Egiptusesse. Ja tema suri seal ja ka meie isad,
16Miili yao ililetwa mpaka Shekemu, ikazikwa katika kaburi Abrahamu alilonunua kutoka kwa kabila la Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
16ja nad viidi Sekemisse ja pandi hauda, mille Aabraham oli hõbeda eest ostnud Hamori laste käest Sekemis.
17"Wakati ulipotimia Mungu aitimize ahadi aliyompa Abrahamu, idadi ya wale watu kule Misri ilikwisha ongezeka na kuwa kubwa zaidi.
17Kui nüüd lähenes selle tõotuse aeg, mille Jumal Aabrahamile oli andnud, kosus rahvas ja kasvas Egiptuses,
18Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.
18kuni tõusis teine kuningas, kes Joosepist midagi ei teadnud.
19Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.
19See tarvitas kavalust meie soo kallal ja tegi kurja meie isadele, nõudes, et nende imikud heidetaks ära, nii et need ei jääks ellu.
20Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,
20Sel ajal sündis Mooses ja ta meeldis Jumalale. Teda kasvatati kolm kuud tema isa kojas.
21na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.
21Aga kui ta oli ära heidetud, siis vaarao tütar lapsendas ta ning kasvatas endale pojaks.
22Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.
22Ja Moosesele õpetati kogu egiptlaste tarkust ja tema oli vägev oma sõnadelt ja tegudelt.
23"Alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.
23Aga kui tal neljakümnes aasta täis sai, tuli tema südamesse mõte minna vaatama oma vendi, Iisraeli lapsi.
24Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri.
24Ja kui ta nägi ühele ülekohut tehtavat, läks ta appi ja maksis kätte selle eest, kellele tehti liiga, lüües egiptlase maha.
25(Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo.)
25Ta arvas, et ta vennad mõistavad, kuidas Jumal tema käe läbi annab neile pääste, aga nad ei mõistnud.
26Kesho yake, aliwaona Waisraeli wawili wakipigana, akajaribu kuwapatanisha, akisema: Ninyi ni ndugu; kwa nini basi, kutendeana vibaya ninyi kwa ninyi?
26Ja järgmisel päeval, sattudes nende juurde, kui nad tülitsesid omavahel, katsus ta neid lepitada ja ütles: 'Mehed, te olete ometi vennad, miks te siis teete teineteisele ülekohut?'
27Yule aliyekuwa anampiga mwenzake alimsukuma Mose kando akisema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wa watu?
27Aga see, kes tegi ligimesele ülekohut, tõukas ta eemale ja ütles: 'Kes sind on tõstnud meile ülemaks ja õigusemõistjaks?
28Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?
28Kas sa tahad ka mind hukata samal kombel, nagu sa eile hukkasid egiptlase?'
29Baada ya kusikia hayo Mose alikimbia, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani na huko akapata watoto wawili.
29Nende sõnade pärast Mooses põgenes ja elas võõrana Midjanimaal, kus talle sündis kaks poega.
30"Miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana alimtokea Mose katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto kule jangwani karibu na mlima Sinai.
30Ja kui nelikümmend aastat sai täis, näitas talle ennast ingel Siinai mäe lähedal kõrbes tuleleegis kibuvitsapõõsas.
31Mose alistaajabu sana kuona jambo hilo hata akasogea karibu ili achungulie; lakini alisikia sauti ya Bwana:
31Mooses imestas seda nägemust nähes, ja kui ta astus lähemale vaatama, kostis Issanda hääl:
32Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Mose akatetemeka kwa hofu na wala hakuthubutu kutazama zaidi.
32'Mina olen sinu isade Jumal, Aabrahami ja Iisaki ja Jaakobi Jumal.' Aga Mooses hakkas värisema ega julgenud enam vaadata.
33Bwana akamwambia: Vua viatu vyako maana hapa unaposimama ni mahali patakatifu.
33Siis ütles Issand talle: 'Võta jalatsid jalast, sest paik, kus sa seisad, on püha maa!
34Nimeyaona mabaya wanayotendewa watu wangu kule Misri. Nimesikia kilio chao, nami nimekuja kuwaokoa. Basi sasa, nitakutuma Misri.
34Ma olen küllalt näinud oma rahva vaevamist Egiptuses ja olen kuulnud nende ägamist ning olen alla tulnud neid vabastama. Ja nüüd mine, ma läkitan su Egiptusesse!'
35"Huyu Mose ndiye yule watu wa Israeli waliyemkataa waliposema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wetu? Kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto, Mungu alimtuma Mose huyo awe kiongozi na mkombozi.
35Sellesama Moosese, kelle nad olid ära salanud, öeldes: 'Kes sind on tõstnud meile ülemaks ja õigusemõistjaks?', selle läkitas Jumal ülemaks ja lunastajaks ingli käe läbi, kes oli ennast talle näidanud kibuvitsapõõsas.
36Ndiye aliyewaongoza wale watu watoke Misri kwa kufanya miujiza na maajabu katika nchi ya Misri, katika bahari ya Shamu na jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
36Seesama Mooses viis nad välja, tehes imetegusid ja tunnustähti Egiptusemaal ja Punases meres ja kõrbes neljakümne aasta jooksul.
37Mose ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: Mungu atawateulieni nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu ninyi wenyewe.
37See on see Mooses, kes ütles Iisraeli lastele: 'Jumal tõstab teie vendade seast teile Prohveti, seesuguse nagu mina.'
38Wakati watu wa Israeli walipokutana pamoja kule jangwani, Mose ndiye aliyekuwako huko pamoja nao. Alikuwa huko pamoja na babu zetu na yule malaika aliyeongea naye mlimani Sinai; ndiye aliyekabidhiwa yale maneno yaletayo uzima atupe sisi.
