Swahili: New Testament

Estonian

Hebrews

11

1Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
1Usk on loodetava tõelisus, nähtamatute asjade tõendus.
2Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
2Selle kohta on ju esivanemad saanud tunnistuse.
3Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana.
3Usus me mõistame, et maailmad on valmistatud Jumala sõna läbi, nii et nägematust on sündinud nähtav.
4Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
4Usus tõi Aabel Jumalale parema ohvri kui Kain, mille tõttu ta sai tunnistuse, et tema on õige, kuna Jumal andis tema andide kohta tunnistuse, ja usu kaudu ta räägib veel surnunagi.
5Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
5Usus võeti ära Eenok, et ta ei näeks surma, ja teda ei leitud enam, sest Jumal oli ta ära võtnud. Aga juba enne, kui ta ära võeti, oli ta saanud tunnistuse, et ta on olnud Jumalale meelepärane.
6Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
6Aga ilma usuta on võimatu olla meelepärane, sest kes tuleb Jumala juurde, peab uskuma, et tema on olemas ja et ta annab palga neile, kes teda otsivad.
7Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
7Usu läbi sai Noa hoiatuse selle kohta, mida veel ei olnud näha, ja ta ehitas jumalakartuses laeva oma pere päästmiseks; ja selle kaudu ta mõistis süüdi maailma ja sai selle õiguse pärijaks, mis tuleb usust.
8Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
8Usus oli Aabraham kuulekas, kui teda kutsuti minema paika, mille ta pidi saama pärandiks, ja ta läks välja, teadmata, kuhu ta läheb.
9Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
9Usus ta asus elama tõotatud maale otsekui võõrsile, elades telkides koos Iisaki ja Jaakobiga, kes olid sellesama tõotuse kaaspärijad.
10Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
10Sest ta ootas kindlale alusele rajatud linna, mille meister ja ehitaja on Jumal.
11Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
11Usus sai isegi Saara väe suguvõsa rajamiseks ja seda eakusest hoolimata, sest ta pidas tõotajat ustavaks.
12Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
12Seepärast ka sündis sellest ühestainsast, pealegi mehejõu kaotanud mehest hulga poolest nii palju järglasi nagu tähti taevas ja nagu liiva mere rannal, mida ei saa ära lugeda.
13Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
13Need kõik surid uskudes, saamata kätte tõotusi, vaid nähes ja tervitades neid kaugelt. Ja nad tunnistasid end olevat võõrad ja majalised maa peal.
14Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
14Kuid kes selliselt kõnelevad, annavad mõista, et nad otsivad kodumaad.
15Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
15Kui nende meeles oleks olnud maa, kust nad olid välja läinud, küllap neil oleks olnud aega pöörduda tagasi.
16Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
16Ent nüüd nad ihkavad paremat, see tähendab taevast kodumaad. Seetõttu ei ole Jumalal nende pärast häbi lasta ennast hüüda nende Jumalaks, kuna ta on valmistanud neile linna.
17Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
17Usus viis Aabraham, kui teda proovile pandi, ohvriks Iisaki; tema, kes oli saanud tõotused, oli valmis ohverdama oma ainusündinu;
18ingawa Mungu alikuwa amemwambia: "Wazawa wako watatokana na Isaka."
18tema, kellele oli öeldud: 'Sinu sugu loetakse Iisakist.'
19Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
19Sest ta arvestas, et Jumal võib ka surnuist üles äratada, seepärast ta saigi tema tagasi ettetähenduseks.
20Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
20Usus õnnistas Iisak ka Jaakobit ja Eesavit tulevaste asjade suhtes.
21Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
21Usus õnnistas surev Jaakob Joosepi mõlemat poega ja kummardas Jumalat oma kepi najal.
22Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
22Usus tuletas Joosep oma elu lõpul meelde Iisraeli laste lahkumist ja andis käsu oma luude kohta.
23Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
23Usus hoidsid Moosese vanemad pärast ta sündimist teda kolm kuud varjul, sest nad nägid ta olevat ilusa lapse ega kartnud kuninga korraldust.
24Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
24Usus keeldus Mooses, kui ta oli saanud suureks, laskmast end nimetada vaarao tütre pojaks.
25Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
25Ta eelistas pigem näha vaeva koos Jumala rahvaga kui üürikest aega nautida pattu,
26Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
26sest Egiptuse aaretest suuremaks rikkuseks pidas ta teotust Kristuse pärast, sest ta tõstis oma silmad tasu poole.
27Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
27Usus jättis ta maha Egiptuse, kartmata kuninga raevu, sest otsekui nähes nähtamatut, püsis ta vaprana.
28Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
28Usus toimetas ta paasat ja vere määrimist uksepiitadele, et hukkaja ei puudutaks nende esikpoegi.
29Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
29Usus läbisid nad Punase mere otsekui kuiva maa, ja kui egiptlased püüdsid teha sedasama, siis nad uppusid.
30Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
30Usus langesid Jeeriko müürid, kui seitse päeva oli käidud nende ümber.
31Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
31Usus ei hukkunud hoor Raahab koos sõnakuulmatutega, sest ta oli rahuga vastu võtnud salakuulajad.
32Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
32Ja mida ma veel ütlen? Mul puudub aeg jutustada Gideonist, Baarakist, Simsonist, Jeftast, Taavetist, Saamuelist ning prohvetitest,
33Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
33kes usu läbi vallutasid kuningriike, mõistsid kohut, said kätte tõotusi, sulgesid lõvide suud,
34Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
34kustutasid tule väe, pääsesid pakku mõõgatera eest, said nõtrusest tugevaks ja vägevaks sõjas, tõrjusid tagasi võõraste vaenuleere.
35Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
35Naised said tagasi oma surnud ülestõusnutena. Ühed lasksid end piinata surnuks, võtmata vastu pakutud vabadust, selleks et saada paremat ülestõusmist.
36Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
36Teised said kogeda pilkamist ja rooska ning ahelaid ja vanglat.
37Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
37Neid on kividega surnuks visatud, pooleks saetud, mõõgaga hukatud, nad on lamba- ja kitsenahas käinud maad mööda ringi, puuduses, viletsuses ja kurja kannatades.
38Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
38Nemad, keda maailm ei olnud väärt, hulkusid ringi kõrbetes ja mägedel ning varjasid end koobastes ja urgudes.
39Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
39Ja kuigi nad kõik said oma usu läbi tunnistuse, ei saanud nad kätte tõotust,
40maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.
40sest Jumal on midagi paremat näinud ette meile, nii et nemad ilma meieta ei saaks täiuslikuks.