1Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
1Seejärel, neljateistkümne aasta pärast, läksin ma taas üles Jeruusalemma koos Barnabasega ning võtsin ka Tiituse kaasa.
2Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
2Ma läksin sinna ilmutuse kohaselt ja kõnelesin neile evangeeliumi, mida ma kuulutan paganate seas; tegin seda eraldi tunnustatud meestele, et ma tühja ei oleks jooksnud ega jookseks.
3Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
3Isegi Tiitust, kes oli minuga, ei sunnitud laskma end ümber lõigata, kuigi ta on kreeklane.
4ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
4Aga sissepugenud valevendade pärast, kes olid kõrvalt tulnud varitsema meie vabadust, mis meil on Kristuses Jeesuses, et meid orjastada,
5Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
5ei andnud me hetkekski järele ega alistunud neile, et teile jääks evangeeliumi tõde.
6Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi--kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje--watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
6Aga need tunnustatud mehed - ükskõik, millised nad olid, Jumal ei pea ju ühest inimesest rohkem lugu kui teisest - jah, tunnustatud mehed ei lisanud mulle midagi juurde.
7Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
7Vastupidi, kui nad nägid, et mulle on usaldatud evangeeliumi kuulutamine ümberlõikamatutele nõnda nagu Peetrusele ümberlõigatutele kuulutamine -
8Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
8sest see, kes tegutseb Peetruse läbi tema apostliametis ümberlõigatute heaks, see tegutseb ka minu läbi paganate heaks -,
9Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
9ja kui Jaakobus ja Keefas ja Johannes, keda peetakse sambaiks, tundsid ära mulle antud armu, siis nad sirutasid parema käe osaduseks mulle ja Barnabasele, et meie mingu paganate juurde, nemad aga ümberlõigatute juurde.
10Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
10Ainult et meil tuleb pidada meeles vaeseid, ja just seda ma olengi hoolega teinud.
11Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
11Aga kui Keefas tuli Antiookiasse, siis ma astusin tema silma ees talle vastu, kuna teda oli tarvis hukka mõista.
12Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
12Sest enne kui mõned olid Jaakobuse juurest tulnud, sõi ta koos paganatega, aga kui need tulid, siis ta tõmbus eemale ja eraldus, kartes ümberlõigatuid.
13Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
13Koos temaga hakkasid silmakirjatsema teisedki juudid, nii et nende silmakirjatsemine tõmbas kaasa ka Barnabase.
14Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: "Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?"
14Kui ma nägin, et nad ei käinud otseteed evangeeliumi tõe järgi, siis ma ütlesin Keefasele kõikide ees: 'Kui sina, kes sa oled juut, elad paganate, aga mitte juudi kombel, kuidas sa siis sunnid paganaid juudi kombeid pidama?
15Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
15Meie oleme sünnilt juudid ega ole patused paganate seast,
16Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
16aga teades, et inimene ei saa õigeks Seaduse tegude kaudu, vaid ainult usu läbi Kristusesse Jeesusesse, siis oleme ka meie uskunud Kristusesse Jeesusesse, et saada õigeks usust Kristusesse ja mitte Seaduse tegude kaudu, sest Seaduse tegude kaudu ei mõisteta õigeks ühtegi inimest.'
17Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
17Kui aga meid meie püüdes saada õigeks Kristuses ometi leitakse patused olevat, kas see tähendab siis, et Kristus on patu teenija? Ei mingil juhul!
18Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
18Sest kui ma ehitaksin jälle üles selle, mille ma olen maha kiskunud, siis ma näitaksin end olevat üleastuja.
19Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
19Sest ma olen Seaduse läbi Seadusele surnud, et elada Jumalale. Ma olen ühes Kristusega risti löödud;
20na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
20nüüd ei ela enam mina, vaid Kristus elab minus. Ja mida ma nüüd elan ihus, seda ma elan usus Jumala Pojasse, kes mind on armastanud ja on iseenese loovutanud minu eest.
21Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!
21Ma ei taha tühistada Jumala armu, sest kui õigus tuleks Seaduse läbi, siis tähendaks see, et Kristus on asjatult surnud.