1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
1Kui te nüüd koos Kristusega olete üles äratatud, siis otsige seda, mis on ülal, kus Kristus istub Jumala paremal käel;
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
2mõtelge sellele, mis on ülal, mitte sellele, mis on maa peal,
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
3sest te olete surnud ja teie elu on koos Kristusega Jumalas.
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
4Kui Kristus, teie elu, saab avalikuks, siis saate ka teie koos temaga avalikuks kirkuses.
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
5Surmake nüüd need liikmed, mis on maa peal: hoorus, rüvedus, kirg, kuri himu ja ahnus, mis on ebajumalateenistus.
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
6Nende pärast tuleb Jumala viha [sõnakuulmatute laste peale].
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
7Nendes käisite muiste ka teie, kui te elasite selliselt.
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
8Nüüd aga jätke teiegi maha see kõik: viha, raev, kurjus, teotamine, siivutud sõnad oma suust.
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
9Ärge valetage üksteisele, sest te olete seljast võtnud vana inimese tema tegudega
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
10ja olete rõivastunud uude inimesse, kes pidevalt uueneb tunnetama oma Looja näo kohaselt.
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
11Kui see sünnib, siis ei ole enam kreeklast ega juuti, ei ümberlõigatut ega ümberlõikamatut, ei umbkeelset ega sküüti, ei orja ega vaba, vaid kõik ja kõikides on Kristus.
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
12Rõivastuge siis nagu Jumala valitud pühad ja armastatud südamliku kaastundega, lahkusega, alandlikkusega, tasadusega ja pika meelega,
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
13üksteist taludes ja üksteisele andestades, kui kellelgi on teise vastu kaebust. Nii nagu Issand teile on andeks andnud, nõnda tehke teiegi!
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
14Aga üle kõige selle olgu armastus - see on täiuslik side!
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
15Ja teie südameis valitsegu Kristuse rahu, millesse te olete kutsutud ühe ihuna. Ja olge tänulikud!
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
16Kristuse sõna elagu rikkalikult teie seas, kõiges tarkuses õpetage ja manitsege üksteist psalmide, hümnide ja vaimulike lauludega, laulge kogu südamest tänulikult Jumalale!
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
17Ja kõik, mida te iial teete sõnaga või teoga, seda tehke Issanda Jeesuse nimel, tema läbi Jumalat Isa tänades!
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
18Naised, alistuge meestele, nagu on sünnis Issandas!
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
19Mehed, armastage naisi ja ärge olge karmid nende vastu!
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
20Lapsed, olge oma vanemaile kuulekad kõigis asjus, sest see on Issandale meelepärane!
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
21Isad, ärge riielge oma lastega, et nad ei muutuks araks!
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
22Orjad, olge oma maistele isandatele kuulekad kõiges, mitte silmapetteks nagu inimeste ees lipitsemiseks, vaid siira südamega, kartes Issandat.
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
23Mida te iial teete, seda tehke kogu hingest, nõnda nagu Issandale ja mitte nagu inimestele,
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
24teades, et te saate Issandalt palgaks pärisosa. Teenige Issandat Kristust!
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
25Sest kes teeb ülekohut, saab kätte, mis ta on teinud ülekohut, ja ei ole mingit erapoolikust.