Swahili: New Testament

Estonian

Hebrews

13

1Endeleeni kupendana kidugu.
1Vennaarmastus jäägu kindlaks!
2Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
2Ärge unustage külalislahkust, sest selle läbi on mõned ise seda aimamata võtnud külalistena vastu ingleid.
3Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
3Pidage meeles vange, nagu te oleksite kaasvangid, ja kurja kannatajaid, sest ka teie olete alles maises ihus.
4Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
4Kõikide juures olgu abielu au sees ja abieluvoodi rüvetamata, sest Jumal nuhtleb hoorajaid ja abielurikkujaid!
5Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa."
5Teie eluviis olgu rahaahnuseta; jääge rahule sellega, mis teil on, sest tema on öelnud: 'Ma ei hülga sind ega jäta sind maha!'
6Ndiyo maana tunathubutu kusema: "Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?"
6Nii võime julgesti öelda: 'Issand on minu abimees, minul ei ole midagi karta, mida võib teha mulle inimene?'
7wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
7Pidage meeles oma juhatajaid, kes teile on rääkinud Jumala sõna; pidades silmas nende elukäigu lõppu, võtke eeskujuks nende usk!
8Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele.
8Jeesus Kristus on seesama eile ja täna ja igavesti!
9Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
9Ärge laske endid õigelt teelt eksitada igasugustel võõrastel õpetustel. On hea, kui süda kinnitatakse armu läbi ja mitte ettekirjutustega toitude kohta, neist ei ole olnud kasu nende täitjatele.
10Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
10Meil on altar, millelt süüa ei ole meelevalda nendel, kes peavad teenistust telgis.
11Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
11Sest nende loomade kehad, kelle vere ülempreester viib ohvriks patu eest kõige pühamasse paika, põletatakse ära väljaspool leeri.
12Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
12Seepärast ka Jeesus, et enese vere läbi pühitseda rahvast, on kannatanud väljaspool väravat.
13Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
13Mingem siis tema juurde väljapoole leeri, kandes tema teotust.
14Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
14Sest meil pole siin jäädavat linna, vaid me taotleme tulevast.
15Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
15Viigem siis tema kaudu alati Jumalale kiitusohvrit, see tähendab tema nime tunnistajate huulte vilja.
16Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
16Ärge unustage teha head ja pidada osadust, sest sellistest ohvritest on Jumalal hea meel!
17Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
17Olge kuulekad oma juhatajaile ja alistuge neile! Nemad ju valvavad teie hingede üle nagu need, kellel tuleb aru anda, et nad teeksid seda tööd rõõmuga, mitte ägades, sest sellest poleks teile kasu!
18Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
18Palvetage meie eest! Me oleme veendunud, et meie südametunnistus on puhas, ja me tahame kõiges käituda hästi.
19Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
19Aga veel enam ma palun seda teha selleks, et mind antaks teile rutem tagasi.
20Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele.
20Aga rahu Jumal, kes igavese lepingu verega on surnuist üles toonud lammaste suure Karjase, meie Issanda Jeesuse,
21Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.
21valmistagu teid kõiges heas tegema tema tahtmist ja saatku korda meie sees, mis on tema silmis meelepärane, Jeesuse Kristuse läbi, kellele olgu kirkus igavesti! Aamen.
22Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
22Vennad, ma kutsun teid üles, võtke heaks see julgustussõna! Ma olen teile ju lühidalt kirjutanud.
23Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
23Teadke, et meie vend Timoteos on lastud vabaks. Temaga koos, kui ta tuleb peatselt, saan minagi teid näha.
24Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
24Tervitage kõiki oma juhatajaid ja kõiki pühasid! Teid tervitavad vennad Itaaliast.
25Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.
25Arm olgu teie kõikidega!