Swahili: New Testament

Estonian

Colossians

4

1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
1Isandad, andke orjadele, mis on õiglane ja kohane, teades, et ka teil on isand taevas!
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
2Palvetage püsivalt, valvake tänupalves!
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
3Palvetage ühtlasi ka meie eest, et Jumal avaks meile sõna ukse kuulutada Kristuse saladust, mille pärast ma ju olen ahelais,
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
4et ma seda oskaksin avaldada nõnda, nagu ma pean rääkima.
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
5Käige tarkuses nende ees, kes on väljaspool, kasutades aega õigesti!
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
6Teie kõne olgu alati armu sees, soolaga maitsestatud, et te teaksite, kuidas teil tuleb igaühele kosta.
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
7Kuidas mu käsi käib, küll seda kõike teatab teile Tühhikos, armas vend ning ustav abiline ja kaassulane Issandas,
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
8kelle ma selleks teie juurde saadan, et te teaksite, kuidas minu käsi käib, ja et ta julgustaks teie südameid.
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
9Ma saadan ta koos ustava ja armsa venna Oneesimosega, kes on pärit teie seast. Küll nemad teatavad teile kõik, kuidas lugu siin on.
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
10Teid tervitab Aristarhos, mu vanglakaaslane, ja Markus, Barnabase õepoeg, kelle kohta te olete juba käsu saanud, et kui ta peaks tulema teie juurde, te võtaksite ta vastu;
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
11terviseid Jeesuselt, keda nimetatakse Justuseks. Nemad on ümberlõigatutest olnud ainukesed kaastöölised Jumala riigi heaks, kes on olnud mulle lohutuseks.
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
12Teid tervitab Epafras, kes on pärit teie seast, Kristuse Jeesuse sulane, kes alati võitleb teie eest palvetades, et te püsiksite täiuslikena ja oleksite täidetud kõigega, mis on Jumala tahtmine.
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
13Ma tunnistan temast, et ta kannab väga suurt hoolt teie eest ja nende eest, kes on Laodikeias ja Hierapolises.
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
14Teid tervitavad armas arst Luukas ja Deemas.
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
15Tervitage vendi Laodikeias ning Nümfat ja kogudust tema kojas!
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
16Ja kui see kiri teie juures on ette loetud, siis tehke nii, et seda loetaks ka Laodikeia koguduses ning et teie loeksite ka Laodikeiast tulevat kirja.
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
17Ja öelge Arhipposele: 'Vaata, et sa täidad seda teenimiseametit, mille sa oled saanud Issandas!'
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.
18Tervitus on mu enese, Pauluse käega. Mõtelge mu vangipõlvele! Arm olgu teiega!