1Baadaye, idadi ya wanafunzi ilipokuwa inazidi kuongezeka, kulitokea manung'uniko kati ya wanafunzi waliosema Kigiriki na wale waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigiriki walinung'unika kwamba wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika ugawaji wa mahitaji ya kila siku.
1Aga neil päevil, kui jüngrite arv kasvas, hakkasid kreekakeelsed juudid nurisema heebrea keelt kõnelevate vastu, et igapäevases abiandmises jäetakse nende lesed kahe silma vahele.
2Kwa hiyo, mitume kumi na wawili waliita jumuiya yote ya wanafunzi, wakasema, "Si vizuri sisi tuache kulihubiri neno la Mungu ili tushughulikie ugawaji wa mahitaji.
2Siis kutsusid need kaksteist kokku jüngrite kogu ning ütlesid: 'See ei sobi, et me Jumala sõna kõrvale jättes hoolitseme toidulaudade eest.
3Hivyo, ndugu zetu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema, waliojawa na Roho na wenye hekima; nasi tutawakabidhi jukumu hilo.
3Vennad, vaadake endi seast seitse meest, kellel on hea maine ja kes on täis Vaimu ja tarkust, et me võiksime nemad seada sellesse ametisse.
4Sisi, lakini, tutashughulika na sala na kazi ya kuhubiri neno la Mungu."
4Meie ise aga tahame pühenduda palvetamisele ja sõna teenimisele.'
5Jambo hilo likaipendeza jumuiya yote ya waumini. Wakawachagua Stefano, mtu mwenye imani kubwa na mwenye kujawa na Roho Mtakatifu, Filipo, Prokoro, Nikanora, Timona, Parmena na Nikolao wa Antiokia ambaye hapo awali alikuwa ameongokea dini ya Kiyahudi.
5See kõne meeldis tervele kogukonnale. Ja nad valisid Stefanose, mehe täis usku ja Püha Vaimu, ja Filippuse ja Prokorose ja Nikanori ja Timoni ja Parmenase ja Nikolaose, juudi usku pöördunud antiooklase.
6Wakawaweka mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono.
6Need nad seadsid apostlite ette, ja kui nad palvetasid, panid nad oma käed nende peale.
7Neno la Mungu likazidi kuenea na idadi ya waumini huko Yerusalemu ikaongezeka zaidi, na kundi kubwa la makuhani wakaipokea imani.
7Ja Jumala sõna levis ning jüngrite arv Jeruusalemmas kasvas väga suureks; ka suur hulk preestreid võttis usu omaks.
8Mungu alimjalia Stefano neema tele, akampa nguvu nyingi hata akawa anatenda miujiza na maajabu kati ya watu.
8Aga Stefanos, täis armu ja väge, tegi imetegusid ja suuri tunnustähti rahva seas.
9Lakini watu fulani wakatokea ili wabishane na Stefano. Baadhi ya watu hao walikuwa wa sunagogi moja lililoitwa "Sunagogi la Watu Huru", nao walitoka Kurene na Aleksandria; wengine walitoka Kilikia na Asia.
9Siis tõusid mõned nõndanimetatud vabakslastute ja küreenlaste ja aleksandrialaste sünagoogist ning nende seast, kes on Kiliikia ja Aasia poolt, Stefanosega vaidlema,
10Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyeongoza maneno yake.
10ent ei suutnud vastu seista tarkusele ja Vaimule, kelle läbi tema rääkis.
11Kwa hiyo waliwahonga watu kadhaa waseme: "Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kumkashifu Mose na kumkashifu Mungu."
11Siis nad kihutasid üles mehi ütlema: 'Me oleme kuulnud teda rääkivat teotussõnu Moosese ja Jumala vastu.'
12Kwa namna hiyo, waliwachochea watu, wazee na walimu wa Sheria. Basi, wakamjia Stefano, wakamkamata na kumleta mbele ya Baraza kuu.
12Nad ässitasid rahvast ja vanemaid ja kirjatundjaid ning tulid, võtsid Stefanose kinni ja viisid ta Suurkohtu ette.
13Walileta Barazani mashahidi wa uongo ambao walisema, "Mtu huyu haachi kamwe kusema maneno ya kupakashifu mahali hapa patakatifu na Sheria ya Mose.
13Nad seadsid sinna ka valetunnistajaid, kes ütlesid: 'See inimene ei lakka rääkimast sõnu püha paiga ja Seaduse vastu.
14Kwa maana tulikwisha msikia akisema eti huyo Yesu wa Nazareti atapaharibu kabisa mahali hapa na kufutilia mbali desturi zile tulizopokea kutoka kwa Mose."
14Me oleme kuulnud teda ütlevat, et see Jeesus Naatsaretlane hävitab selle koha ja muudab kombed, mis Mooses meile on pärandanud.'
15Wote waliokuwa katika kile kikao cha Baraza walimkodolea macho Stefano, wakauona uso wake umekuwa kama wa malaika.
15Ja kui kõik Suurkohtus istujad teda ainiti vaatasid, nägid nad tema palge olevat otsekui ingli palge.