Swahili: New Testament

Estonian

Colossians

2

1Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
1Ma tahan, et te teaksite, kui suur võitlus on mul teie ja laodikeialaste pärast ning kõikide pärast, kes mind ennast ei ole näinud,
2Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
2et julgustada nende südameid, kes on kokku liidetud armastuses ja täieliku mõistmise kogu rikkuse, Jumala saladuse - Kristuse - tunnetamises,
3Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
3kelles peituvad kõik tarkuse ja tunnetuse aarded.
4Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
4Ma ütlen seda selleks, et keegi teid ei eksitaks ilukõnedega,
5Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
5sest ehk ma küll ihulikult olen eemal, olen ma vaimu poolest ometi teiega, rõõmustades, kui ma näen teie korda ning teie kindlat usku Kristusesse.
6Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
6Nii nagu te nüüd olete Kristuse Jeesuse võtnud vastu Issandaks, nõnda käige temas,
7Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
7olles juurdunud ja ülesehitatud temas ning kinnitatud usus, nõnda nagu teid on õpetatud, ja olge ülevoolavad tänus.
8Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
8Vaadake, et keegi teid ei riisuks tarkuseõpetuse ja tühja pettuse abil, mis vastavad inimeste pärimusele, maailma algainetele, ja mitte Kristusele.
9Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
9Sest temas elab kogu jumalik täius ihulikult,
10nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
10ja teie olete saanud osa tema täiusest, kes on iga valitsuse ja meelevalla pea.
11Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
11Temas te olete ka ümber lõigatud kätega tehtamatu ümberlõikamisega, lihaliku ihu äraheitmisega, Kristuse ümberlõikamisega,
12Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
12kui teid koos temaga ristimises maha maeti ja ka koos temaga üles äratati usu läbi Jumala väesse, kes tema üles äratas surnuist
13Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
13ning teid, kes olite surnud üleastumistes ja oma ihu ümberlõikamatuses - teid on Jumal koos Kristusega elavaks teinud, andestades meile kõik üleastumised,
14alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
14kustutades ära meie võlakirja koos määrustega, mis olid meie vastu, ning selle on ta kõrvaldanud, naelutades selle risti külge.
15Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
15Jumal on paljastanud valitsused ja meelevallad, häbistanud neid avalikult, võidutsedes nende üle Kristuses.
16Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
16Ärgu siis keegi mõistku teie üle kohut sööma või jooma ega mingi püha või noorkuu või hingamispäevade pärast,
17Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
17mis on tulevaste asjade vari, aga Kristuse ihu on tõelisus.
18Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
18Ärgu võtku teie võiduandi ükski, kes seda tahab alandlikkuse ja inglite teenimise kaudu, ja kes selle üle, mis ta on näinud, asjata oma lihalikus mõistuses hoopleb
19na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
19ega hoia kinni peast, kelles kogu ihu kokku liidetakse ja koos hoitakse kõõluste ja sidemete abil, ning kasvab Jumala kasvamist.
20Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
20Kui te koos Kristusega olete maailma algainetele surnud, miks te siis lasete endale teha korraldusi, nagu elaksite alles maailmas:
21"Msishike hiki," "Msionje kile," "Msiguse kile!"
21'Ära hakka kinni! Ära maitse! Ära puuduta!'?
22Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
22See kõik on määratud kuluma kasutamise läbi. Need on vaid inimeste käskimised ja õpetused,
23Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.
23mis on küll tarkuse moodi isetehtud vagaduse ja alandlikkuse ja karmuse tõttu ihu vastu, aga neil ei ole mingit kaalu himude ohjeldamiseks.