1Mtu mmoja aitwaye Anania na mkewe Safira waliuza shamba lao vilevile.
1Aga keegi mees, Hananias nimi, oli koos oma naise Safiiraga müünud omandi
2Lakini, mkewe akiwa anajua, Anania akajiwekea sehemu ya fedha alizopata na ile sehemu nyingine akawakabidhi mitume.
2ja osa saadud rahast naise teades kõrvale toimetanud, ja osa ta tõi ja pani apostlite jalgade ette.
3Basi, Petro akamwuliza, "Anania, mbona Shetani ameuingia moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu kwa kujiwekea sehemu ya fedha ulizopata kutokana na lile shamba?
3Siis ütles Peetrus: 'Hananias, mispärast on saatan vallanud su südame, et sa valetasid Pühale Vaimule ja toimetasid kõrvale osa maatüki eest saadud rahast?
4Kabla ya kuliuza lilikuwa mali yako, na baada ya kuliuza, bado hizo fedha zilikuwa zako uzitumie utakavyo. Kwa nini basi, uliamua moyoni mwako kufanya jambo la namna hii? Hukumdanganya mtu; umemdanganya Mungu!"
4Eks see sinu käes olles olnud su oma ja müüdunagi sinu meelevallas? Mispärast sa oled selle ette võtnud oma südames? Sa ei ole valetanud inimestele, vaid Jumalale.'
5Anania aliposikia hayo, akaanguka chini, akafa. Watu wote waliosikia habari ya tukio hilo waliogopa sana.
5Neid sõnu kuuldes langes Hananias maha ja heitis hinge. Ja suur kartus tuli kõikide peale, kes seda kuulsid.
6Vijana wakafika wakaufunika mwili wake, wakamtoa nje, wakamzika.
6Noormehed aga tõusid ja mässisid ta linasse, kandsid välja ja matsid maha.
7Baada ya muda wa saa tatu hivi, mke wake, bila kufahamu mambo yaliyotukia, akaingia mle ndani.
7Umbes kolme tunni pärast juhtus, et tema naine tuli sisse ega teadnud, mis oli sündinud.
8Petro akamwambia, "Niambie! Je, kiasi hiki cha fedha ndicho mlichopata kwa kuuza lile shamba?" Yeye akamjibu, "Naam, ni kiasi hicho."
8Peetrus küsis temalt: 'Ütle mulle, kas te müüsite maatüki sellise hinnaga?' Tema ütles: 'Jah, selle hinnaga.'
9Naye Petro akamwambia, "Mbona mmekula njama kumjaribu Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale watu waliokwenda kumzika mume wako, sasa wako mlangoni na watakuchukua wewe pia."
9Peetrus ütles nüüd talle: 'Mispärast te olete ühte nõusse heitnud, et Issanda Vaimu kiusata? Ennäe, nende jalad, kes su mehe on matnud, on ukse taga ja nad kannavad välja sinugi.'
10Mara Safira akaanguka mbele ya miguu ya Petro, akafa. Wale vijana walipoingia, walimkuta amekwisha kufa; hivyo wakamtoa nje, wakamzika karibu na mume wake.
10Otsekohe kukkus naine tema jalge ette ja heitis hinge. Ja kui noormehed sisse tulid, leidsid nad ta surnud olevat ning kandsid ta välja ja matsid ta tema mehe kõrvale.
11Kanisa lote pamoja na wote waliosikia habari ya tukio hilo, waliogopa sana.
11Ja suur kartus tuli terve koguduse peale ja kõikide peale, kes seda kuulsid.
12Mitume walifanya miujiza na maajabu mengi kati ya watu. Waumini walikuwa wakikutana pamoja katika ukumbi wa Solomoni.
12Apostlite käte läbi sündis palju tunnustähti ja imetegusid rahva seas, ja nad olid kõik koos ühel meelel Saalomoni sammaskäigus.
13Mtu yeyote mwingine ambaye hakuwa mwamini hakuthubutu kujiunga nao. Hata hivyo, watu wengine wasiokuwa wa imani hiyo waliwasifu.
13Ehkki muudest inimestest ei söandanud keegi nendega lähedalt suhelda, pidas rahvas neist suurt lugu.
