1Na sasa sikilizeni enyi matajiri! Lieni na kuomboleza kwa sababu ya taabu zitakazowajieni.
1Kuulge nüüd, rikkad, nutke ja ulguge oma tulevaste hädade pärast!
2Mali zenu zimeoza, na nguo zenu zimeliwa na nondo.
2Teie rikkus on pehkinud ja teie rõivad koitanud,
3Dhahabu yenu na fedha vimeota kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu, nayo itakula miili yenu kama vile moto. Ninyi mmejilundikia mali katika siku hizi za mwisho!
3teie kuld ja hõbe on roostes ning nende rooste saab tunnistuseks teie vastu ja sööb teie liha nagu tuli. Te olete kogunud tagavara viimseil päevil.
4Hamkuwalipa mishahara watumishi waliofanya kazi katika mashamba yenu. Sikilizeni malalamiko yao! Kilio cha hao wanaovuna mashamba yenu kimefika masikioni mwa Bwana, Mwenye Nguvu.
4Vaata, tööliste palk, mille te olete jätnud oma põldudel lõikajatele maksmata, kisendab, ja viljakoristajate karjed on tunginud vägede Issanda kõrvu.
5Mmeishi duniani maisha ya kujifurahisha na ya anasa. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa.
5Te olete priisanud ja prassinud maa peal, nuumanud end tapapäeval,
6Mmemhukumu na kumwua mtu asiye na hatia, naye hakuwapigeni.
6te olete hukka mõistnud õige ja ta mõrvanud. Tema ju ei hakka teile vastu.
7Basi, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapokuja. Tazameni mkulima anavyongoja kwa subira mimea yake itoe mavuno mazuri. Yeye hungojea kwa subira mvua za masika na za vuli.
7Olge nüüd pika meelega, vennad, Issanda tulemiseni! Vaata, põllumees ootab kallist põlluvilja pika meelega, kuni ta saab varase ja hilise vihma.
8Nanyi pia mnapaswa kuwa na subira; imarisheni mioyo yenu, maana siku ya kuja kwake Bwana inakaribia.
8Olge siis teiegi pika meelega, kinnitage oma südant, sest Issanda tulemine on lähedal!
9Ndugu zangu, msinung'unikiane ninyi kwa ninyi msije mkahukumiwa na Mungu. Hakimu yu karibu, tayari kuingia.
9Vennad, ärge nurisege üksteise vastu, et teie üle ei mõistetaks kohut! Vaata, kohtunik seisab ukse ees!
10Ndugu, mkitaka kuona mfano wa subira na uvumilivu katika mateso, fikirini juu ya manabii ambao walinena kwa jina la Bwana.
10Vennad, võtke prohveteid, kes on rääkinud Issanda nimel, kurja kannatamise ja pika meele eeskujuks.
11Tunawaita hao wenye heri kwa sababu walivumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wa Yobu, na mnajua jinsi Bwana alivyomtendea mwishoni. Maana Bwana amejaa huruma na rehema.
11Vaata, me kiidame õndsaks kannatlikke. Te olete kuulnud Iiobi kannatlikkusest ja näinud Issanda antud elulõppu, sest Issand on halastav ja armuline.
12Zaidi ya hayo yote, ndugu zangu, msiape kwa mbingu, wala kwa dunia, wala kwa kitu kingine chochote. Semeni "Ndiyo" kama maana yenu ni ndiyo, na "La" kama maana yenu ni la, na hapo hamtahukumiwa na Mungu.
12Aga ennekõike, mu vennad, ärge vanduge ei taeva ega maa juures ega mingit muud vannet. Teie 'jah' olgu 'jah' ja 'ei' olgu 'ei', et te ei langeks kohtu alla.
13Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa.
13Kui keegi teie seast kannatab kurja, siis ta palvetagu! Kui kellelgi on hea meel, siis ta laulgu tänulaule!
14Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
14Kui keegi teie seast on haige, siis ta kutsugu kogudusevanemad enese juurde ja need palvetagu tema kohal teda õliga võides Issanda nimel.
15Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.
15Ja usupalve päästab tõbise ja Issand tõstab ta üles, ja kui ta on pattu teinud, siis antakse talle andeks.
16Basi, ungamanianeni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.
16Tunnistage siis üksteisele patud üles ja palvetage üksteise eest, et te saaksite terveks! Õige inimese mõjuvõimas eestpalve saadab palju korda.
17Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo mvua isinyeshe, nayo haikunyesha nchini kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita.
17Eelija oli meiesugune inimene, ent ta palvetas püsivalt, et ei sajaks vihma, ning kolm aastat ja kuus kuud ei sadanud piiskagi vihma maa peale.
18Kisha akaomba tena, mvua ikanyesha kutoka angani na nchi ikatoa mazao yake.
18Siis ta palvetas taas ja taevas andis vihma ning maa laskis tärgata oma viljal.
19Ndugu zangu, mmoja wenu akipotoka kuhusu ukweli, na mwingine akamrudisha,
19Mu vennad, kui keegi teist on ära eksinud tõest ning keegi pöörab ta tagasi,
20fahamuni kwamba, huyo anayemrudisha mwenye dhambi kutoka njia yake ya upotovu, ataiokoa roho yake kutoka kifo, na dhambi nyingi zitaondolewa.
20siis ta teadku: see, kes patuse pöörab ta eksiteelt, päästab tema hinge surmast ja katab kinni pattude hulga.