Swahili: New Testament

Estonian

John

2

1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
1Ja kolmandal päeval olid pulmad Galilea Kaanas ja Jeesuse ema oli seal.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
2Ka Jeesus ja ta jüngrid olid kutsutud pulma.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
3Aga kui veinist tuli puudus, ütles Jeesuse ema talle: 'Neil ei ole enam veini.'
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
4Jeesus ütles talle: 'Mis on sul minuga asja, naine? Minu tund ei ole veel tulnud.'
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
5Ta ema ütles teenritele: 'Mida iganes tema teile ütleb, seda tehke!'
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
6Seal oli aga kuus kivianumat juutide puhastuskombe pärast, igaühte võis mahtuda vähemalt sada liitrit.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
7Jeesus ütles neile: 'Täitke anumad veega!' Ja nad täitsid need ääretasa.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
8Ja ta ütles neile: 'Ammutage nüüd ja viige pulmavanemale!' Ja nemad viisid.
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
9Aga kui pulmavanem maitses vett, mis oli muutunud veiniks, ega teadnud, kust see on - teenrid aga, kes olid vee ammutanud, teadsid seda -, siis pulmavanem kutsus peigmehe
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
10ja ütles talle: 'Igaüks paneb esmalt lauale hea veini, ja kui juba küllalt on joodud, lahjema; sina aga oled hoidnud hea veini praeguseni alles.'
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
11See tegu Galilea Kaanas oli esimene tunnustäht, millega Jeesus avaldas oma kirkust, nõnda et ta jüngrid jäid temasse uskuma.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
12Pärast seda läks Jeesus koos oma ema ja vendade ja jüngritega alla Kapernauma ja viibis seal mõned päevad.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
13Juutide paasapühad olid lähedal, ja Jeesus läks üles Jeruusalemma.
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
14Ja ta leidis pühakojas neid, kes müüsid härgi ja lambaid ja tuvisid, ja rahavahetajaid istumas.
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
15Ja ta tegi paeltest piitsa ning ajas pühakojast välja kõik, nii lambad kui härjad, ja ta puistas laiali rahavahetajate mündid ning lükkas kummuli nende lauad
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
16ja ütles tuvimüüjatele: 'Viige need siit minema! Ärge tehke minu Isa koda kaubakojaks!'
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
17Tema jüngritele tuli meelde, et on kirjutatud: 'Kiivus sinu koja pärast neelab mu ära.'
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
18Siis ütlesid juudid Jeesusele: 'Mis tunnustähte sa meile näitad, et sa nõnda tohid teha?'
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
19Jeesus vastas: 'Lammutage see tempel, ja ma püstitan selle kolme päevaga uuesti!'
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
20Siis ütlesid juudid: 'Seda templit on ehitatud nelikümmend kuus aastat, ja sina püstitad selle kolme päevaga uuesti?'
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
21Aga tema mõtles 'templi' all oma ihu.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
22Siis, kui ta oli üles tõusnud surnuist, tuli ta jüngritele meelde, et ta seda oli öelnud, ja nad uskusid kirja ning sõna, mis Jeesus oli öelnud.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
23Aga kui Jeesus oli paasapühadel Jeruusalemmas, hakkasid paljud tema nimesse uskuma, nähes tunnustähti, mida ta tegi.
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
24Kuid Jeesus ise ei usaldanud ennast nende kätte, sest ta tundis inimesi,
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
25ning tal ei olnud tarvis, et keegi oleks andnud tunnistust teise inimese kohta, sest ta teadis, mis oli inimeses.