38Tema on see, kes oli koguduse seas kõrbes koos ingliga, kes kõneles talle Siinai mäel, ja oli koos meie isadega, kes said elavaid sõnu meile edasiandmiseks.
39"Lakini yeye ndiye babu zetu waliyemkataa kumsikiliza; walimsukuma kando, wakatamani kurudi Misri.
39Kuid meie isad ei tahtnud olla talle kuulekad, vaid tõukasid ta eemale ja pöördusid oma südamega Egiptuse poole,
40Walimwambia Aroni: Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata Mose huyu aliyetuongoza kutoka Misri!
40öeldes Aaronile: 'Tee meile jumalaid, kes käiksid meie eel, sest me ei tea, mis on juhtunud selle Moosesega, kes tõi meid välja Egiptusest!'
41Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.
41Ja nad tegid noil päevil vasika ja viisid sellele ebajumalale ohvreid ja rõõmustasid oma käte tegude üle.
42Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii: Enyi watu wa Israeli! Si mimi mliyenitolea dhabihu na sadaka kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani!
42Jumal aga pööras neile selja ning jättis nad teenima taevavägesid, nõnda nagu prohvetite raamatus on kirjutatud: 'Kas teie, Iisraeli sugu, tõite mulle tapa- ja roaohvreid nelikümmend aastat kõrbes olles?
43Ninyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki, na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu. Kwa sababu hiyo nitakupeleka mateka mbali kupita Babuloni!
43Ei, vaid te võtsite Mooloki telgi ja oma jumala Raifa tähe, kujud, mis te olite teinud, et neid kummardada; ja ma asutan teid teisele poole Paabelit.'
44Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema lililoshuhudia kuweko kwa Mungu. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichoonyeshwa.
44Meie isadel oli tunnistustelk kõrbes, nõnda nagu oli seadnud ingel, kes Moosesel käskis selle teha eeskuju järgi, mida ta oli näinud.
45Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.
45Selle telgi võtsid meie isad omaks ja koos Joosuaga tõid selle kaasa nende rahvaste maa vallutamisel, kelle Jumal oli tõuganud eemale meie isade palge eest. Nii see oli Taaveti päevini,
46Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.
46Taavet leidis armu Jumala silmis ja palus, et ta leiaks eluaseme Jaakobi soole.
47Lakini Solomoni ndiye aliyemjengea Mungu nyumba.
47Saalomon ehitas aga temale koja.
48"Hata hivyo, Mungu Mkuu haishi katika nyumba zilizojengwa na binadamu; kama nabii asemavyo:
48Kuid Kõigekõrgem ei ela kätega tehtus, nagu prohvet ütleb:
49Bwana asema: Mbingu ni kiti changu cha enzi na dunia ni kiti changu cha kuwekea miguu.
49'Taevas on mu troon ja maa minu jalajäri. Millise koja teie tahate mulle ehitada?' ütleb Issand.
50Ni nyumba ya namna gani basi mnayoweza kunijengea, na ni mahali gani nitakapopumzika? Vitu hivi vyote ni mimi nimevifanya, au sivyo?
50'Eks minu käsi ole kõik need teinud?!'
51"Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa. Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
51Te kangekaelsed ja ümberlõikamatud südamelt ja kõrvadelt! Teie panete alati vastu Pühale Vaimule, nii nagu teie isad, nõnda teete teiegi.
52Je, yuko nabii yeyote ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua hao Mungu aliowatuma watangaze kuja kwake yule Mwenye Haki. Na sasa, ninyi mmemsaliti, mkamuua.
52Keda prohvetitest teie isad ei ole taga kiusanud? Ja nad on tapnud need, kes kuulutasid ette selle Õige tulemist, kelle reetjaiks ja mõrtsukaiks nüüd olete saanud teie,
53Ninyi mliipokea ile Sheria iliyoletwa kwenu na Malaika, lakini hamkuitii."
53kes te saite Seaduse inglite antud korralduse kaudu, ent ei ole seda pidanud.'
54Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.
54Aga kui nad seda kuulsid, lõikas see neil südamesse ja nad kiristasid hambaid.
55Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
55Stefanos aga, täis Püha Vaimu, vaatas ainiti taevasse ja nägi Jumala kirkust ning Jeesust seismas Jumala paremal käel
56Akasema, "Tazameni! Ninaona mbingu zimefunuliwa na Mwana wa Mtu amesimama upande wa kulia wa Mungu."
56ja ütles: 'Ennäe, ma näen taevaid avanevat ja Inimese Poja seisvat Jumala paremal käel.'
57Hapo, watu wote katika kile kikao cha Baraza, wakapiga kelele na kuziba masikio yao kwa mikono yao. Kisha wakamrukia wote kwa pamoja,
57Selle peale nad karjusid valju häälega ja oma kõrvu kinni hoides sööstsid nagu üks mees tema kallale
58wakamtoa nje ya mji, wakampiga mawe. Wale mashahidi wakayaweka makoti yao chini ya ulinzi wa kijana mmoja jina lake Saulo.
58ja kihutasid ta linnast välja ning viskasid teda kividega. Ja tunnistajad panid oma rõivad maha ühe noormehe jalgade ette, keda kutsuti Sauluseks,
59Waliendelea kumpiga mawe Stefano, huku akiwa anasali: "Bwana Yesu, ipokee roho yangu!"
59ja nad viskasid kividega Stefanost, kes valjusti hüüdis: 'Issand Jeesus, võta mu vaim vastu!'
60Akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa: "Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii." Baada ya kusema hivyo, akafa.
60Ja ta laskus põlvili ning hüüdis suure häälega: 'Issand, ära pane seda neile patuks!' Ja kui ta seda oli öelnud, uinus ta.