1Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, na dhambi ile inayotung'ang'ania. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
1Seepärast ka meie, kelle ümber on nii suur pilv tunnistajaid, pangem maha kõik koormav ja patt, mis hõlpsasti takerdab meid, ja jookskem püsivusega meile määratud võidujooksu!
2Tumwelekee Yesu ambaye ndiye aliyeianzisha imani yetu na ambaye ataikamilisha. Kwa ajili ya furaha iliyokuwa inamngojea, yeye alivumilia kifo msalabani, bila kujali juu ya aibu yake, na sasa anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
2Vaadakem üles Jeesusele, usu alustajale ja täidesaatjale, kes häbist hoolimata kannatas risti temale seatud rõõmu asemel ja on nüüd istunud Jumala trooni paremale käele.
3Fikirini juu ya mambo yaliyompata Yesu, jinsi alivyostahimili upinzani mkubwa kwa watu wenye dhambi. Basi, msife moyo, wala msikate tamaa.
3Võtke siis eeskujuks teda, kes on kannatanud niisugust patuste vaenu enese vastu, et te ei väsiks ega teie hing ei nõrkeks.
4Maana katika kupambana na dhambi, ninyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu.
4Teie ei ole veel vereni vastu pannud patu vastu võideldes!
5Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja ninyi kuwa wanawe? "Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.
5Ja te olete täiesti unustanud julgustuse, mis teile nagu poegadele ütleb: 'Mu poeg, ära põlga Issanda karistust ja ära nõrke, kui tema sind noomib!
6Maana Bwana humwadhibu kila anayempenda, humpinga kila anayekubali kuwa mwanae."
6Sest keda Issand armastab, seda ta karistab, ta piitsutab iga poega, kelle ta vastu võtab.'
7Vumilieni adhabu kwani ni mafundisho; Mungu huwatendea ninyi kama wanawe. Maana ni mwana gani asiyeadhibiwa na baba yake?
7Kannatused on teile kasvatuseks: Jumal kohtleb teid nagu poegi, sest mis poeg see on, keda isa ei kasvata?
8Lakini msipoadhibiwa kama wana wengine, basi, ninyi si wanawe, bali ni wana haramu.
8Kui te olete ilma kasvatuseta, mille osaliseks on saanud kõik, siis tähendab see, et te olete sohilapsed ja mitte pojad.
9Zaidi ya hayo sisi tunawaheshimu wazazi wetu waliotuzaa hata wanapotuadhibu. Basi, tunapaswa kumtii zaidi Baba yetu wa kiroho ili tupate kuishi.
9Pealegi olid meie lihased isad meile kasvatajaiks ja me pelgasime neid; kas me siis palju enam ei peaks alistuma vaimude Isale, et elada?
10Wazazi wetu hapa duniani walituadhibu kwa muda, kama wao wenyewe walivyoona kuwa vema; lakini Mungu anatuadhibu kwa ajili ya faida yetu wenyewe, tupate kuushiriki utakatifu wake.
10Lihased isad kasvatasid meid ju lühikest aega ja oma äranägemise järgi, aga tema kasvatab meid meie kasuks, et saaksime osa tema pühadusest.
11Kuadhibiwa si jambo la kufurahisha bali la kuhuzunisha. Lakini wale waliofunzwa kuwa na nidhamu mwishowe watavuna tuzo la amani kutoka katika maisha adili!
11Ükski kasvatamine ei tundu samal hetkel olevat rõõm, vaid toob kurvastust; aga hiljem see annab õiguse rahuvilja neile, keda selle varal on harjutatud.
12Basi, inueni mikono yenu inayolegea na kuimarisha magoti yenu yaliyo dhaifu.
12Seepärast tehke jälle tugevaks lõtvunud käed ja jõuetud põlved
13Endeleeni kutembea katika njia iliyonyoka, ili kile kilicholemaa kisiumizwe, bali kiponywe.
13ja õgvendage teerajad oma jalgadele, et lonkur ei väänaks jalga, vaid pigem saaks terveks.
14Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo.
14Taotlege rahu kõikidega ja pühitsust, milleta keegi ei saa näha Issandat,
15Jitahidini sana mtu yeyote asije akapoteza neema ya Mungu. Muwe waangalifu ili mti mchungu usizuke kati yenu na kuwaua wengi kwa sumu yake.
15ja valvake, et keegi ei jääks ilma Jumala armust, et mingi kibe juur üles kasvades ei tooks tüli ning paljud selle läbi ei rüvetuks,
16Jihadharini ili miongoni mwenu pasiwe na mtu mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, aliyeuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mlo mmoja.
