Swahili: New Testament

Estonian

Hebrews

7

1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
1Seesama Melkisedek oli ju Saalemi kuningas, Kõigekõrgema Jumala preester, kes tuli vastu Aabrahamile, kui see pöördus tagasi kuningaid löömast, ja õnnistas teda,
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
2kellele ka Aabraham jagas kümnist kõigest, ja kes on, nagu ta nimi esmalt tõlgitakse, 'Õiguse kuningas', siis aga ka Saalemi kuningas, see on 'Rahu kuningas',
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
3isatu, ematu, suguvõsatu, kellel ei ole päevade algust ega elu otsa, aga sarnaselt Jumala Pojaga jääb preestriks jäädavalt.
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
4Vaadake siis, kui suur on see, kellele ka peavanem Aabraham andis kümnist sõjasaagist!
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
5Leevi poegadel, kes saavad preestriameti, on küll käsk võtta Seaduse järgi kümnist rahva, see tähendab oma vendade käest, ehk küll nemadki on lähtunud Aabrahami niuetest.
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
6Aga see, kelle sugu nende sekka ei arvata, võttis kümnist Aabrahami käest ja õnnistas teda, kellel olid tõotused.
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
7Vastuvaidlematult on nii, et alam saab õnnistuse ülemalt.
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
8Ja siin võtavad kümnist surelikud inimesed, seal aga see, kellest tunnistatakse, et ta elab.
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
9Jah, võib isegi öelda, et ka Leevi, kes võttis kümnist, oli ise Aabrahami kaudu maksnud kümnist,
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
10sest ta oli alles esiisa niuetes, kui Melkisedek Aabrahamile vastu tuli.
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
11Kui nüüd täiuslikkus oleks olnud olemas leviitide preestriameti kaudu - selle läbi on rahvas ju saanud Seaduse -, miks oli siis veel vaja esile tõsta teistsugune preester Melkisedeki korra järgi, mitte aga Aaroni korra järgi?
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
12Preestriameti muutmisega sünnib ju paratamatult ka seaduse muutmine.
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
13Sest see, kelle kohta kõike seda öeldakse, on ju teise suguharu liige, kust veel keegi pole teeninud altari juures.
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
14On ju ilmne, et meie Issand on tõusnud Juudast, kelle suguharule Mooses ei ole midagi rääkinud preestriametist.
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
15Ja asi saab veel selgemaks, kui Melkisedeki sarnaselt tõstetakse preestriks üks teine,
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
16kes ei ole preestriks saanud lihaliku käsu Seadust mööda, vaid hävimatu elu väge mööda.
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
17Sest tunnistatakse ju: 'Sina oled igavesti preester Melkisedeki korra järgi.'
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
18Varasem käsk tühistatakse, sest see oli nõder ja kasutu -
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
19Moosese Seadus ei ole ju midagi teinud täiuslikuks -, asemele tuuakse aga hoopis parem lootus, mille kaudu me võime saada Jumala ligi.
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
20Ja niivõrd kui see ei sündinud ilma vandeta - sest leviidid on saanud preestriks vandeta,
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
21Jeesus aga vandega selle kaudu, kes talle ütleb: 'Issand on vandunud ja tema ei kahetse seda: Sina oled igavesti preester' -,
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
22sedavõrd on parem ka leping, mille käemeheks on saanud Jeesus.
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
23Teisi, kes on järjekorras saanud preestriks, on küll palju olnud, sest surm keelas neid selleks jäämast;
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
24Jeesusel on aga selle tõttu, et ta jääb igavesti, muudetamatu preestriamet.
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
25Just seepärast ta võibki päriselt päästa neid, kes tulevad Jumala ette tema läbi, elades aina selleks, et nende eest paluda.
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
26Just selline ülempreester on meile kohane: püha, veatu, laitmatu, patustest lahutatud ja kõrgemaks saanud kui taevad.
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
27Tema ei ole sunnitud teiste ülempreestrite kombel päevast päeva tooma esmalt ohvreid omaenda pattude eest ja alles seejärel rahva pattude eest, sest seda ta on teinud ühe korra ja alatiseks, kui ta ohverdas iseenda.
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.
28Sest Moosese Seadus seab ülempreestreiks inimesed, kes on nõrgad, aga vande sõna, mis on Seadusest hilisem, seab selleks Poja, kes on saanud täiuslikuks igavesti.