Swahili: New Testament

Estonian

Colossians

1

1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
1Paulus, Jumala tahtmisel Kristuse Jeesuse apostel, ja vend Timoteos - pühadele, kes on Kolossas, ustavatele vendadele Kristuses:
2tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
2Armu teile ja rahu Jumalalt, meie Isalt [ja meie Issandalt Jeesuselt Kristuselt]!
3Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
3Me täname Jumalat ja meie Issanda Jeesuse Kristuse Isa alati, kui me teie eest palvetame,
4Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
4sest me oleme kuulnud teie usust Kristusesse Jeesusesse ja armastusest kõigi pühade vastu
5Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
5lootuse pärast, mis teile on tallele pandud taevas. Sellest lootusest te olete juba kuulnud evangeeliumi tõesõnas,
6Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
6mis on tulnud teie juurde, nõnda nagu see kogu maailmas on vilja kandmas ja kasvamas. Nii on see ka teie seas sellest päevast peale, mil te kuulsite ja tõeliselt ära tundsite Jumala armu;
7Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
7nõnda nagu te olete õppinud Epafrase, meie armsa kaassulase käest, kes on ustav Kristuse teener teie heaks.
8Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
8See ongi tema, kes meile on teatanud teie armastusest Vaimus.
9Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
9Seepärast ei ole ka meie, sellest päevast peale kui me seda kuulsime, lakanud teie eest palvetamast ega palumast, et teid täidetaks tema tahtmise tundmisega kogu tarkuses ja vaimulikus mõistmises,
10Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
10et te käiksite Issanda vääriliselt talle kõigiti meeldida püüdes, kandes vilja igasuguses heas töös ja kasvades Jumala tundmises
11Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
11ning saaksite vägevaks kogu väega tema kirkuse tugevust mööda kõigeks püsivuseks ja pikaks meeleks, rõõmuga
12Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
12tänades Isa, kes teid on teinud kõlblikuks osa saama pühade pärandist valguse riigis,
13Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
13kes meid on kiskunud välja pimeduse meelevallast ja asetanud oma armsa Poja kuningriiki,
14ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
14kelles meil on lunastus, pattude andeksandmine.
15Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
15Tema on nähtamatu Jumala kuju, kogu loodu esmasündinu,
16Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
16sest tema läbi on loodud kõik, mis on taevais ja maa peal, mis on nähtav ja nähtamatu, olgu troonid või ülemused, olgu valitsused või meelevallad - kõik on loodud tema läbi ja tema poole.
17Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
17Tema ise on enne kõike ja kõik püsib koos temas
18Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
18ja ta on oma ihu, koguduse pea. Tema on algus, esmasündinu surnuist, et ta kõiges saaks esimeseks.
19Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
19Sest Jumalal on olnud hea meel lasta kogu täiusel temas elada
20Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
20ja lepitada tema läbi enesega kõik, niihästi maapealsed kui taevalised, tehes rahu tema ristivere läbi.
21Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
21Ka teid, kes te varem olite Jumalast võõrdunud ja oma mõtlemise poolest tema vaenlased oma kurjade tegudega,
22Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
22on Kristus lepitanud nüüd oma lihalikus ihus surma läbi, et teid seada pühadena ja veatutena ja laitmatutena Jumala palge ette,
23Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
23kui te vaid jääte kindlaks ja rajatuks usule ega lase end kõrvale viia evangeeliumis olevast lootusest, mida te olete kuulnud ja mida on kuulutatud kogu loodule taeva all ja mille teenriks olen saanud mina, Paulus.
24Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
24Nüüd ma rõõmustan oma kannatustes teie pärast, ja oma ihus ma täidan puuduvat osa Kristuse kannatustest tema ihu, see tähendab koguduse heaks,
25Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
25kelle teenriks ma olen saanud Jumala korralduse järgi, mis mu kätte on antud teie heaks, et teile täielikult kuulutada Jumala sõna,
26ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake.
26seda saladust, mis oli varjatud endiste aegade ja sugupõlvede eest, nüüd on aga avaldatud tema pühadele,
27Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
27kellele Jumal tahtis teada anda, mis on selle saladuse kirkuse rikkus kõigi rahvaste seas; see on - Kristus teie sees, kirkuse lootus.
28Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
28Meie kuulutame teda, manitsedes iga inimest ja õpetades iga inimest kogu tarkuses, et seada iga inimest Jumala ette täiuslikuna Kristuses.
29Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.
29Selleks ka mina näen vaeva ja võitlen tema jõu toimel, mis minus on tegev väega.