16et keegi ei oleks hooraja ega ka kõlvatu nagu Eesav, kes üheainsa kõhutäie eest andis käest oma esmasünniõiguse.
17Ninyi mnafahamu kwamba hata alipotaka kuipata tena ile baraka iliyokuwa yake, alikataliwa, maana hakupata tena nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
17Te ju teate, et kui ta pärastpoole küll tahtis pärida õnnistust, tunnistati ta kõlbmatuks; ta ei leidnud meeleparanduseks kohta, ehk ta küll seda pisaratega otsis.
18Ninyi hamkuwasili mlimani Sinai, ambao unaweza kushikika kama walivyofanya watu wa Israeli, hamkufika kwenye moto uwakao, penye giza, tufani,
18Teie ei ole astunud käega katsutava ja tules põleva mäe ligi, ei sünguse, ei pimeduse, ei raju,
19mvumo wa tarumbeta na sauti ya maneno. Wale waliosikia sauti hiyo waliomba wasisikie tena neno jingine,
19ei pasunahääle ega niisuguse kõne kõla juurde, mille kuuljad palusid, et sellele ei lisataks ühtegi sõna;
20kwani hawakuweza kustahimili amri iliyotolewa: "Atakayegusa mlima huu, hata kama ni mnyama, atapigwa mawe."
20sest nad ei suutnud kanda seda korraldust: 'Kui ka loom peaks puutuma mäe külge, siis visatagu ta kividega surnuks!';
21Hayo yote yalionekana ya kutisha mno, hata Mose akasema, "Naogopa na kutetemeka."
21ja see vaatepilt oli nii õudne, et Mooses ütles: 'Ma olen kabuhirmus ja värisen!' -
22Lakini ninyi mmefika katika mlima wa Sioni, kwenye mji wa Mungu aliye hai. Mmefika Yerusalemu, mji wa mbinguni, ambapo wamekusanyika malaika elfu nyingi wasiohesabika.
22vaid teie olete tulnud Siioni mäe juurde ja elava Jumala linna, taevase Jeruusalemma juurde ja kümnete tuhandete inglite juurde,
23Mmefika kwenye kusanyiko kubwa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mnasimama mbele ya Mungu aliye hakimu wa wote, na mbele ya roho za watu waadilifu waliofanywa kuwa wakamilifu.
23esikpoegade koguduse juurde, kes on kirja pandud taevas, ja Jumala, kõikide kohtumõistja juurde, ja täiuslikuks saanud õigete vaimude juurde,
24Mmefika kwa Yesu ambaye ameratibisha agano jipya, na ambaye damu yake iliyomwagika inasema mambo mema zaidi kuliko ile ya Abeli.
24ja uue lepingu vahemehe Jeesuse juurde, ja piserdamisvere juurde, mis kõneleb paremini Aabeli verest.
25Basi, jihadharini msije mkakataa kumsikiliza yeye ambaye anasema nanyi. Kama wale walikataa kumsikiliza yule aliyewaonya hapa duniani hawakuokoka, sisi tutawezaje kuokoka kama tukikataa kumsikiliza yule anayetuonya kutoka mbinguni?
25Vaadake, et teie ei tõrgu kõnelejat kuulamast! Sest kui ei pääsenud maa peal pakku need, kes tõrkusid kuulamast sõnatoojat, siis palju vähem pääseme meie, kui me pöörame selja temale, kes on taevaist.
26Wakati ule sauti ilitetemesha nchi, lakini sasa ameahidi: "Nitatetemesha nchi tena, lakini si nchi tu bali pia mbingu."
26Tollal pani tema hääl kõikuma maa, aga nüüd on ta tõotanud: 'Veel kord panen ma värisema mitte üksnes maa, vaid ka taeva!'
27Neno hili: "tena" linatuonyesha kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vitatetemeshwa na kutoweka ili vibaki vile visivyotetemeshwa.
27Sõnad 'veel kord' näitavad kõigutatavate kui loodud asjade muutumist, et püsiksid kõigutamatud.
28Sisi basi, na tushukuru kwani tunapokea utawala usiotikisika. Tuwe na shukrani na kumwabudu Mungu kwa namna itakayompendeza, kwa ibada na hofu;
28Olgem siis tänulikud, et me saame kuningriigi, mis ei kõigu, ja teenigem seepärast Jumalat talle meelepäraselt allaheitlikkuse ja aukartusega;
29maana Mungu wetu kweli ni moto mkali unaoteketeza.
29sest meie Jumal on neelav tuli!