1Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.
1Aga variseride hulgas oli inimene nimega Nikodeemos, üks juutide ülemaid.
2Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, "Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye."
2Ta tuli ühel ööl Jeesuse juurde ja ütles talle: 'Rabi, me teame, et sa oled Jumala juurest tulnud Õpetaja, sest keegi ei suudaks teha neid tunnustähti, mida sina teed, kui temaga ei oleks Jumal.'
3Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu."
3Jeesus vastas talle: 'Tõesti, tõesti, ma ütlen sulle, kes ei sünni ülalt, ei või näha Jumala riiki.'
4Nikodemo akamwuliza, "Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!"
4Nikodeemos ütles talle: 'Kuidas saab inimene sündida, kui ta on vana? Ega ta saa ju minna tagasi oma ema üska ja teist korda sündida?'
5Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.
5Jeesus vastas: 'Tõesti, tõesti, ma ütlen sulle, kes ei sünni veest ja Vaimust, ei saa minna Jumala riiki.
6Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
6Lihast sündinu on liha, ja Vaimust sündinu on vaim.
7Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.
7Ära imesta, et ma sulle ütlen: Te peate sündima ülalt!
8Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho."
8Tuul puhub, kuhu ta tahab, ja sa kuuled ta häält, kuid ei tea, kust ta tuleb ja kuhu läheb. Niisamuti on kõigiga, kes on sündinud Vaimust.'
9Nikodemo akamwuliza, "Mambo haya yanawezekanaje?"
9Nikodeemos kostis: 'Kuidas see on võimalik?'
10Yesu akamjibu, "Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?
10Jeesus vastas talle: 'Sina oled Iisraeli õpetaja, ja ei tea seda?
11Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.
11Tõesti, tõesti, ma ütlen sulle, meie räägime, mida teame, ja tunnistame, mida oleme näinud, ja ometi ei võta teie meie tunnistust vastu.
12Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?
12Te ei usu mind juba siis, kui ma räägin maistest asjadest, kuidas te usuksite siis, kui ma teile räägiksin taevaseid asju?'
13Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.
13Ja ometi ei ole keegi läinud üles taevasse peale Inimese Poja, kes on tulnud taevast alla.
14"Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,
14Ja nõnda nagu Mooses ülendas kõrbes vaskmao, nõnda peab ülendatama Inimese Poeg,
15ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele.
15et igaühel, kes usub, oleks temas igavene elu.
16Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
16Sest nõnda on Jumal maailma armastanud, et ta oma ainusündinud Poja on andnud, et ükski, kes temasse usub, ei hukkuks, vaid et tal oleks igavene elu.
17Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.
17Jumal ei ole ju läkitanud oma Poega maailma, et ta kohut mõistaks maailma üle, vaid et maailm tema läbi päästetaks.
18"Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.
18Kes temasse usub, selle üle ei mõisteta kohut, ja kes ei usu, selle üle on kohus juba mõistetud, sest ta ei ole uskunud Jumala ainusündinud Poja nimesse.
19Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.
19Ent kohus on see, et valgus on tulnud maailma, aga inimesed on armastanud pimedust enam kui valgust, sest nende teod on kurjad.
20Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.
20Igaüks, kes teeb halba, vihkab valgust ega tule valguse juurde, et ta tegusid ei paljastataks.
21Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu."
21Aga kes teeb tõtt, see tuleb valguse juurde, et ta teod saaksid avalikuks, sest need on tehtud Jumalas.
22Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.
22Pärast seda läks Jeesus oma jüngritega Juudamaale; ta viibis seal koos nendega ja ristis.
23Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
23Ka Johannes oli Ainonis Salimi lähedal, sest seal oli palju vett, ja inimesed tulid sinna ja lasksid end ristida;
24(Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)
24sest Johannest ei olnud veel vangi heidetud.
25Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.
25Siis hakkasid Johannese jüngrid ühe juudiga puhastamiste üle vaidlema.
26Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, "Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea."
26Ja nad tulid Johannese juurde ja ütlesid talle: 'Rabi! See, kes oli sinuga sealpool Jordanit ja kellest sa tunnistasid, vaata, ka see ristib ja kõik lähevad tema juurde.'
27Yohane akawaambia, "Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
27Johannes kostis: 'Keegi ei suuda võtta midagi, kui see ei ole temale antud taevast.
28Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
28Teie ise olete mu tunnistajad, et ma ütlesin, mina ei ole Messias, vaid ainult tema eele läkitatu.
29Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
29Kellel on mõrsja, see on peigmees. Peigmehe sõber seisab aga kõrval ja kuulab teda ning on väga rõõmus peigmehe hääle üle. Nii on nüüd ka minu rõõm saanud täielikuks.
30Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
30Tema peab kasvama, aga mina pean kahanema.'
31"Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
31Kes tuleb ülalt, on üle kõikide. Kes on maast, on maast ja räägib maast. Kes tuleb taevast, on üle kõikide.
32Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
32Tema tunnistab seda, mida on näinud ja kuulnud, ja ometi ei võta keegi tema tunnistust vastu.
33Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
33Tema tunnistuse vastuvõtmine tähendab pitseriga kinnitamist, et Jumal on tõeline.
34Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
34Jah, see, kelle Jumal on läkitanud, räägib Jumala sõnu; Jumal ei anna ju Vaimu mõõdu järgi.
35Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
35Isa armastab Poega ja on andnud tema kätte kõik.
36Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake."
36Kes usub Pojasse, sellel on igavene elu, aga kes ei kuula Poja sõna, see ei näe elu, vaid tema peale jääb Jumala viha.