14Idadi ya watu waliomwamini Bwana, wanaume kwa wanawake, iliongezeka zaidi na zaidi.
14Seda enam aga lisandus neid, kes uskusid Issandasse, suurel hulgal nii mehi kui naisi,
15Kwa sababu hiyo, watu walikuwa wakipeleka wagonjwa barabarani na kuwalaza juu ya vitanda na mikeka ili Petro akipita, walau kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
15nii et nad kandsid ka haigeid tänavatele ning panid need kanderaamidele ja vooditele, et Peetruse möödudes kas või tema varigi langeks mõne peale neist.
16Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kando kando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.
16Ka Jeruusalemma ümbruse linnade rahvas tuli kokku, tuues haigeid ja rüvedatest vaimudest vaevatuid, kes kõik said terveks.
17Kisha, Kuhani Mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.
17Aga ülempreester ja kõik ta kaaslased, saduseride erakond, muutusid kadedaks
18Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.
18ja pistsid oma käed apostlite külge ning panid nad üldvanglasse.
19Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,
19Issanda ingel avas aga öösel vangimaja uksed, viis nad välja ja ütles:
20"Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu kila kitu kuhusu maisha haya mapya."
20'Minge, seiske ja kõnelge rahvale pühakojas kõik selle elu sõnad!'
21Mitume walitii, wakaingia Hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha. Kuhani Mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu, yaani halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.
21Kui apostlid seda olid kuulnud, tulid nad koidu ajal pühakotta ja hakkasid õpetama.Aga kui ülempreester ja tema kaaslased pärale jõudsid, kutsusid nad kokku Suurkohtu ja kõik Iisraeli rahva vanemad ning läkitasid kohtuteenrid vangimajja apostleid ära tooma.
22Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,
22Kui need nüüd pärale jõudsid, ei leidnud nad apostleid vanglast. Nad pöördusid tagasi ja teatasid:
23wakisema, "Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani."
23'Me leidsime vangimaja küll täiesti kindlalt lukustatuna ja valvurid ustel seismas, aga kui me ukse avasime, ei leidnud seest kedagi.'
24Mkuu wa walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia habari hiyo wakawa na wasiwasi, wasijue yaliyowapata.
24Neid sõnumeid kuuldes olid templipealik ja ülempreestrid nõutud - mis küll võis juhtuda?
25Akafika mtu mmoja, akawaambia, "Wale watu mliowafunga gerezani, hivi sasa wamo Hekaluni, wanawafundisha watu."
25Siis aga saabus keegi, kes teatas neile: 'Ennäe, mehed, kelle teie panite vanglasse, seisavad pühakojas ja õpetavad rahvast!'
26Hapo mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na watu wake walikwenda Hekaluni, akawaleta. Lakini hawakuwakamata kwa kutumia nguvu, maana waliogopa kwamba watu wangewapiga mawe.
26Siis läks templipealik sulastega kaasa ja tõi apostlid ära; aga mitte vägisi, sest nad kartsid, et muidu rahvas viskab nad kividega surnuks.
27Basi, wakawapeleka, wakawasimamisha mbele ya Baraza. Kuhani Mkuu akawaambia,
27Nad tõid siis apostlid ning panid seisma Suurkohtu ette. Ja ülempreester küsis neilt:
28"Tuliwakatazeni waziwazi kufundisha kwa jina la mtu huyu; sasa mmeyaeneza mafundisho yenu pote katika Yerusalemu na mnakusudia kutuwekea lawama ya kifo cha mtu huyo."
28'Eks me ole teid rangelt keelanud õpetamast selle nimel? Ja vaata, te olete Jeruusalemma oma õpetusega täitnud ja tahate selle inimese vere tuua meie peale!'
29Hapo Petro, akiwa pamoja na wale mitume wengine, akajibu, "Lazima tumtii Mungu, na siyo binadamu.
29Peetrus ja teised apostlid kostsid: 'Jumala sõna tuleb enam kuulata kui inimese sõna.
30Mungu wa babu zetu alimfufua Yesu baada ya ninyi kumwua kwa kumtundika msalabani.
30Meie isade Jumal on üles äratanud Jeesuse, kelle teie olete tapnud, riputades ta ristipuu külge.
31Huyu ndiye yule aliyekwezwa na Mungu mpaka upande wake wa kulia, akawa kiongozi na Mwokozi, ili awawezeshe watu wa Israeli watubu, wapate kusamehewa dhambi zao.
31Jumal on just tema oma parema käega ülendanud Juhiks ja Päästjaks, andma Iisraeli rahvale meeleparandust ja pattude andeksandmist.
32Sisi ni mashahidi wa tukio hilo, naye Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii, anashuhudia pia tukio hilo."
32Ja meie oleme kõige selle tunnistajad ning samuti Püha Vaim, kelle Jumal on andnud neile, kes on talle kuulekad.'
33Wajumbe wote wa lile Baraza waliposikia hayo, wakawaka hasira, hata wakaamua kuwaua.
33Kui nad seda kuulsid, lõikas see neile südamesse ja nad tahtsid apostlid hukata.
34Lakini Mfarisayo mmoja aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimika sana mbele ya watu wote, alisimama mbele ya lile Baraza, akataka wale mitume watolewe nje kwa muda mfupi.
34Siis aga tõusis Suurkohtus üles üks variser, Gamaliel nimi, Moosese Seaduse õpetaja, keda kogu rahvas hindas, käskis mehed natukeseks ajaks välja viia
35Kisha akawaambia wale wajumbe wa Baraza, "Wananchi wa Israeli, tahadhari kabla ya kutekeleza hicho mnachotaka kuwatenda watu hawa!
35ning ütles Suurkohtu liikmetele: 'Iisraeli mehed, olge ettevaatlikud nende inimestega, mida te ka tahate teha!
36Zamani kidogo, kulitokea mtu mmoja jina lake Theuda, akajisema kuwa mtu wa maana na watu karibu mia nne wakajiunga naye. Lakini aliuawa, kisha wafuasi wake wote wakatawanyika na kikundi chake kikafa.
36Sest hiljaaegu tõusis Teudas, öeldes enese kellegi olevat, ja tema poole kaldus arvult ligi nelisada meest. Ta hukati ja kõik tema pooldajad hajutati ning neist ei jäänud midagi järele.
37Tena, baadaye, wakati ule wa kuhesabiwa watu, alitokea Yuda wa Galilaya. Huyu naye, aliwavuta watu wakamfuata; lakini naye pia aliuawa, na wafuasi wake wakatawanyika.
37Pärast teda tõusis rahvaloenduspäevil üles galilealane Juudas ja ahvatles rahva enese järel ära taganema. Temagi hukkus ja kõik tema pooldajad pillutati laiali.
38Na sasa pia mimi nawaambieni, msiwachukulie watu hawa hatua yoyote; waacheni! Kwa maana, ikiwa mpango huu au shughuli hii yao imeanzishwa na binadamu, itatoweka yenyewe.
38Ja nüüd ma ütlen teile: Jätke need inimesed rahule ja laske neil olla - sest kui see nõu või tegu on inimestest, siis see läheb tühja,
39Lakini kama imeanzishwa na Mungu, siyo tu kwamba hamtaweza kuwashinda, bali mtajikuta mnapigana na Mungu." Basi, wakakubaliana naye.
39aga kui see on Jumalast, ei suuda teie seda hävitada -, et teist ei saaks sõdijaid Jumala enese vastu!' Nad võtsidki teda kuulda
40Hivyo wakawaita wale mitume, wakaamuru wachapwe viboko na kuwaonya wasifundishe tena kwa jina la Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
40ja kutsusid apostlid sisse, peksid neid ja keelasid neil rääkida Jeesuse nimel ning lasksid nad vabaks.
41Basi, mitume wakatoka nje ya ule mkutano wa halmashauri wakiwa wamejaa furaha, kwani walistahili kuaibishwa kwa ajili ya jina la Yesu.
41Aga nemad läksid Suurkohtu palge eest minema, rõõmustades, et neid on väärt arvatud kannatama teotust selle nime pärast.
42Wakaendelea kila siku kufundisha na kuhubiri Habari Njema ya Kristo, Hekaluni na nyumbani mwa watu.
42Ja nad ei lakanud iga päev pühakojas ja kodasid mööda õpetamast ja kuulutamast evangeeliumi Kristusest Jeesusest.